Wednesday, July 29, 2026
Tuesday, July 28, 2026
DAGLO ASEMA WAPIGANAJI WAKE "HURU SASA" KUPAMBANA NA JESHI
Mkuu wa
wanamgambo wa RSF nchini Sudan Mohamed Hamdan Daglo amewaambia wapiganaji wake
kuwa "wameachiliwa huru" sasa kupambana na jeshi la nchi hiyo.
Ujumbe huu wa
Daglo kwa wapiganaji wake ambao wametuhumiwa kwa mauaji ya kimbari unakuja siku
moja baada ya kupoteza udhibiti wa barabara moja kuu kati ya Mji Mkuu Khartoum
na mji mkubwa wa eneo la Kordofan wa El-Obeid.
Kwa wiki
kadhaa sasa Umoja wa Mataifa umeonya kuwa huenda wapiganaji wa RSF
wakasababisha mauaji makubwa katika eneo la Kordofan, wakati wanapotafuta
kuuzingira mji wa El-Obeid kuelekea uvamizi mkubwa wanaotazamia kuufanya.
Wafanyakazi wa
misaada ya kiutu wanakadiria kuwa tangu Aprili 2023, vita kati ya wapiganaji wa
Daglo na mkuu wa jeshi Abdel Fattah al-Burhan vimesababisha vifo vya zaidi ya
watu laki mbili na kusababisha mgogoro mkubwa zaidi duniani wa njaa na raia
kuyakimbia makaazi yao.
Chanzo: DW
PROF. GEORDAVIE MAFANIKIO HAYAJAWEKWA KWA AJILI YA WATU FULANI
Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie amewataka watu kutambua kwamba kufanikiwa hakuji tu na wala mafanikio hayajawekwa kwa ajili ya watu fulani.
Ameyaema hayo
mwishoni mwa wiki {Julai 25, 2026} wakati akifundisha katika mkutano wa akili ya fedha
uliofanyika katika ukumbi wa PAPU Tower uliopo Philips jijini Arusha.
Akifundisha
Prof. GeorDavie amesema mafanikio hayajawekwa kwa ajili ya watu Fulani ni
mtazamo jambo ambalo amesema ni tatizo linawasumbua watu wengi kutokana na
Fikra za mambo yaliyopita.
Habari Na Beatrice Maina
UNAIDS: DUNIA IKO HATARINI KWA MLIPUKO MWENGINE WA UKIMWI
Umoja wa Mataifa unasema
kuna dunia iko kwenye hatari ya kuzuka tena kwa mlipuko wa virusi vya ukimwi.
Shirika la umoja wa
Mataifa linaloshughulikia UKIMWI UNAIDS limesema hii ni kutokana na ufadhili
duniani kupungua pakubwa mwaka jana.
Katika ripoti yake ya
kurasa 60 iliyozinduliwa huko Brazil kuelekea kuanza kwa Kongamano la Kimataifa
la UKIMWI, Umoja wa Mataifa unasema jamii ya kimataifa imeingia katika enzi za
siasa na ubanaji wa fedha mambo yanayotishia kuharibu mazuri yote yaliyopatikana
kwa miongo kadhaa katika vita dhidi ya virusi hivyo.
Shirika la UNAIDS
linasema ufadhili ulipungua kwa asilimia 18 mwaka 2025 hadi dola bilioni 7.3
hicho kikiwa kiwango cha chini zaidi katika karibu miongo miwili.
Kabla kuingia madarakani
kwa Donald Trump, Marekani ndiyo iliyokuwa mfadhili mkuu ikichangia asilimia 75
ya ufadhili jumla wa dunia.
Chanzo: DW
UMEME JUA KISHAPU AWAMU YA PILI KUIONGEZEA TANZANIA MEGAWATI 100 ZA NISHATI JADIDIFU
Hatua
hiyo imekuja baada ya kukamilika kwa awamu ya kwanza ya mradi huo wenye uwezo
wa kuzalisha jumla ya megawati 50 na kuingizwa katika Gridi ya Taifa, jambo
lililoongeza uwezo na uthabiti wa gridi hiyo na kuimarisha upatikanaji wa umeme
katika maeneo mbalimbali nchini.
Akizungumza
katika hafla hiyo Julai 27, 2026, Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi,
amesema sekta ya nishati ni mhimili wa maendeleo ya Taifa ambapo Serikali
inaendelea kufanya jitihada za kuongeza vyanzo mseto vya uzalishaji wa umeme
(Energy Mix) ili kuhakikisha Tanzania haitegemei chanzo kimoja pekee cha
uzalishaji wa umeme.
Monday, July 27, 2026
MOROCCO, ALGERIA ZAANZA VIZURI WAFCON
Timu za Taifa za soka za
wanawake za Morocco na Algeria zimeanza vyema kampeni zao za Kombe la Mataifa
ya Afrika kwa Wanawake (WAFCON) 2026 kwa kuibuka na ushindi katika michezo yao
ya kwanza ya hatua ya makundi.
