Monday, July 27, 2026

MOROCCO, ALGERIA ZAANZA VIZURI WAFCON


Timu za Taifa za soka za wanawake za Morocco na Algeria zimeanza vyema kampeni zao za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake (WAFCON) 2026 kwa kuibuka na ushindi katika michezo yao ya kwanza ya hatua ya makundi.

Wenyeji Morocco wameonyesha ubora kwa kuichapa Kenya (Harambee Starlets) mabao 4-0 katika mchezo wa Kundi A, huku Algeria ikiifunga Senegal mabao 2-0 na kuanza michuano hiyo kwa pointi tatu muhimu.

Michuano hiyo inaendelea leo ambapo Timu ya Taifa ya Wanawake ya Tanzania, Twiga Stars, itashuka dimbani kuivaa Afrika Kusini katika mchezo wa Kundi B utakaochezwa saa 2:00 usiku.

 


MAAMBUKIZI YA EBOLA YAPINDUKIA 3,000 KONGO

 


Haya yanafanyika wakati ambapo maambukizi yameripotiwa kuongezeka kwa karibu 1,000 katika kipindi cha siku kumi tu.

Takwimu rasmi zinaonesha kuwa jumla ya visa 3,075 sasa vimethibitishwa katika mikoa mitano baada ya mlipuko huo wa Ebola kuvuka maambukizi 2,000 mnamo Julai 15.

Mamlaka zinasema ugunduzi wa maambukizi na juhudi za kupima zimechangia katika kugundua maambukizi zaidi.

Mlipuko huo uliotangazwa mnamo Mei 15, unasababishwa na aina ya kirusi cha Bundibugyo ambacho bado hakijapata chanjo au tiba.

Kulingana na Shirika la Afya Ulimwenguni, WHO, karibu asilimia 90 ya visa vimeripotiwa katika mkoa wa kaskazini mashariki wa Ituri, ambao unapakana na Sudan Kusini na Uganda.

Mlipuko huo huenda ukadumu kwa miezi kadhaa zaidi kutokana na mgomo wa wahudumu wa afya wanaolalamikia kutolipwa mishara yao na kutatiza utoaji huduma katika baadhi ya hospitali.

Thursday, July 23, 2026


Kambi ya matibabu ya bure iliyofanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha, imefanikiwa kutoa huduma kwa wagonjwa zaidi ya 24,871, hatua inayoonyesha mwitikio mkubwa wa wananchi katika kupata huduma za afya za kibingwa na kibobezi. 

Idadi hiyo inaonesha mafanikio makubwa ya kambi hiyo iliyowaleta pamoja madaktari bingwa na wabobezi kutoka hospitali na taasisi mbalimbali nchini, wakitoa huduma za uchunguzi, matibabu, vipimo na ushauri wa afya bila malipo kwa wananchi kutoka Arusha na mikoa jirani. 

Makonda amesema kuwa,Kambi ya matibabu ya madaktari bingwa imefanikiwa kubaini wananchi 1,930 waliokuwa na shinikizo la juu la damu bila kufahamu hali zao za kiafya, hatua iliyotajwa kuwa muhimu katika kuzuia madhara ya magonjwa yasiyoambukiza kupitia uchunguzi wa mapema.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukamilika kwa kambi hiyo, Mbunge wa Arusha ambaye pia ni Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Mhe. Paul Makonda, amesema jumla ya wananchi 6,070 walifanyiwa uchunguzi wa shinikizo la damu, ambapo asilimia 65 walibainika kuwa na tatizo hilo

Amesema kati yao, wananchi 1,930 waligundulika kwa mara ya kwanza kuwa na ugonjwa huo na wataendelea kufuatiliwa na wataalamu wa afya ili kupata matibabu na ushauri unaostahili.

MALI, NIGER NA BURKINA FASO ZATAFUTA KUANDAA AFCON 2032


Mali, Niger na Burkina Faso, nchi tatu zinazoongozwa na serikali za kijeshi zinawania kwa pamoja kuwa wenyeji wa Kombe la Mataifa ya Afrika AFCON mwaka 2032.

Shirikisho la Soka la Mali lilisema katika taarifa kwamba maafisa wake walikutana na rais wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Patrice Motsepe, Jumamosi mjini New York, "kwa lengo la kuandaa zabuni ya pamoja ya kuandaa Kombe la Mataifa ya Afrika 2032."



Nchi hizo tatu jirani, ambazo pia ni washirika ndani ya Muungano wa Nchi za Sahel (Alliance of Sahel States - AES), zinaongozwa na tawala za kijeshi zilizochukua madaraka kupitia mapinduzi.

Aidha, zinakabiliwa na changamoto kubwa za kiusalama kutokana na mashambulizi ya makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali, ambayo yamesababisha vifo vya maelfu ya watu.


TAZAMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO JULAI 23, 2026












 

Sunday, July 19, 2026

HISPANIA YATWAA KOMBE LA DUNIA 2026 BAADA YA KUWABWAGA ARGENTINA


Timu ya Taifa ya Hispania imefanikiwa kutwaa Kombe la Dunia 2026 baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Argentina katika mchezo wa fainali uliochezwa kwenye Uwanja wa MetLife, New Jersey, Marekani.

Bao pekee la ushindi lilifungwa na mshambuliaji Ferran Torres katika dakika ya 116 ya mchezo.

Mchezo huo ulilazimika kuchezwa hadi dakika 120 baada ya dakika 90 za kawaida kumalizika kwa sare ya bila kufungana.

Argentina ilimaliza dakika 30 za nyongeza ikiwa pungufu uwanjani baada ya kiungo Enzo Fernández kuonyeshwa kadi nyekundu.





TAZAMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO JULAI 20, 2026