Sunday, November 17, 2019

#NENO LA WIKI HII KINABII LATANGAZWA/NABII MKUU KUWEPO TENA JUMAPILI IJAYO/WAGENI HAWA KUHUDHURIA

NABII MKUU TANZANIA MH DKT GEORDAVIE AMETANGAZA KUWA HII NI WIKI YA MAWAZO YAKO KUPATA KIBALI,

NABII MKUU AMETANGAZA NENO HILO HII LEO KATIKA IBADA YA CHUO KIKUU CHA MANABII HEMANI KISONGO ARUSHA AMBAPO ILIKUWA NI IBADA YA KUPATANISHWA NA MADHABAHU.

NA NABII MKUU AMESEMA HIVI

Tuesday, July 9, 2019

Simanzi: Sala ya kuaga miili ya wafanyakazi watano wa Azam Tv yafanyika

Marehemu wafanyakazi wa Azam Tv wamepewa heshima za mwisho


Vilio na simanzi vimetawala katika ofisi za makao makuu ya kampuni ya Azam TV hii leo ambapo wafanyakazi watano wa kampuni hiyo wanaagwa baada ya kufariki kwenye ajali ya barabarani.
Ajali iliyogharimu maisha ya wafanyakazi hao ilitokea Shelui mkoani Singida asubuhi ya Jumatatu Juni 8.

LIVE: RAIS MAGUFULI ANAZINDUA HIFADHI YA TAIFA YA BURIGI

Ambassador 'has PM's full support' despite Trump criticism

Composite image of President Trump and Sir Kim Darroch

Downing Street has reaffirmed its "full support" for the UK's ambassador to the US after Donald Trump said he will no longer work with him.

Makamu Wa Rais Mhe. Samia Ahudhiria Mkutano Wa 12 Wa Dharura Wa Wakuu wa Nchi wa Umoja wa Afrika


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan,  ameshiriki katika Mkutano wa 12 wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika kuhusu Mkataba wa Uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA) unaofanyika jijini Niamey nchini Niger.

Bunge la Tanzania kuwa mwenyeji wa vikao vya Kamati ya Uongozi na ya Bajeti za Chama cha Wabunge wa Nchi za Jumuiya ya Madola–Kanda ya Afrika


Bunge la Tanzania linatarajia kuwa mwenyeji wa vikao vya Kamati ya Uongozi na ya Bajeti za Chama cha Wabunge wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola–Kanda ya Afrika (CPA-AFRICA REGION) vitakavyofanyika tarehe 9 hadi 14, Julai, 2019 katika Ofisi Ndogo za Bunge la Tanzania, Jijini Dar es Salaam.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne 9 July


Upandaji holela wa miti katika njia za umeme Kahama watajwa kusababisha nishati ya umeme kukatika.



Upandaji holela wa miti katika njia kuu za Umeme Wilayani kahama mkoani Shinyanga umetajwa kuchangia kusababisha Nishati hiyo kukatika mara kwa mara kutoka na miti hiyo kugusa nyanya za Umeme.

LIVE | SHUGHULI YA KUWAAGA WAFANYAKAZI WATANO WA AZAM MEDIA WALIOFARIKI ...

Wednesday, July 3, 2019

RASMI IBRAHIM AJIBU MIGOMBA AMEREJEA SIMBA SC KWA MKATABA WA MIAKA MIWILI



KIUNGO mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Ibrahim Ajibu Migomba amesaini mkataba wa miaka miwili kurejea klabu yake ya zamani, Simba SC kutoka kwa mahasimu, Yanga SC.

HOSPITALI YA HAYDOM YANUNUA X RAY MPYA YA KISASA

HOSPITALI ya rufaa ya Haydom Wilayani Mbulu, Mkoani Manyara imenunua mashine mpya ya kisasa ya uchunguzi (X-ray) kwa lengo la kuhudumia wagonjwa wengi, kuongeza ufanisi na kutoa huduma kwa urahisi zaidi.

