Tuesday, February 19, 2019

WAPEWA PESA ZA MITAJI MIDOGO...!!


Jumla ya sh. Milioni moja, laki tisa na elfu hamsini (1,950,000) zimetolewa na Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie kwa watu takribani kumi (10) wenye uhitaji wa aina mbalimbali waliojitokeza.
Ni katika ibada ya Chuo Kikuu Cha Manabii iliyofanyika katika hema la kukutania Ngurumo Ya Upako, ambapo Nabii Mkuu aliwataka watu wenye uhitaji wa pesa za kujikimu kujitokeza ambapo watu hao walijitokeza na kuweza kupata Neema hiyo ya kusaidiwa na Nabii Mkuu.
Pia watu wengine tofauti tofauti kwa nyakati tofauti wameweza kufikiwa na neema ya kusaidiwa kifedha na Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie ambapo amekuwa akituma pesa kwa kadiri jinsi Roho Wa Mungu amekuwa akimuongoza kuwasaidia watu hao ambao wamekuwa wakimuelezea uhitaji wao pamoja na hali ngumu wanazopitia kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi kwa kupitia namba ya kunyanyua mikono ya Nabii.
Aidha Nabii Mkuu anatarajia kuwepo siku ya ijumaa katika hema la kukutania Ngurumo Ya Upako, Kisongo, Arusha ambapo itakuwa ni siku ya International Partners (IP) siku ambayo ni maalum kwa wana-International Partners kuwasilisha michango yao kwaajili ya ku-support GeorDavie Tv mikononi mwa Nabii Mkuu.

NB: Usisahau ku-download application ya GeorDavie Ministries itakayo kuwezesha kutazama GeorDavie Tv pamoja na kusikiliza 99.3 N.Y.U Radio

Monday, February 4, 2019

ALIPIWA DENI, KODI NA MTAJI..

"Mungu amenikumbuka, ameniona na amenifuta machozi" ni kauli ambayo ilitolewa na mwanamama aliyesaidiwa na Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie baada ya kulipiwa kodi ya nyumba ya mwaka mzima pamoja na miezi mingine minne aliyokuwa akidaiwa ambapo pia aliongezewa mtaji wa biashara yake.
Mwanamama huyo anayefanya biashara ndogo ndogo alifika akilia mbele ya Nabii Mkuu ambapo alisema kuwa amekimbiwa na mume na kuachiwa watoto wanne, wakiwa wanaishi katika chumba kimoja ambacho alikuwa akidaiwa kodi ya miezi minne pamoja na watoto wake.
Baada ya kujieleza Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie alitoa pesa taslimu na kumkabidhi ili aweze kulipa kodi hiyo aliyokuwa akidaiwa pamoja na kumuongezea nyingine kwa ajili ya mwaka mzima ambapo alimuongezea mtaji wake ili aweze kujikimu na maisha.
Akizungumzia hilo Nabii Mkuu amesema kuwa Serikali Tukufu Ya Ufalme Wa Mungu imeamua kugusa matatizo ya kifedha waliyonayo watu wake ili kuhakikisha shida zinawapungukia na hatimaye kuisha kabisa.
Hayo yamejiri siku ya jana katika ibada ya Chuo Kikuu Cha Manabii, Ngurumo Ya Upako, ambapo ilikuwa ni ibada ya "Kufuta kumbukumbu zote mbaya maishani" ikiongozwa nae Nabii Mkuu.
Akizungumza katika ibada hiyo Nabii Mkuu alisema kumbukumbu mbaya hufanya watu wasipige hatua katika maisha, waishi wakiwa na huzuni pamoja na chuki ambapo alitamka matamko ya Kinabii kwaajili ya kuwatenganisha watu na hali hiyo.
Wakati huo huo Nabii Mkuu anatarajia kuwepo katika kipindi cha "Q and A AKILI KUBWA" siku ya leo kuanzia saa mbili na nusu za usiku, kipindi kitakachoruka kwa kupitia 99.3 N.Y.U Radio pamoja na GeorDavie Tv ambapo jumla ya 2,000,000 (milioni mbili) zitatolewa kwa washindi watakaoweza kujibu maswali kwa ufasaha kabisa.

NB: Usisahau ku-download application ya GeorDavie Ministries itakayo kuwezesha kutazama GeorDavie Tv pamoja na kusikiliza 99.3 N.Y.U Radio.

Sunday, February 3, 2019

ZAIDI YA MILIONI 14 YATOLEWA KWA JAMII- JANUARY..



Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie ametoa zaidi ya sh. 14,490,000 (Milioni kumi na nne, laki nne na elfu tisini), kwa mwezi wa January kama zawadi na misaada kwa watu mbalimbali.
Fedha hizo zimetolewa kwa nyakati tofauti tofauti kwa kupitia vipindi mbalimbali vilivyokuwa vikiruka kupitia 99.3 N.Y.U FM pamoja na GEORDAVIE TV lakini wengine wakiweza kujipatia zawadi zao kwa kupitia ibada za Chuo Kikuu Cha Manabii.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya watu walioweza kujishindia zawadi hizo, wamemshukuru Nabii Mkuu kwa zawadi hizo huku wakieleza pia jinsi ambavyo fedha hizo zimeweza kuwasaidia katika maeneo mbalimbali maishani mwao ikiwa ni pamoja na kutatua matatizo ambayo walikuwa nayo.
Katika mwaka huu wa 2019 ambao ni "Mwaka wa kujenga uwezo" Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie, amesema kuwa hizi ni Zama Mpya ambapo Serikali tukufu ya Ufalme wa Mungu inawagusa watu wenye mahitaji kwa njia ya tofauti ambayo ni ya kuwasaidia kifedha na huu ukiwa muendelezo wa zoezi hilo lililoanza mwishoni mwa mwaka jana na bado likiwa endelevu.

NB: Usisahau ku-download application ya GeorDavie Ministries itakayo kuwezesha kutazama GeorDavie Tv pamoja na kusikiliza 99.3 N.Y.U Radio