Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Luanda, Angola ambapo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla ya Uzinduzi wa Hospitali iliyopewa jina la Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, tarehe 31 Julai.
Friday, July 31, 2026
Thursday, July 30, 2026
Wednesday, July 29, 2026
Tuesday, July 28, 2026
DAGLO ASEMA WAPIGANAJI WAKE "HURU SASA" KUPAMBANA NA JESHI
Mkuu wa
wanamgambo wa RSF nchini Sudan Mohamed Hamdan Daglo amewaambia wapiganaji wake
kuwa "wameachiliwa huru" sasa kupambana na jeshi la nchi hiyo.
Ujumbe huu wa
Daglo kwa wapiganaji wake ambao wametuhumiwa kwa mauaji ya kimbari unakuja siku
moja baada ya kupoteza udhibiti wa barabara moja kuu kati ya Mji Mkuu Khartoum
na mji mkubwa wa eneo la Kordofan wa El-Obeid.
Kwa wiki
kadhaa sasa Umoja wa Mataifa umeonya kuwa huenda wapiganaji wa RSF
wakasababisha mauaji makubwa katika eneo la Kordofan, wakati wanapotafuta
kuuzingira mji wa El-Obeid kuelekea uvamizi mkubwa wanaotazamia kuufanya.
Wafanyakazi wa
misaada ya kiutu wanakadiria kuwa tangu Aprili 2023, vita kati ya wapiganaji wa
Daglo na mkuu wa jeshi Abdel Fattah al-Burhan vimesababisha vifo vya zaidi ya
watu laki mbili na kusababisha mgogoro mkubwa zaidi duniani wa njaa na raia
kuyakimbia makaazi yao.
Chanzo: DW
PROF. GEORDAVIE MAFANIKIO HAYAJAWEKWA KWA AJILI YA WATU FULANI
Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie amewataka watu kutambua kwamba kufanikiwa hakuji tu na wala mafanikio hayajawekwa kwa ajili ya watu fulani.
Ameyaema hayo
mwishoni mwa wiki {Julai 25, 2026} wakati akifundisha katika mkutano wa akili ya fedha
uliofanyika katika ukumbi wa PAPU Tower uliopo Philips jijini Arusha.
Akifundisha
Prof. GeorDavie amesema mafanikio hayajawekwa kwa ajili ya watu Fulani ni
mtazamo jambo ambalo amesema ni tatizo linawasumbua watu wengi kutokana na
Fikra za mambo yaliyopita.
Habari Na Beatrice Maina
UNAIDS: DUNIA IKO HATARINI KWA MLIPUKO MWENGINE WA UKIMWI
Umoja wa Mataifa unasema
kuna dunia iko kwenye hatari ya kuzuka tena kwa mlipuko wa virusi vya ukimwi.
Shirika la umoja wa
Mataifa linaloshughulikia UKIMWI UNAIDS limesema hii ni kutokana na ufadhili
duniani kupungua pakubwa mwaka jana.
Katika ripoti yake ya
kurasa 60 iliyozinduliwa huko Brazil kuelekea kuanza kwa Kongamano la Kimataifa
la UKIMWI, Umoja wa Mataifa unasema jamii ya kimataifa imeingia katika enzi za
siasa na ubanaji wa fedha mambo yanayotishia kuharibu mazuri yote yaliyopatikana
kwa miongo kadhaa katika vita dhidi ya virusi hivyo.
Shirika la UNAIDS
linasema ufadhili ulipungua kwa asilimia 18 mwaka 2025 hadi dola bilioni 7.3
hicho kikiwa kiwango cha chini zaidi katika karibu miongo miwili.
Kabla kuingia madarakani
kwa Donald Trump, Marekani ndiyo iliyokuwa mfadhili mkuu ikichangia asilimia 75
ya ufadhili jumla wa dunia.
Chanzo: DW
UMEME JUA KISHAPU AWAMU YA PILI KUIONGEZEA TANZANIA MEGAWATI 100 ZA NISHATI JADIDIFU
Hatua
hiyo imekuja baada ya kukamilika kwa awamu ya kwanza ya mradi huo wenye uwezo
wa kuzalisha jumla ya megawati 50 na kuingizwa katika Gridi ya Taifa, jambo
lililoongeza uwezo na uthabiti wa gridi hiyo na kuimarisha upatikanaji wa umeme
katika maeneo mbalimbali nchini.
Akizungumza
katika hafla hiyo Julai 27, 2026, Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi,
amesema sekta ya nishati ni mhimili wa maendeleo ya Taifa ambapo Serikali
inaendelea kufanya jitihada za kuongeza vyanzo mseto vya uzalishaji wa umeme
(Energy Mix) ili kuhakikisha Tanzania haitegemei chanzo kimoja pekee cha
uzalishaji wa umeme.
%20Instagram.png)




































%20Instagram.png)