WIZARA YA VIWANDA YAJIPANGA KUKUZA MASOKO NDANI NA NJE YA NCHI


MAONESHO ya 43 ya biashara maarufu kama sabasaba yenye  kauli mbiu ya usindikaji wa mazao ya kilimo kwa maendeleo ya viwanda yamezinduliwa rasmi leo jijini Dar es Salaam huku masuala ya utafutaji wa masoko pamoja na kuelimimisha wafanyabiashara kuhusiana na kliniki ya biashara yakitiliwa mkazo.

NUNDU APIGA HESABU ZA UBUNGE JIMBO LA TANGA 2020

ALIYEKUWA Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano katika serikali ya awamu ya nne Mhandisi Omari Nundu ametangaza nia ya kuwania Ubunge wa Jimbo la Tanga mwaka 2020 mara baada ya kipenga kutangazwa rasmi. 

Mawaziri Bara, Zanzibar Wasaini Makubaliano ya Ushirikiano



Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe pamoja na Waziri wa Habari, Utalii na Mambo Kale Zanzibar  Mhe. Mahmoud Thabit Kombo na Waziri wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo Balozi Ally Abeid Karume wamesaini makubaliano ya ushirikiano katika kusimamia na kutekeleza sekta za Habari, Utamaduni,Sanaa na michezo ili kuongeza tija.

Hizi hapa Timu 16 zilizotinga hatua ya 16 bora AFCON 2019 Pamoja na Ratiba


Baada ya timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' kupoeza mechi zake zote kwenye kundi C michuano ya Afcon zilizotinga hatua ya 18 hizi hapa na ratiba yake ipo namna hii:-

IGP Sirro Aongoza Kikao Cha Utendaji Cha Maofisa Wakuu Wa Jeshi La Polisi


Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro (katikati), akiongoza Kikao cha Utendaji cha Maofisa Wakuu  wa Makao Makuu ya Polisi jijini Dar es salaam, kujadili utendaji wa kazi za Polisi, kufanya tathmini, Mafanikio, Changamoto na kuweka mikakati ya kutekeleza kazi za Polisi hususan kulinda maisha ya raia na mali zao.

Sunday, June 23, 2019

Taifa Stars kushuka dimbani leo dhidi ya Senegal .....Mchezo Utapigwa Saa Mbili Usiku


Timu yetu ya Tanzania, Stars  leo Jumapili June 23  itachuana na Senegal katika mchezo wa Fainali za Afcon, mechi itakayopigwa saa 2 usiku kwa saa za nyumbani (Tanzania).

Wakala wa CIA anyongwa nchini Iran


Taarifa iliyotolewa na mahakama ya kijeshi nchini Iran inasema adhabu ya kunyongwa hadi kufa aliyopewa jasusi wa CIA na Marekani,Jalal Haji Zevar imetekelezwa katika gereza la Recai Shar lililopo kerec kaskazini magharibi mwa Tehran.

Iran yaionya Marekani na njama zake za kutaka kuishambulia kijeshi nchi hiyo


Image result for IRAN VS MAREKANI
Msemaji wa makao makuu ya jeshi la Iran, Meja Jenerali Ebulfazl Shikarchi amesema shambulizi lolote la kijeshi kutoka kwa Marekani litajibiwa vikali kwa wao kushambulia maslahi ya Marekani katika eneo hilo pamoja na kushambulia washirika wa Marekani.

Katibu Mkuu CCM Dr. Bashiru ahoji maswali Haya kwa wanaosema uchumi wa Tanzania haukui


NA RICH VOICE.
KATIBU wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Taifa ,Bashiru Ally amezindua ujenzi wa ukumbi wa kisasa wa mikutano wa CCM mkoani Pwani,ambapo amechangisha zaidi ya milioni 25 na vifaa mbalimbali.

#LIVE: KUTOKA HEMANI KISONGO IBADA INAENDELEA IKIONGOZWA NA NABII MKUU D...

