Monday, August 24, 2026

MTUME KATHRYN KRICK ASEMA ANAWEZA KUFANYA CHOCHOTE AMBACHO MUNGU AMEMUAGIZA KUFANYA

Kiongozi wa kanisa la @5fchurch @apostlekathrynkrick amesema anaweza kufanya chochote ambacho Mungu amemuagiza kukifanya bila kujali watu watasemaje kuhusu jambo hilo.

Ameyasema hayoo siku ya jana kwenye ibada katika kanisa la 5F church lililopo los angles Marekani.

Ameeleza amejinza hayo kutoka kwa baba yake wa kiroho Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie ambaye ni mtu jasiri na anayefanya mambo ambayo Mungu amemuamrisha kuyafanya bila kujali maneno ya watu.

Aidha amesema anamuheshimu baba yake wa kiroho Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie kama Biblia inaelekeza kuwaheshimu wanaoshtahili heshima.

Mtume Kathryine krick amekuwa akifanya huduma za kiroho katika nchi mbalimbali duniani Zaidi ya 190 huku akiowaombea Baraka na uponyaji kwa nguvu ya Mungu inayowashangaza mataifa.



MCHUNGAJI KIONGOZI MAMA ANNA DAVIE AWASHUKURU INTERNATIONAL PARTNERS KUENDELEA KUSAPOTI KAZI YA MUNGU

Mchungaji Kiongozi Mama Anna Davie amewashukuru na kufurahishwa na wana international Partner ambao wanatoa fedha zao kwa moyo wakupenda kwa ajili ya kusapoti maono ya Mtu mkuu wa Mungu.

Ameyasema hayo hii leo wakati wa ibada ya chuo kikuu cha manabii iliyofanyika katika nyumba nyumba ya matamko ngurumo ya upako kisongo.

Akizungumza amesema kuwa ni jambo la ajabu mtu kutoa kwa hiari na kwa furaha kwa ajili ya kutimiza kazi ya huduma huku wakitegemea kupokea baraka.

Naye Mtume Elisifa Kephasi akifundisha somo la chagua kwenda mbele sio kurudi nyuma amesema kuwa katika kwenda mbele lazima uchague kwenda na Mungu na sio kundi la watu kwa sababu watu wanaweza kukuacha njiani lakini Mungu hawezi kukuacha.

Kwa upande wake Mchungaji Paulo Mkumbo amesema mtu atakapo liandama agano ambalo Mungu amefanya na Baba wa Kiroho kwa nguvu zote utamuona Mungu katika Maisha yako.

Pia kijana Jackline Kessy amepata nafasi ya kuhubiri ambapo kupitia kichwa cha somo kisemacho KUBALI MCHAKATO WA KUOZA ILI UMEE TENA amesema kuwa ili mbegu iote na kukua lazima ioze na unapokubali kuoza unakubali kuongozeka.



Wednesday, August 19, 2026

SERIKALI YATOA MAELEKEZO KUADIMIKA KWA SARUJI

Serikali imewapa siku saba wamiliki wa viwanda vya kuzalisha saruji nchini kuwasilisha mapendekezo ya namna ya kutatua changamoto ya bei ya saruji inayotajwa kuwa juu katika soko pamoja na upatikanaji wake.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Balozi Waziri Salum, kukutana na kufanya mazungumzo na wamiliki wa viwanda vya saruji Agosti 18, 2026 jijini Dodoma.

Salum amesema, kikao kimelenga kutafuta suluhu ya changamoto iliyosababisha kuadimika kwa bidhaa hiyo na bei kuwa juu sokoni.

Kikao hicho kimehudhuriwa pia na viongozi wa taasisi mbalimbali zinazohusika na udhibiti, viwango na masoko, ikiwemo Tume ya Ushindani (FCC), Shirika la Viwango Tanzania (TBS), TanTrade, pamoja na Wakurugenzi kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara.

Akizungumza katika kikao hicho, Balozi Salum amesisitiza umuhimu wa kupata suluhu ya kudumu itakayosaidia kuhakikisha saruji inapatikana kwa bei inayozingatia maslahi ya wazalishaji, wafanyabiashara na wananchi.

