Tuesday, December 25, 2018

NABII MKUU MHE. DR. GEORDAVIE AMEWATAKA WATU KUTOKUANGALIA MAZINGIRA YANASEMA NINI BALI WAANGALIE KUSUDI LA MUNGU KATIKA MAISHA YAO.





   Jumapili ya tarehe 23.12.018 Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie aliongoza ibada ya jiji katika Chuo Kikuu Cha Manabii Ngurumo Ya Upako Arusha, ambapo ilikuwa ni ibada ya Christmas ya kudhihirisha kusudi la Mungu maishani.

   Akifundisha somo lenye kichwa kisemacho "Usiangalie mazingira bali kusudi la Mungu" Nabii Mkuu amesema kuwa kuna wakati mazingira yanaweza kueleza kitu kingine lakini pia Mungu akawa na kusudi maishani mwako ambapo alimtolea mfano Yesu Kristo na kusema kuwa kuzaliwa kwake katika hori la ng'ombe haikuwa sababu ya kusudi alilokuwa nalo kupotea.
   Aidha Nabii Mkuu amesema kuwa katika maisha kuna vitu vitatu.. Mazingira, Wakati na Kusudi na kuongeza kwamba "Mazingira hukabiliwa na wakati" ikiwa siyo wakati wa Mungu huwezi kulazimisha na pia ikiwa ni wakati wa Mungu huwezi kuuzuia.

   Mbali na hayo Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeoDavie alifungua watu mbalimbali waliofika wakiwa na vifungo vya nguvu za giza, na pia kutamka maneno ya baraka kwa watu wote ili wazidi kuinuka, kubarikiwa, kung'aa na kufanikiwa.

   Pia Nabii Mkuu ametangaza kuwepo tena katika katika hema la kukutania Ngurumo Ya Upako siku ya jumatano ya tarehe 26.12.018 ambapo itakuwa ni ibada ya hitimisho la Siku kuu ya kukusanya (SKYK) ambapo watu wote wametakiwa kufika wakiwa wamefunga pamoja na bajeti zao za mwaka 2019.


    NB: Usisahau ku-download application ya GeorDavie Ministries itakayo kuwezesha kutazama  GeorDavie Tv pamoja na kusikiliza 99.3 N.Y.U Radio.

Monday, December 10, 2018

NABII MKUU MHE. DR. GEORDAVIE AONGOZA IBADA YA MWISHO KWA SILVER PARTNERS.



KUTOKA KATIKA IBADA YA JIJI, CHUO KIKUU CHA MANABII, ILIYOFANYIKA KATIKA HEMA LA KUKUTANIA NGURUMO YA UPAKO, KISONGO, ARUSHA..
Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie aliongoza ibada ya chuo kikuu cha manabii siku ya jana ambapo ilikuwa ni ibada ya Silver Partners ya mwisho kwa mwaka huu wa 2018, ambapo aliweza kutamka baraka mbalimbali kwa wana-Silver Partners wote.

Saturday, October 13, 2018

Waziri Mkuu Aitisha Nyaraka Za Uendeshaji Soko La Kibaigwa.....Ni baada ya wafanyabiashara na mbunge kulalamikia uendeshwaji wake

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wasimamizi na waendeshaji wa Soko la Kimataifa la Mazao Mchanganyiko la Kibaigwa pamoja viongozi wa Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (MVIWATA) kufika ofisini kwake Oktoba 22, 2018 wakiwa na nyaraka zote zinazoonesha uendeshaji wa soko hilo.

Taifa Stars Yapigwa 3-0 Na Cape Verde

Kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars'  jana usiku kimekubali kichapo cha mabao 3-0 kutoka kwa Cape Verde  na sasa kitalazimika kuanza kupiga mahesabu ya mataifa yaliyopo kundi L ili kuona kama kinaweza kufuzu fainali za AFCON 2019 nchini Cameroon.

MAGAZETI YA LEO OCTOBER 13.