Wednesday, June 19, 2019

Rais Magufuli Ang’ara Jarida la Forbes.... Aendelea kukubalika Kimataifa


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli, ameendelea kukubalika kimataifa baada ya Jarida maarufu Duniani la Forbes kubashiri kwamba ataivusha Tanzania na kuwa nchi yenye kipato cha kati kupitia ajenda yake ya Tanzania ya viwanda chini ya mpango wa maendeleo wa 2025.

Pierre Liquid A.KA "Konki Fire" Katua Tena Bungeni....Tazama Hapa Akisalimiana na Waziri Mkuu


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Msanii Pierre Liquid kwenye viwanja vya Bunge jijini Dodoma, Juni 19, 2019.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Msanii Pierre Liquid kwenye viwanja vya Bunge jijini Dodoma, Juni 19, 2019.  Wa pili kulia ni Mbunge wa Tunduru Kaskazini, Mhandisi Ramo Makani.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Serikali Kutoa Tamko Rasmi Kuhusu Ugonjwa wa Dengue


Serikali imeeleza kuwa inatarajia kuja na utaratibu mpya wa kutibu ugonjwa wa Dengue ambao umezuka katika baadhi ya mikoa nchini ikiwemo Dar es Salaam na kupelekea vifo kwa baadhi ya watu na wengine kuugua.

DK.MABODI NA UGENI WA FRELIMO

UJUMBE wa Viongozi wa Chama Tawala cha Msumbiji cha FRELIMO wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Chama hicho Ndugu Roque Silva Samuel wakipewa maelezo katika Eneo la Kihistoria alipouawa kwa kupigwa Risasi na Wapinga Maendeleo Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Sheikh Abeid Amani Karume April 7, Mwaka 1972.

POLISI WAMSHIKILIA KIJANA WA MIAKA 19 KWA TUHUMA ZA MAUAJI YA MWANAFUNZI JIJINI DAR

*

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam inamshikilia kijana mweye umri 19 Ernest Joseph kwa tuhuma za mauji ya mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala (KIU) kilichopo Gongolamboto jijini Anifa Mgaya(21).

Tuesday, June 18, 2019

THE MONA SHOW (A Chat With Momo and Wilton Part 2 ) - GeorDavie TV

MAJINI YASHIKA ADABU MBELE YA NABII MKUU ( JIONEE MWENYEWE!!! ) - GeorDa...

THE MONA SHOW (A Chat With Momo and Wilton Part 1) - GeorDavie TV

Breaking News:Lori Lagonga treni Dodoma....Wajeruhiwa 29


Watu 29 wamejeruhiwa baada ya lori kugonga treni jijini Dodoma. Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Protas Katambi amesema leo asubuhi Jumanne Juni 18, 2019 kuwa ajali hiyo imetokea jana saa 5.30 usiku.

Wabunifu wa umeme wa Njombe wakabidhiwa mamilioni yao na Tanesco kisa magufuli .


Shirika la umeme Tanzania Tanesco limewakabidhi kiasi cha shilingi milioni 30 (15mil kila mmoja) wabunifu wawili  wa umeme mkoani Njombe ili ziweze kuwasaidia katika kuboresha miundombinu yao.

Watumishi Saba Wa NIDA wanashikiliwa na jeshi la polisi Kwa Tuhuma Za Wizi Wa Vifaa Na Vitambulisho.



WATUMISHI Saba wa mamlaka ya vitambulisho vya Taifa (NIDA) wanashikiliwa na Jeshi la polisi mkoani Pwani, wakidaiwa kuiba raslimali vifaa vyenye thamani ya sh.mil.15 ambavyo walikuwa wakivichepusha ,kisha kuuza kwa maslahi yao binafsi.


Kati ya watumishi hao walipopekuliwa kwenye makazi yao ,pia walikutwa na vitambulisho vya Taifa boksi moja ambalo ndani vimo vitambulisho 15,000 pamoja na komputa mpakato mbili na nyaya za komputa.