KICHERE ASISITIZA UMUHIMU WA KUIMARISHA USHIRIKIANO KATI YA TAASISI ZA UKAGUZI, MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere, amesisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi za ukaguzi, mapambano dhidi ya rushwa na udhibiti wa manunuzi ya umma katika kuzuia upotevu wa rasilimali za Serikali na kukabiliana na utakatishaji fedha. 

Ofisi ya CAG ina jukumu la kufanya ukaguzi unaolenga kuimarisha uwazi, uwajibikaji na usimamizi bora wa rasilimali za umma.  

Ameyasema hayo leo jijijini Arusha wakati akizungumza katika mkutano wa mwaka wa 19 wa INTOSAI Working Group on the Fight Against Corruption and Money Laundering (WGFACML) ulioandaliwa na Ofisi ya Taifa ya ukaguzi (NAOT).

Kichere amesema mapambano dhidi ya rushwa na uhalifu wa kifedha yanahitaji taasisi mbalimbali kufanya kazi kwa pamoja badala ya kila taasisi kutekeleza wajibu wake kwa kujitegemea.

Amesema ukaguzi wa Serikali haupaswi kuishia katika kubaini dosari baada ya fedha za umma kutumika, bali unapaswa pia kusaidia kutambua vihatarishi vinavyoweza kusababisha upotevu wa fedha, ubadhirifu na vitendo vya rushwa mapema.

Tuesday, August 11, 2026

KLABU YA FENERBAHCE IMEFIKIA MAKUBALIANO NA NAPOLI YA KUMSAJILI MSHAMBULIAJI, ROMELU LUKAKU

 


Klabu ya Fenerbahce ya Nchini Uturuki imefikia makubaliano na na Napoli ya Italia juu ya kumsajili mshambuliaji, Romelu Lukaku (33) kwa ada ya uhamisho ya euro milioni 6 itakayofikia euro milioni 8 pamoja na nyongeza.

Nyota huyo wa Kimataifa wa Ubelgiji tayari amefikia makubaliano ya maslahi binafsi na klabu hiyo na anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka miwili na chaguo la ongezeko la mwaka mmoja zaidi.

Mshambuliaji huyo wa zamani Chelsea na Manchester United anatarajiwa kutia kibindoni mshahara wa Euro milioni 10 (zaidi ya Tsh bilioni 30.5) kwa mwaka.

Miaka mitano iliyopita Chelsea ilimsajili nyota huyo kwa dau la Euro milioni 113 akitokea Inter Milan kabla ya kuuzwa kwenda Napoli kwa dau la Euro milioni 30.7 mnamo Agosti 2024 na sasa anatarajiwa kutimkia Uturuki kwa dau la Euro milioni 8.

Monday, August 3, 2026

TAZAMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO AGOSTI 04, 2026

 










UNAPOKUWA NA MOYO WA KUSHUKURU MUNGU ANAKUONGEZA AFYA, NGUVU, UWEZO NA FAIDA YA KUISHA NA WATU.

Imeelezwa kuwa unapokuwa na moyo wa kushukuru Mungu anakuongeza afya, nguvu, uwezo na faida ya kuisha na watu katika maisha yako.

Hayo yamesemwa na mchungaji kiongozi mama Anna Davie katika ibada ya chuo kikuu cha Manabii iliyofanyika jana katika nyumba ya matamko kisongo Arusha ambapo ilikuwa ni ibada ya shukrani kuu mbele za Mungu.

Naye Askofu Msaidizi Ken Davie alipata nafasi ya kuzungumza katika ibada hiyo na amesema kuwa kila mmoja na wajibu wa kuupendezesha ufalme wa Mungu huku akiongeza kuwa hata shukrani zetu zinatakiwa ziwe harufu nzuri kwa mungu.

Mtume Rose Abel alitapanafasi ya kuhubiri na amemtaka kila mtu kuwa na utaratibu wa kumshukuru mungu hata anapopitia changamoto mbalimbali katika maisha.

Kwa upande wake kijana MeikoKing amesema SHUKRANI inampa mtu 'PROMOTION' katika maisha ya kila siku.




 

TAZAMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO AGOSTI 03, 2026