JOEL LWAGA Feat CHRIS SHALOM UMEJUA KUNIFURAHISHA OFFICIAL VIDEO

Thursday, September 27, 2018

Kivuko cha MV Nyerere kilichokuwa kimepinduka na kuzama chainuliwa


Kivuko cha MV Nyerere kilichokuwa kimepinduka na kuzama kichwa chini, kimeinuliwa nakuwa wima kama kilivyokuwa hapo awali kabla ya ajali.

Tuesday, June 12, 2018

Anthony Joshua: Deontay Wilder amekubali pigano la kuunganisha mikanda Uingereza

Deontay Wilder kuzipiga na Anthtony Joshua 
Bingwa wa uzani mzito duniani Deontay Wilder anadai kwamba amekubali kuzipiga dhidi ya Anthony Joshua nchini Uingereza

ACT – Wazalendo kuibua mjadala mkuu wa Kitaifa uchambuzi wa bajeti (+video)

Chama cha ACT- Wazalendo kupitia Katibu Kamati ya Uenezi na Mawasiliano ya Umma, Ado Shaibu kimepanga kuja na majadala wa uchambuzi

Viongozi wa dini msiwe na wasemaji ambao sio viongozi – Rais Magufuli (+video)




Vifo vyaongezeka Ajali ya wanafunzi UDSM


Majeruhi mmoja kati ya wawili wa ajali iliyotokea eneo la River Side jijini Dar es Salaam ikihusisha gari la wagonjwa la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam amefariki dunia leo Juni 12, 2018.

Updates: Trump aridhika na mazungumzo pamoja na Kim, Wasaini Makubaliano Maalumu


Rais Donald Trump na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un wamemaliza mazungumzo ya kwanza ya kihistoria kwa kutia saini taarifa juu ya ahadi za kuangamiza silaha za nuklia za Korea Kaskaizni.

Saturday, June 9, 2018

KARIA AWAPA YANGA SAA 48 KUTENGUA KAULI YA KUJITOA KOMBE LA KAGAME, VINGINEVYO…



RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wallace Karia ameutaka uongozi wa klabu ya Yanga kutoa jibu linaloeleweka hadi kufika Jumapili juu ya kujitoa kwao kwenye michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame.
Kauli hiyo ya Karia leo, inafuatia Yanga kuiandikia barua TFF kuwaarifu kutoshiriki michuano hiyo kutokana na kubanwa na ratiba ya mashindano mengine.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya June 9

Waziri Mkuu Ataka Wanaotoa Taarifa Za Uongo Wadhibitiwe

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameliagiza Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi wawachukulie hatua kali wananchi wote wanaotumia vibaya namba za mawasiliano za jeshi hilo kwa kutoa taarifa za uongo kuhusu matukio ya majanga ya moto.

Friday, June 8, 2018

Mfumuko Wa Bei Nchini Waendelea Kupungua Toka Asilimia 3.8 Hadi Asilimia 3.6

Na. Eliphace Marwa – Maelezo
Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) leo imetoa taarifa ya mfumuko wa bei kwa mwezi Mei mwaka huu ambao umepungua hadi kufikia asilimia 3.6 ikilinganishwa na asilimia 3.8 ilivyokuwa kwa mwezi Aprili mwaka huu.

Waziri wa Elimu: Serikali Haitavumilia Walimu Wanaoshiriki Vitendo Vya Udhalilishaji Kwa Wanafunzi

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako Ndalichako ameweka wazi kwamba serikali haiwezi kuvumilia vitendo vya udhalilishaji  ambavyo vimeonekana kufanywa na mwalimu wa shule St. Florence iliyopo jijini Dar es salaam.

Waziri Mkuu Afungua Mkutano Wa Mawaziri Wa Madini Na Kuzindua Maabara Ya Kisasa Ya Madini........Inauwezo wa kutambua aina za madini na yalikotoka

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amezindua maabara ya kisasa ya na ya kwanza barani Afrika yenye uwezo wa kupima na kutambua aina mbalimbali za madini.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya June 8

Mkuu Wa Majeshi Ahamasisha Vijana Kujiunga Jkt Kupata Stadi Za Kazi Ziwasaidie Kujiajiri

Na Stella Kalinga, Simiyu
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi  Jenerali Venance Mabeyo amewahamasisha vijana kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa ili waweze kupata stadi za ufundi na hatimaye wajiajiri badala ya kutegemea kuajiriwa na Serikali.