Akielezea juu ya tukio hilo ,kamanda wa polisi mkoani Pwani (ACP) Wankyo Nyigesa alisema ,kati ya watuhumiwa hao wanaodaiwa kufanya tuhuma hizo sita ni wanaume na mmoja mwanamke ambapo majina yao yanehifadhiwa kwa uchunguzi zaidi.

Hata hivyo,kamanda huyo alibainisha,taarifa za tukio hilo zilipokelewa kutoka kwa uongozi wa juu wa NIDA kwenda jeshi la polisi mkoa Juni 14 mwaka huu na mara moja lilifuatilia na kuwakamata watuhumiwa saba na gari T.365 DFS aina ya Toyota spacio rangi ya silver ambayo ilikuwa imebeba jenereta moja mali ya NIDA.

“Awali watumishi wa NIDA waliokuwa wanafanya kazi mkoani hapo walikuwa wanatumia ofisi za kilipokuwa kiwanda cha kubangua korosho TANITA KwaMatias Kibaha na baadae serikali iliwajengea ofisi mpya za kisasa eneo la Machinjioni huko Loliondo Mjini Kibaha.”

“:Baaada ya majengo kukamilika walitakiwa kuhamia katika ofisi hizo mpya wao wenyewe na vitendea kazi vyao kama komputa,meza,scanner,camera,stationaries,BVR kits na vingine”alifafanua Wankyo.

Wankyo alielezea,watumishi wanaoshikiliwa na polisi waliteuliwa na uongozi wa mamlaka hiyo kuhamisha raslimali vifaa kutoka TANITA kwenda Loliondo ambapo wakiwa njiani walikosa uaminifu na kuanza kuvichepusha ,kuviuza na kujipatia pesa kwa manufaa yao binafsi .

Wankyo alitoa rai kwa watumishi wa umma , taasisi na mashirika ya watu binafsi wanapokabidhiwa madaraka na mali za serikali wawe waaminifu ,watiifu kwa kuzilinda kama mboni ya jicho lao na amekemea kuacha ubadhilifu wa mali za umma kwa maslahi ya matumbo yao.

Polisi Kilimanjaro wakamata ndoo 60 za samaki Wachanga .


by RICH VOICE.
Polisi mkoani Kilimanjaro wamekamata ndoo 60 za samaki wanaodaiwa kuvuliwa kinyume cha sheria katika Bwawa la Nyumba ya Mungu wilayani Mwanga  wakiwa wanafirishwa kwenda Arusha.

Sunday, June 16, 2019

Hong Kong protest: 'Nearly two million' join demonstration

The street can no longer be seen beneath the heaving crowd in this shot of a light rail station, the ring and arches of its architecture visible above them


Nearly two million people have taken part in a mass protest in Hong Kong against a controversial extradition bill, organisers say.

Katibu Mkuu wa Maliasili na Utalii atembelea Makumbusho


Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Prof Adolf Mkenda jumamosi tarehe 15 Juni, 2019 alitembelea Makumbusho ya Taifa kujionea urithi na hazina kubwa ya Taifa la Tanzania. Urithi huu wa utamaduni na asili ni pamoja na mafuvu na masalia ya binadamu wa kale au zamadamu, kama Australopithecus afarensis, Zinjanthropus (Paranthropus) boisei, Homo habilis, Homo erectus na Homo sapiens sapiens, yenye umri wa tangu miaka milioni 3.6 had miaka 200,000 iliyopita.

Akiwa Makumbusho ya Taifa, Pof. Mkenda alijadiliana na kuielekeza Menejimenti ya Makumbusho ya Taifa hatua ambazo Wizara ya Maliasili na Utalii inachukua kuimarisha sekta ya malikale na hususan, Shirika la Makumbusho ya Taifa la Tanzania.

