Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie leo ametoa kiasi cha shilingi
milioni 58 ambapo shilingi milioni 53 ni kwa ajili ya kusapoti maono ya rais wa
umoja wa makanisa ya kitume na kinabii tanzania Nabii Dkt. Joshua Mwantyala na
shilingi milioni 5 kwa mchungaji hananja.
Ametoa fedha hizo alipokuwa akizungumza na mitume na manabii
kupitia kongamano la kurejesha thamani lililofanyika Morogoro katika huduma ya Nabii
Dkt. Joshua ambaye pia ndio muandaaji wa kongamano hilo ambapo shilingi miloni
50 ni kwa ajili ya kuendeleza maono, shilingi milioni tatu kwa ajili ya nh’ombe
wa maziwa ikiwa ni zawadi ya kumbukizi yake ya siku ya kuzaliwa.
Amempongeza na kufurahishwa na maono yake na kusema kuwa
kiasi hicho cha fedha amempa ili zimsaidie kuendeleza maono yake.
%20Facebook.png)
%20Facebook.png)
%20Facebook.png)























































