Thursday, July 23, 2026


Kambi ya matibabu ya bure iliyofanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha, imefanikiwa kutoa huduma kwa wagonjwa zaidi ya 24,871, hatua inayoonyesha mwitikio mkubwa wa wananchi katika kupata huduma za afya za kibingwa na kibobezi. 

Idadi hiyo inaonesha mafanikio makubwa ya kambi hiyo iliyowaleta pamoja madaktari bingwa na wabobezi kutoka hospitali na taasisi mbalimbali nchini, wakitoa huduma za uchunguzi, matibabu, vipimo na ushauri wa afya bila malipo kwa wananchi kutoka Arusha na mikoa jirani. 

Makonda amesema kuwa,Kambi ya matibabu ya madaktari bingwa imefanikiwa kubaini wananchi 1,930 waliokuwa na shinikizo la juu la damu bila kufahamu hali zao za kiafya, hatua iliyotajwa kuwa muhimu katika kuzuia madhara ya magonjwa yasiyoambukiza kupitia uchunguzi wa mapema.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukamilika kwa kambi hiyo, Mbunge wa Arusha ambaye pia ni Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Mhe. Paul Makonda, amesema jumla ya wananchi 6,070 walifanyiwa uchunguzi wa shinikizo la damu, ambapo asilimia 65 walibainika kuwa na tatizo hilo

Amesema kati yao, wananchi 1,930 waligundulika kwa mara ya kwanza kuwa na ugonjwa huo na wataendelea kufuatiliwa na wataalamu wa afya ili kupata matibabu na ushauri unaostahili.

MALI, NIGER NA BURKINA FASO ZATAFUTA KUANDAA AFCON 2032


Mali, Niger na Burkina Faso, nchi tatu zinazoongozwa na serikali za kijeshi zinawania kwa pamoja kuwa wenyeji wa Kombe la Mataifa ya Afrika AFCON mwaka 2032.

Shirikisho la Soka la Mali lilisema katika taarifa kwamba maafisa wake walikutana na rais wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Patrice Motsepe, Jumamosi mjini New York, "kwa lengo la kuandaa zabuni ya pamoja ya kuandaa Kombe la Mataifa ya Afrika 2032."



Nchi hizo tatu jirani, ambazo pia ni washirika ndani ya Muungano wa Nchi za Sahel (Alliance of Sahel States - AES), zinaongozwa na tawala za kijeshi zilizochukua madaraka kupitia mapinduzi.

Aidha, zinakabiliwa na changamoto kubwa za kiusalama kutokana na mashambulizi ya makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali, ambayo yamesababisha vifo vya maelfu ya watu.


TAZAMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO JULAI 23, 2026












 

Sunday, July 19, 2026

HISPANIA YATWAA KOMBE LA DUNIA 2026 BAADA YA KUWABWAGA ARGENTINA


Timu ya Taifa ya Hispania imefanikiwa kutwaa Kombe la Dunia 2026 baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Argentina katika mchezo wa fainali uliochezwa kwenye Uwanja wa MetLife, New Jersey, Marekani.

Bao pekee la ushindi lilifungwa na mshambuliaji Ferran Torres katika dakika ya 116 ya mchezo.

Mchezo huo ulilazimika kuchezwa hadi dakika 120 baada ya dakika 90 za kawaida kumalizika kwa sare ya bila kufungana.

Argentina ilimaliza dakika 30 za nyongeza ikiwa pungufu uwanjani baada ya kiungo Enzo Fernández kuonyeshwa kadi nyekundu.





TAZAMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO JULAI 20, 2026











 

Thursday, July 16, 2026

FIFA KUANGALIA UWEZEKANO WA KUIADHIBU ARGENTINA

Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) linachunguza uwezekano wa kuichukulia hatua za kinidhamu timu ya taifa ya Argentina, baada ya wachezaji wake kuinua bango lenye ujumbe wa kisiasa kuhusu Visiwa vya Falkland.

Tukio hilo lilitokea Jumatano usiku mara baada ya Argentina kuifunga England mabao mawili kwa moja katika nusu fainali ya Kombe la Dunia.

Wachezaji wa Argentina walisherehekea ushindi huo kwa kubeba bango lililoandikwa "Visiwa vya Falkland ni vya Argentina."

Serikali ya Uingereza, kupitia ofisi ya Waziri Mkuu, imeunga mkono wito wa kutaka FIFA ichukue hatua kali dhidi ya mabingwa hao watetezi. Visiwa vya Falkland ni eneo la ng'ambo la Uingereza tangu vita vya mwaka 1982, na wananchi wake walipiga kura mwaka 2013 kusalia chini ya Uingereza.

Sheria za FIFA zinakataza vikali ujumbe wa kisiasa uwanjani, na tayari Argentina ilishawahi kupigwa faini kwa kosa kama hili mwaka 2024.

TANZANIA KUONGEZA KASI KATIKA HUDUMA YA UPANDIKIZAJI WA ULOTO


Serikali imeeleza dhamira yake ya kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha huduma za afya za kibingwa katika Afrika Mashariki na Kati huku ikitoa wito kwa Watanzania na wadau mbalimbali kushiriki kuchangia Mfuko wa Upandikizaji wa Figo na Uloto ili kuwawezesha wagonjwa wasiokuwa na uwezo kupata matibabu yanayookoa maisha.

Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa (Mb), wakati akiwasilisha taarifa kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), katika hafla ya chakula cha pamoja cha kuchangisha fedha kwa ajili ya kugharamia huduma za upandikizaji wa figo na uloto katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, iliyofanyika jijini Dodoma.


TAZAMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO JULAI 17, 2026