“Wizara inaiimarisha na kuijengea uwezo Makumbusho ya Taifa ili itimize majukumu yake ya msingi ya kutafiti, kuhifadhi, kuonesha na kuelimisha umma juu ya urithi wa Taifa na dunia kwa ujumla”.

Prof. Mkenda, aliyasema hayo alipotembelea chumba maalumu cha kuhifadhia mikusanyo adhimu, na kujionea masalia hayo ya binadamu wa kale, hati ya Uhuru wa Tanganyika, tai ya uhuru, kinyago maarufu cha kimakonde na chungu, mchanga na vibuyu halisi vilivyotumiwa na Baba wa Taifa Mwal. Julius K. Nyerere kuchanganya mchanga kama ishara ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 26 Aprili, 1964.

Prof. Mkenda alisema kuwa kufika kwake Makumbusho ya Taifa inadhihirisha kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli imejipambanua na inajali na kuthamini urithi wa Taifa na iko tayari kuulinda urithi huu kwa gharama yoyote kwa sababu ukipotea haupatikani tena.

“Vitu hivi ni muhimu na ni urithi wetu, hivyo tunatakiwa kuvitunza kwa gharama yoyote kwani ni utambulisho wa Taifa la Tanzania, vinaleta amani, mshikamano, uzalendo na furaha. Aidha, vinavutia watalii wa ndani na nje na hivyo kuongeza pato la Taifa”, alisema Prof. Mkenda.

Akizungumza na menejemeti na baadhi ya wataalamu wa Makumbusho ya Taifa Prof. Mkenda ameweka wazi kuridhishwa na uhifadhi na kazi iliyofanywa na Makumbusho ya Taifa kwa kushirikiana na Ofisi ya Usalama wa Majengo ya Serikali ya kukiimarisha chumba hicho maalumu.

Hata hivyo, Katibu Mkuu huyo alimuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa na Menejimenti yake kuimarisha zaidi uhifadhi na ulinzi wa urithi huu wa nchi yetu na dunia kwa ajili ya kizazi cha sasa na kijacho.

Fuvu la Zinjanthropus lenye umri wa miaka milioni 1.75 iliyopita liligunduliwa kwenye bonde la Olduvai, Ngorongoro tarehe 17 July, 1959 na wataalamu wa Akiolojia Dkt. Louis Leakey na mke wake Dkt. Mary Leakey.

Uguduzi huo ulibadilisha uelewa wa wanasayansi kuhusu mchango wa bara la Afrika katika sayansi ya chimbuko la binadamu duniani. Masalia ya Zinjanthropus (Paranthropus) boisei pamoja na masalia mengine ya binadamu wa kale (kama Homo habilis, Homo erectus), zana zao za mawe na masalia ya mifupa ya wanyama waliyokula bonde la Olduvai miaka milioni 2.0-1.0 iliyopita, vinathibitishia dunia kuwa Tanzania ndiyo nchi pekee yenye taarifa bora na sahihi kuhusu chimbuko la binadamu na utamaduni wake (tabia, teknolojia, chakula na namna ya kupata chakula hicho) katika kipindi hicho; na kwamba bonde la Olduvai ndilo Chimbuko la Binadamu wote duniani (the Cradle of Humankind).

Prof. Mkenda ameitaka Makumbusho ya Taifa kuanzisha kampeni ya kutangaza vivutio mbalimbali ambavyo vinapatikana katika makumbusho zetu yakiwemo masalia ya binadamu wa kale.

“Elimu hii na vitu nilivyoviona leo nimefurahi sana, lakini Watanzania wangapi wanavijua? Serikali ya Awamu ya tano inajipambanua kujali na kujivunia vitu vyetu, lugha yetu ya Kiswahili, maliasili zetu, malikale zetu na utamaduni wetu, alisema Prof Mkenda..

Alisema matangazo kwenye luninga, redio na magazeti kuhusu vitu vinavyotunzwa Makumbusho ya Taifa, yatajenga uelewa kwa wananchi juu ya umuhimu wa makumbusho na hivyo, kufanya watu wengi kuja kutembelea makumbusho zetu.

