Monday, July 13, 2026

MHE. NABII MKUU PROF. GEORDAVIE ATOA KIASI CHA SHILINGI MILIONI 58

Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie leo ametoa kiasi cha shilingi milioni 58 ambapo shilingi milioni 53 ni kwa ajili ya kusapoti maono ya rais wa umoja wa makanisa ya kitume na kinabii tanzania Nabii Dkt. Joshua Mwantyala na shilingi milioni 5 kwa mchungaji hananja.

Ametoa fedha hizo alipokuwa akizungumza na mitume na manabii kupitia kongamano la kurejesha thamani lililofanyika Morogoro katika huduma ya Nabii Dkt. Joshua ambaye pia ndio muandaaji wa kongamano hilo ambapo shilingi miloni 50 ni kwa ajili ya kuendeleza maono, shilingi milioni tatu kwa ajili ya nh’ombe wa maziwa ikiwa ni zawadi ya kumbukizi yake ya siku ya kuzaliwa.

Amempongeza na kufurahishwa na maono yake na kusema kuwa kiasi hicho cha fedha amempa ili zimsaidie kuendeleza maono yake.

MHE. NABII MKUU PROF. GEORDAVIE AWATAKA WATUMISHI WA MUNGU KUWA NA UMOJA NA UPENDO

Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie mlezi wa umoja wa makanisa ya kitume na kinabii amewataka watumishi wa mungu kuwa na umoja na upendo ili mungu aweze kuonekana katika utumishi wao.

Ameyasema hayo jumapili ya July 12, 2026 alipokuwa akizungumza  na watumishi wa mungu, wachungaji, walimu, wainjilisti, mitume na manabii kupitia kongamano la kurejesha thamani lililofanyika Mkoani Morogoro.

Akizungumza Nabii Mkuu amesema kuwa upendo wa kweli unakosekana kwa watumishi ka sababu kuna mafarakano mengi ambayo yanasababisha Mungu asionekane.

Amesema watumishi wa Mungu watakaposhikana mungu ataonekana zaidi na watafanya kazi zaidi katika huduma zao.


Sunday, July 12, 2026

MHE. NABII MKUU PROF. GEORDAVIE AMEMUWEKA WAKFU MTUMISHI WA MUNGU NABII JOSHUA MWANTYALA


Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie amemuweka Wakfu Mtumishi wa Mungu Nabii Joshua Mwantyala ambaye pia ni Rais wa umoja wa makanisa ya kitume na Kinabii Tanzania.

Zoezi hilo amelifanya kupitia siku ya mwisho ya kongamano la siku tatu la kurejesha thamani aliloliandaa mkoani Morogoro ambapo wakfu huo amemuweka kwa kummiminia mafuta yeye kama Madhabahu na kumpokea rasmi kama mtoto wake wa kiroho.

Akimuweka wakfu Nabii Mkuu ametamka ya kuwa majira mapya yanakuja huku akiachilia matamko kwa Nabii Joshua kuwa na baraka za uwepo wa Mungu, Baraka ya ulinzi, baraka ya uongozi ambapo na alimkabidhi kipaza sauti microphone kama baraka ya fimbo kwa musa na kwamba atakapoongea sauti yake itakwenda juu sana kwa nchi na itakuwa na mamlaka yenye utiisho.


WAZIRI DEUS SANGU AWAOMBA WATUMISHI WA MUNGU KUENDELEA KUDUMISHA AMANI YA NCHI


Waziri wa nchi, ofisi ya Waziri mkuu, kazi, ajira na mahusiano ya kazi Deusi Sangu amewaomba watumishi wa mungu waendelee kudumisha umaadili, mshikamano na amani ya nchi.

Ameyasema hayo katika kongamano la kurejesha thamani, lililofanyika Mkoani Morogoro ambalo pia lilikuwa na lengo la kuiombea nchi ambapo ameongeza kuwa serikali inawatambua na kuwathamani watumishi wa mungu.

Amesema katika kuishi dhamira hiyo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani wakati akizindua bunge la 13 aliipa wizara yake jukumu la kuratibu mahusiano baina ya serikali na makundi ya kijamii ambapo uratibu huo unahusisha wadau wa siasa, taasisi za dini, Asasi za Kiraia na mashirika yasiyo ya kiserikali na kwamba wanafanya kazi na wadau hao wote kwa karibu ili kuhakikisha wanaimarisha amani, utulivu upendo, mshikamano na maridhiano ya kitaifa.