Thursday, June 7, 2018

Waziri Mkuu: Kutangaza Nyongeza Ya Mishahara Hadharani Kuna Madhara


Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeweka wazi kuwa suala la kutangaza nyongeza za mishahara kwa watumishi wa umma hadharani husababisha athari kwa jamii nzima na kwa wale ambao siyo watumishi.

Waziri Mkuu Asisitiza Kuzichukulia Hatua Asasi Za Kiraia


Mbunge wa Longido (CCM) Dkt. Steven Kiruswa ameitaka Serikali kuyafutia usajili Mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO’s) ambayo huongeza uchochezi nchini kwa kujishughulisha katika masuala ya siasa na hivyo kuhatarisha amani ya watanzania

Wednesday, May 30, 2018

Petroli yasafirishwa kwa chupa kutoka Dar es Salaam hadi Mafia

Vibanda vya kuuza mafuta kama hivi vimekuwa msaada mkubwa kwa wamiliki wa vyombo vya usafiri 
Kisiwani Mafia Tanzania, Mafuta ya petrol na dizeli huuzwa kwa reja reja katika vibanda, huku kukiwa hakuna sheli ya mafuta kwa ajili ya mahitaji ya matumizi ya watu wenye vyombo vya usafiri kisiwani humo.

Walioshtakiwa ulaji rushwa Kenya kukaa rumande wiki moja

Mkurugenzi Mkuu wa NYS Richard Ndubai akiwa mahakamani Jumanne 
Watuhumiwa 24 walioshtakiwa kuhusiana na kashfa ya ufujaji wa pesa katika Shirika la Vijana wa huduma kwa Taifa (NYS) watakaa rumande kwa wiki moja.

Bashiru Ali Kakurwa atangazwa kuwa katibu Mkuu mpya wa CCM

Rais Magufuli na Bashiru Ali Katibu Mkuu mpya wa CCM 
Kamati kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM nchini Tanzania imemteua Dkt. Bashiru Ali Kakurwa kuwa Katibu Mkuu wa Chama hicho.

Lugola Akiri Changamoto Upatikanaji Taarifa Sahihi Za Wazanzibar


Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira imesema changamoto iliyopo katika kupata taarifa sahihi za Wazanzibar wanaopata ajira katika Taasisi za Muungano anuani ya makazi.

Wednesday, May 23, 2018

Rais Trump atilia shaka mkutano adimu na kiongozi wa Korea kaskazini Kim Jong-un

Rais Trump



Rais Trump ametilia shaka kufanyika mkutano adimu na kiongozi wa Korea kaskazini Kim Jong-un mwezi june huko Singapore .

Rwanda kushirikiana na Arsenal kuimarisha utalii

Arsenal kutangaza utalii wa Rwanda




Rwanda imetangaza mpango wa ushirikiano na timu ya Arsenal inayocheza ligi kuu ya England.Ushirikiano huo wa miaka 3 unalenga kuimarisha sekta ya utalii nchini Rwanda,uwekezaji na maendeleo ya mchezo wa soka.

Mahiga: Watanzania Waishio Nje Hutuma Fedha Nyingi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Augustine Mahiga amesema Watanzania waishio nje ya nchi wanatuma zaidi ya Sh trilioni moja nchini kwa mwaka.

Hakuna Mtu Aliyethibitika Kuwa Na Ugonjwa Wa Ebola Na Hakuna Ugonjwa Huu Tanzania


NAIBU Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto dkt. Faustine Ndugulile amethibitisha kuwa hakuna mtu aliyethibitika kuwa na ugonjwa wa EBOLA hapa nchini wala hakuna ugonjwa huo hapa Tanzania.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya May 23

Maofisa Watatu Kituo cha Uwekezaji cha nchini ( TIC ) Wafariki kwa Ajali

Maofisa watatu wa Kituo cha Uwekezaji cha nchini  (Tanzania Investment Center (TIC) wamefariki dunia katika  ajali ya gari usiku wa kuamkia jana Mei 22, 2018 maeneo ya Chalinze wakiwa njiani kuelekea jijini Dodoma.

