Tuesday, August 11, 2026

KLABU YA FENERBAHCE IMEFIKIA MAKUBALIANO NA NAPOLI YA KUMSAJILI MSHAMBULIAJI, ROMELU LUKAKU

 


Klabu ya Fenerbahce ya Nchini Uturuki imefikia makubaliano na na Napoli ya Italia juu ya kumsajili mshambuliaji, Romelu Lukaku (33) kwa ada ya uhamisho ya euro milioni 6 itakayofikia euro milioni 8 pamoja na nyongeza.

Nyota huyo wa Kimataifa wa Ubelgiji tayari amefikia makubaliano ya maslahi binafsi na klabu hiyo na anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka miwili na chaguo la ongezeko la mwaka mmoja zaidi.

Mshambuliaji huyo wa zamani Chelsea na Manchester United anatarajiwa kutia kibindoni mshahara wa Euro milioni 10 (zaidi ya Tsh bilioni 30.5) kwa mwaka.

Miaka mitano iliyopita Chelsea ilimsajili nyota huyo kwa dau la Euro milioni 113 akitokea Inter Milan kabla ya kuuzwa kwenda Napoli kwa dau la Euro milioni 30.7 mnamo Agosti 2024 na sasa anatarajiwa kutimkia Uturuki kwa dau la Euro milioni 8.

Monday, August 3, 2026

TAZAMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO AGOSTI 04, 2026

 










UNAPOKUWA NA MOYO WA KUSHUKURU MUNGU ANAKUONGEZA AFYA, NGUVU, UWEZO NA FAIDA YA KUISHA NA WATU.

Imeelezwa kuwa unapokuwa na moyo wa kushukuru Mungu anakuongeza afya, nguvu, uwezo na faida ya kuisha na watu katika maisha yako.

Hayo yamesemwa na mchungaji kiongozi mama Anna Davie katika ibada ya chuo kikuu cha Manabii iliyofanyika jana katika nyumba ya matamko kisongo Arusha ambapo ilikuwa ni ibada ya shukrani kuu mbele za Mungu.

Naye Askofu Msaidizi Ken Davie alipata nafasi ya kuzungumza katika ibada hiyo na amesema kuwa kila mmoja na wajibu wa kuupendezesha ufalme wa Mungu huku akiongeza kuwa hata shukrani zetu zinatakiwa ziwe harufu nzuri kwa mungu.

Mtume Rose Abel alitapanafasi ya kuhubiri na amemtaka kila mtu kuwa na utaratibu wa kumshukuru mungu hata anapopitia changamoto mbalimbali katika maisha.

Kwa upande wake kijana MeikoKing amesema SHUKRANI inampa mtu 'PROMOTION' katika maisha ya kila siku.




 

TAZAMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO AGOSTI 03, 2026












 

Friday, July 31, 2026

TAZAMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO AGOSTI 01, 2026










 

RAIS SAMIA KUFANYA ZIARA YA KIKAZI NCHINI ANGOLA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Luanda, Angola ambapo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla ya Uzinduzi wa Hospitali iliyopewa jina la Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, tarehe 31 Julai.




TAZAMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO JULAI 31, 2026