“Msipotangaza hakuna anayewezea kujua kuwa vitu muhimu kama hivi viko hapa Makumbusho ya Taifa, tunatakiwa tuwaambie wananchi ili waje kuviona,” alisisitiza.

Prof. Mkenda alisema, “tunapoelekea kwenye maadhimisho ya miaka 60 tangu kugunduliwa kwa fuvu la Zinjanthropus, fuvu hilo, halitaondolewa Makumbusho ya Taifa kwenda bonde la Olduvai, bali litaendelea kuhifadhiwa na kutunzwa vizuri Makumbusho ya Taifa na badala yake nakala itatumika pale inapohitajika.

Aidha, amesisitiza kuwa matangazo hayo yawe ya ndani na nje ya nchi (International Promotion) kwa sababu kuna watafiti wengi nje ya Tanzania ambao wangependa kuja kufanya utafiti katika Nyanja za akiolojia na paleontolojia.

Sambamba na hilo, aliwaagiza Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Dkt. Freddy Manongi na Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Prof. Audax Mabulla, kuisimamia Kamati inayohusika na maandalizi ya maadhimisho hayo kubuni na kupanga matukio mbali mbali yatakayoleta hamasa katika kuadhimisha miaka 60 ya ugunduzi wa Zinjanthropus na kutangaza vivutio mbalimbali vilivyoko Tanzania.

Alisisitiza kuwa matukio tofauti yaandaliwe kuanzia mwezi Julai mpaka Desemba mwaka huu kama sehemu ya kumbukumbu ya ugunduzi wa fuvu la Zinjanthropus boisei.
 
BY RICH VOICE

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (CDF), Venance Mabeyo Asema dhana ya kulitegemeza Kanisa inatakiwa kufanyika kwa umakini


Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (CDF), Venance Mabeyo amesema dhana ya kulitegemeza Kanisa inatakiwa kufanyika kwa umakini ili lsiathiri shughuli za kiroho za Kanisa Katoliki.

Tanzania Yaungana Na Mataifa Mengine Barani Afrika Wanachama Wa Umoja Wa Afrika Kuadhimisha Wiki Ya Utumishi Wa Umma Kuanzia Leo Juni 16 Hadi 23-2019.


Tanzania inaungana na Mataifa mengine wanachama wa Umoja wa Afrika katika  kuadhimisha wiki ya Utumishi wa Umma barani Afrika   ambayo yameanza leo Jumapili Mwezi Juni 16  ambapo kilele chake itakuwa Juni 23,jijini Nairobi nchini Kenya kwa Bara zima la Afrika. 

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili June 16


Saturday, June 15, 2019

Friday, June 14, 2019

MAJINI YASHIKA ADABU MBELE YA NABII MKUU ( JIONEE MWENYEWE!!! ) - GeorDa...

EMMANUEL MBASHA: “NABII MKUU ANAVYOJUA KUVAA MIMI NAIGA KUTOKA KWAKE” - ...

ZIARA YA RAIS FELIX TSHISEKEDI WA JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA KONGO NCHIN...

Shambulizi la meli ya mafuta katika Ghuba: Iran yasema madai ya Marekani hayana msingi


Iran imesema kuwa imepuuzilia mbali madai ya Marekani kwamba ndio iliotekeleza shambulio dhidi ya meli mbili za mafuta katka Ghuba ya Oman.

Uturuki kulipiza kisasi ikiwekewa vikwazo na Marekani


Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki amesema nchi yake italipiza kisasi dhidi ya uwezekano wowote ule wa Marekani kuiwekea vikwazo nchi yake kutokana na makubaliano yake na Urusi ya kununua mfumo wa kukinga makombora aina ya S-400. 