Tibaijuka: Kwa Hili Serikali ni Lazima Iwajibike.....Utawala wa Sheria Uheshimiwe

Mbunge wa Muleba Kusini(CCM), Profesa Anna Tibaijuka ameitaka serikali ya awamu ya tano iwajibike kuwanunulia ng'ombe wafugaji walioshinda kesi zao Mahakamani kama sheria inavyosema nasio vinginevyo.

Friday, May 18, 2018

Korea Kaskazini na Marekani: Kwa nini Kim Jong-un anamuogopa Donald Trump

Kim Jong-un (L) talking with South Korea's President Moon Jae-in (R) before the inter-Korean summit at the Peace House building on the southern side of the truce village of Panmunjom on 27 April (picture released by North Korean state media)\
Rais wa Marekani Donald Trump ametoa matamshi yanayokinzana na ya mshauri wake wa masuala ya usalama wa taifa, akisema mfumo wa Libya wa kumaliza zana za nyuklia hauwezi kutumiwa nchini Korea Kaskazini.

Trump Amgeuka Mshauri Wake Kuhusu Kuifanya Korea Kaskazini Kama Libya

Rais wa Marekani, Donald Trump amepinga kauli ya mshauri wake mkuu wa masuala ya ulinzi, John Bolton aliyedai kuwa mfumo wa kuondoa silaha za kinyuklia nchini Korea Kaskazini utafanana na uliotumika Libya.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya May 18

Mwakyembe Awataka Vijana kuiga Mfano Wa Flaviana Matata


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe amempongeza mwanamitindo wa kimataifa Bibi. Flaviana Matata kwa juhudi za kusaidia watoto wa kike kupata elimu kwa kuwawezesha  vifaa muhimu vya shule ikiwemo ada na madaftari.

Saturday, May 12, 2018

breaking news:Watu 26 wauawa katika shambulio Burundi

Raia waliokuwa wakiandamana nchini Burundi wakipinga uamuzi wa rais Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu 2015 
serikali ya Burundi inasema kuwa watu 26 wameuawa wakati wa shambulio kaskazini magharibi wa taifa hilo.

KIKOSI CHA SIMBA DHIDI YA SINGIDA UNITED LEO


simba_1wg9iatlvvie114248gh77zh68
Kikosi cha Simba kitakachoanza dhidi ya Singida United, mchezo wa Ligi Kuu Bara

WAAMUZI WAWILI WAONDOLEWA KUCHEZESHA LIGI YA MABINGWA WA MIKOA KWA MCHEZO MCHAFU


Nembo-ya-TFF
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania(TFF) limewaondoa Waamuzi wawili kwenye orodha ya Waamuzi wa Ligi ya Mabingwa wa Mikoa(RCL) inayoendelea kwenye vituo vinne vya Geita,Singida,Rukwa na Kilimanjaro.

SPIKA NDUGAI AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA KATIBU MKUU SEKRETARIETI YA NCHI ZA UKANDA WA MAZIWA MAKUU OFISINI KWAKE MJINI DODOMA


V25A6390

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akisalimiana na mgeni wake Katibu Mkuu wa Sekretarieti ya Nchi za Ukanda wa Maziwa Mkuu Mhe. Onyango kakoba (kulia) alipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.

Waziri Ummy Mwalimu apewa tuzo ya heshima


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM), amepewa tuzo ya heshima na klabu ya soka ya Coastal Union ya jijini Tanga.

Forbes yatangaza watu 10 wenye ushawishi zaidi Duniani


Kiongozi wa China Xi Jinping ndiye mtu mwenye ushawishi Zaidi duniani, kwa mujibu wa jarida la Forbes. Amechukua nafasi hiyo baada ya bunge China kumpa mamlaka zaidi na kuondoa kikomo cha muhula wa rais.

Waziri Mkuu Azuiwa Kusafiri


Waziri Mkuu wa zamani Najib Razak na mkewe Rosmah Mansor wamezuiwa kuondoka nchini, Idara ya Uhamiaji imesema Jumamosi.