Wenyeji Morocco
wameonyesha ubora kwa kuichapa Kenya (Harambee Starlets) mabao 4-0 katika
mchezo wa Kundi A, huku Algeria ikiifunga Senegal mabao 2-0 na kuanza michuano
hiyo kwa pointi tatu muhimu.
Michuano hiyo inaendelea
leo ambapo Timu ya Taifa ya Wanawake ya Tanzania, Twiga Stars, itashuka dimbani
kuivaa Afrika Kusini katika mchezo wa Kundi B utakaochezwa saa 2:00 usiku.
MAAMBUKIZI YA EBOLA YAPINDUKIA 3,000 KONGO
Haya yanafanyika wakati ambapo maambukizi yameripotiwa kuongezeka kwa karibu 1,000 katika kipindi cha siku kumi tu.
Takwimu rasmi
zinaonesha kuwa jumla ya visa 3,075 sasa vimethibitishwa katika
mikoa mitano baada ya mlipuko huo wa Ebola kuvuka maambukizi 2,000 mnamo Julai
15.
Mamlaka
zinasema ugunduzi wa maambukizi na juhudi za kupima zimechangia
katika kugundua maambukizi zaidi.
Mlipuko huo uliotangazwa
mnamo Mei 15, unasababishwa na aina ya kirusi cha Bundibugyo ambacho bado
hakijapata chanjo au tiba.
Kulingana na Shirika la
Afya Ulimwenguni, WHO, karibu asilimia 90 ya visa vimeripotiwa katika mkoa wa
kaskazini mashariki wa Ituri, ambao unapakana na Sudan Kusini na Uganda.
Mlipuko huo huenda
ukadumu kwa miezi kadhaa zaidi kutokana na mgomo wa wahudumu wa afya
wanaolalamikia kutolipwa mishara yao na kutatiza utoaji huduma katika baadhi ya
hospitali.
Sunday, July 26, 2026
Thursday, July 23, 2026
Kambi ya matibabu ya bure iliyofanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha, imefanikiwa kutoa huduma kwa wagonjwa zaidi ya 24,871, hatua inayoonyesha mwitikio mkubwa wa wananchi katika kupata huduma za afya za kibingwa na kibobezi.
Idadi hiyo inaonesha
mafanikio makubwa ya kambi hiyo iliyowaleta pamoja madaktari bingwa na wabobezi
kutoka hospitali na taasisi mbalimbali nchini, wakitoa huduma za uchunguzi,
matibabu, vipimo na ushauri wa afya bila malipo kwa wananchi kutoka Arusha na
mikoa jirani.
Makonda amesema
kuwa,Kambi ya matibabu ya madaktari bingwa imefanikiwa kubaini wananchi 1,930
waliokuwa na shinikizo la juu la damu bila kufahamu hali zao za kiafya, hatua
iliyotajwa kuwa muhimu katika kuzuia madhara ya magonjwa yasiyoambukiza kupitia
uchunguzi wa mapema.
Akizungumza na waandishi
wa habari baada ya kukamilika kwa kambi hiyo, Mbunge wa Arusha ambaye pia ni
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Mhe. Paul Makonda, amesema jumla
ya wananchi 6,070 walifanyiwa uchunguzi wa shinikizo la damu, ambapo asilimia
65 walibainika kuwa na tatizo hilo
Amesema kati yao,
wananchi 1,930 waligundulika kwa mara ya kwanza kuwa na ugonjwa huo na
wataendelea kufuatiliwa na wataalamu wa afya ili kupata matibabu na ushauri
unaostahili.
MALI, NIGER NA BURKINA FASO ZATAFUTA KUANDAA AFCON 2032
Mali, Niger na Burkina Faso, nchi tatu zinazoongozwa na
serikali za kijeshi zinawania kwa pamoja kuwa wenyeji wa Kombe la Mataifa ya
Afrika AFCON mwaka
2032.
Shirikisho la Soka la Mali lilisema katika taarifa kwamba
maafisa wake walikutana na rais wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Patrice
Motsepe, Jumamosi mjini New York, "kwa lengo la kuandaa zabuni ya pamoja
ya kuandaa Kombe la Mataifa ya Afrika 2032."
Nchi hizo tatu jirani, ambazo pia ni washirika ndani ya Muungano wa
Nchi za Sahel (Alliance of Sahel States - AES), zinaongozwa na
tawala za kijeshi zilizochukua madaraka kupitia mapinduzi.
Aidha, zinakabiliwa na changamoto kubwa za kiusalama kutokana
na mashambulizi ya makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali, ambayo
yamesababisha vifo vya maelfu ya watu.













%20Instagram.png)









