Tanzania Yapata Heshima Nyingine Kimataifa.....Dkt. Kijazi Ashinda Kwa Kishindo Nafasi Ya Umakamu Wa Tatu Wa Rais Wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO)


Kwa mara nyingine Tanzania imeingia katika historia ya kimataifa kwa Mkurugennzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania na mwakilishi wa kudumu Tanzania katika Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) kuibuka mshindi wa nafasi ya umakamu wa tatu wa Rais wa WMO. Dkt. Kijazi anachukua nafasi hiyo kwa kipindi cha miaka minne kuanzia 2019-2022 akiwa mwanamke wa kwanza na mjumbe wa kwanza kutoka nchi zinazoendelea kushika nafasi hiyo. Dkt. Kijazi atakuwa na majukumu makubwa ya kumsaidia Rais kuongoza shirika hilo katika kutekeleza majukumu yenye tija kwa wanachama wake ikiwemo Tanzania

Hotuba ya Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango akiwasilisha bungeni mapendekezoya Serikali kuhusu makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2019/20


 I.    UTANGULIZI
1.    Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu lipokee, lijadili na kukubali kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka 2019/20. Hii ni bajeti ya nne ya Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Bajeti hii inawasilishwa kwa kuzingatia matakwa ya Ibara ya 137 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ikisomwa pamoja na kifungu cha 26 cha Sheria ya Bajeti namba 11 ya mwaka 2015.

Thursday, June 13, 2019

LIVE: Rais wa DR Congo, Felix Tshisekedi Ikulu Dar es Salaam

Uturuki Kupokea ngao ya makombora ya S-400 ya Urusi Mwezi Ujao


Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amesema serikali yake tayari imenunua mtambo wa kujikinga na makombora kutoka Urusi. 

Wabunifu waliobuni mtambo mdogo wa kufua umeme Wapewa Mamilioni ya Mtaji....Rais Magufuli Atoa Maagizo Mazito TANESCO


Rais John Magufuli ameliijia juu Shirika la umeme nchini (Tanesco) kwa kushindwa kuwaunga mkono wabunifu waliobuni mtambo mdogo wa kufua umeme kwa kutumia maji ya mto Mkoani Njombe, na kuwataka kuwalipa wabaunifu hao fedha watakazozitumia kama kianzio cha kununua vifaa kwaajili ya shughuli zao.

Thamani ya shilingi ya Tanzania yazidi kuimarika


Thamani ya shilingi ya Tanzania imeendelea kuimarika na katika kipindi kinachoishia Aprili 2019, Dola moja ya Marekani ilibadilishwa kwa wastani wa Sh2,300.9 ikilinganishwa na Sh2,270.3 katika kipindi kama hicho mwaka 2018.

Kocha Amunike Apitisha Rungu Taifa Stars Misri....Mastaa 9 Watemwa


BENCHI la Ufundi la Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) likiongozwa na Kocha Mkuu, Emmanul Amunike, raia wa Nigeria limefanya mchujo wa kikosi cha wachezaji watakaoshiriki michuano ya AFCON2019 nchini Misri kutoka achezaji 32 hadi achezaji 23 huku wachezaji 9 wakitemwa.

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA WABUNIFU WADOGO WA MITAMBO YA KUFUA UMEME ...

Iran Yatupiwa Lawama baada ya Wahouthi wa Yemen kuushambulia uwanja wa ndege Saudia


Muungano wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia umeapa kujibu vikali shambulizi la kombora lililofanywa jana na wapiganaji wa Houthi nchini Yemen kwenye uwanja wa kiraia wa ndege kusini mwa Saudia na kuwajeruhi watu 23.

#UNABII: ATEGULIWA TEGO ALILOTEGEWA MUME WAKE AKIPANDA DALADALA NA KUPON...

BUNGE LIVE: 13/06/2019 - Fuatilia kipindi cha maswali na majibu kutoka B...

Rais wa DR Congo, Felix Tshisekedi kutua nchini leo


Rais mpya wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Felix Tshisekedi anatarajiwa kuwasili nchini leo kuanza ziara ya siku mbili.