Amesema mambo hayo ndio nguzo kuu na mahusiano na dhamira ya maendeleo ya taifa ya mwaka 2026.


TAZAMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO JULAI 13, 2026

 















Wednesday, July 8, 2026

MAREKANI YAANZISHA UPYA MASHAMBULIZI NCHINI IRAN


Marekani imefanya mashambulizi mapya ya anga dhidi ya Iran mapema leo, hatua iliyojibiwa na Iran kwa kuyalenga mataifa ya Bahrain, Kuwait na Qatar. Hali hii inaongeza mvutano na kuhatarisha tena makubaliano ya muda yaliyolenga kutafuta njia ya kumaliza vita.

Jeshi la Marekani lilishambulia maeneo mbalimbali ya kijeshi na miundombinu ya bandari mapema Jumatano, kufuatia mashambulizi ya Iran dhidi ya meli kadhaa za biashara katika pwani ya Oman, hali iliyosababisha Iran kujibu kwa mashambulizi mengine.

Mashambulizi ya Marekani yalifanywa saa chache baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kusema makubaliano hayo yamefika mwisho kufuatia mashambulizi hayo ya Iran.

Hata hivyo, mashambulizi ya Alhamisi yalionekana kuwa makubwa zaidi kuliko ya awali huku Jeshi la Kuwait likisema limezuia na kudungua droni pamoja na makombora yaliyoelekezwa nchini humo.

Vyombo vya habari vya serikali ya Iran viliripoti milipuko katika maeneo kadhaa, yakiwemo Bushehr, ambako kuna kituo cha nishati ya nyuklia cha Iran, pamoja na miji ya bandari ya kusini ya Chabahar, Konarak, Bandar Abbas na Sirik.

Chanzo: DW

WAIRAN KUMZIKA AYATOLLAH ALI KHAMENEI NYUMBANI KWAKE MASSHAD

Raia nchini Iran hii leo wanajiandaa kumzika kiongozi wao Ali Khamenei, katika mji alikozaliwa wa Mashhad, huku mashambulizi mapya ya Marekani yakitishia kusababisha ongezeko jipya la mvutano.

Mazishi ya kiongozi huyo mkuu wa zamani yanafuatia ibada za maombolezo zilizodumu kwa siku kadhaa na kuhudhuriwa na mamilioni ya waombolezaji katika miji mbalimbali nchini Iran na Iraq.

Ali Khamenei aliuawa Februari 28, siku ya kwanza ya mashambulizi ya Marekani na Israel nchini Iran yaliyochochea vita hivyo.

Baada ya maandamano makubwa ya mazishi yaliyopita katika miji mitakatifu ya Najaf na Karbala nchini Iraq siku ya Jumatano, mwili wake ulitarajiwa kufikishwa katika makazi yake ya mwisho katika mji mtakatifu wa Mashhad.

Gavana wa Mashhad, Hassan Hosseini alinukuliwa na televisheni ya serikali akisema kuwa "anatarajia watu milioni 15” kuhudhuria mazishi hayo ya Khamenei.

Chanzo: DW


MANCHESTER UNITED YAANGUKIA KWA ANDREY SANTOS BAADA YA KUMKOSA MATEUS FERNANDES


Klabu ya Manchester United imefikia makubaliano na Chelsea juu ya kumsajili kiungo, Andrey Santos kwa ada ya uhamisho ya Euro milioni 56 pamoja na nyongeza ya Euro milioni 2.4 huku Chelsea akipachika kifungu cha asilimia 10 za mauzo ya siku za usoni.

Santos 22, raia wa Brazil tayari amefikia makubaliano ya maslahi binafsi na mashetani hao Wekundu na tayari amepata ruhusa ya kufanya vipimo vya afya kabla ya kukamilika uhamisho huo.

Mashetani hao Wekundu ambao pia wanatarajiwa kumtangaza, Mbrazil mwingine, Ederson kama mchezaji mpya walilazimika kutafuta kiungo mwingine kwa ajili ya kurithi mikoba ya Casemiro ikiwa ni baada ya kuangukia pua katika jitihada zao za kuinasa saini ya Mateus Fernandes aliyetimkia Tottenham Hotspur.

TAZAMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO JULAI 09, 2026