Tuesday, July 28, 2026

DAGLO ASEMA WAPIGANAJI WAKE "HURU SASA" KUPAMBANA NA JESHI

Mkuu wa wanamgambo wa RSF nchini Sudan Mohamed Hamdan Daglo amewaambia wapiganaji wake kuwa "wameachiliwa huru" sasa kupambana na jeshi la nchi hiyo.

Ujumbe huu wa Daglo kwa wapiganaji wake ambao wametuhumiwa kwa mauaji ya kimbari unakuja siku moja baada ya kupoteza udhibiti wa barabara moja kuu kati ya Mji Mkuu Khartoum na mji mkubwa wa eneo la Kordofan wa El-Obeid.

Kwa wiki kadhaa sasa Umoja wa Mataifa umeonya kuwa huenda wapiganaji wa RSF wakasababisha mauaji makubwa katika eneo la Kordofan, wakati wanapotafuta kuuzingira mji wa El-Obeid kuelekea uvamizi mkubwa wanaotazamia kuufanya.

Wafanyakazi wa misaada ya kiutu wanakadiria kuwa tangu Aprili 2023, vita kati ya wapiganaji wa Daglo na mkuu wa jeshi Abdel Fattah al-Burhan vimesababisha vifo vya zaidi ya watu laki mbili na kusababisha mgogoro mkubwa zaidi duniani wa njaa na raia kuyakimbia makaazi yao.

 

Chanzo: DW


PROF. GEORDAVIE MAFANIKIO HAYAJAWEKWA KWA AJILI YA WATU FULANI


Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie amewataka watu kutambua kwamba kufanikiwa hakuji tu na wala mafanikio hayajawekwa kwa ajili ya watu fulani.

Ameyaema hayo mwishoni mwa wiki {Julai 25, 2026} wakati akifundisha katika mkutano wa akili ya fedha uliofanyika katika ukumbi wa PAPU Tower uliopo Philips jijini Arusha.

Akifundisha Prof. GeorDavie amesema mafanikio hayajawekwa kwa ajili ya watu Fulani ni mtazamo jambo ambalo amesema ni tatizo linawasumbua watu wengi kutokana na Fikra za mambo yaliyopita.


                                                               Habari Na Beatrice Maina

UNAIDS: DUNIA IKO HATARINI KWA MLIPUKO MWENGINE WA UKIMWI



Umoja wa Mataifa unasema kuna dunia iko kwenye hatari ya kuzuka tena kwa mlipuko wa virusi vya ukimwi.

Shirika la umoja wa Mataifa linaloshughulikia UKIMWI UNAIDS limesema hii ni kutokana na ufadhili duniani kupungua pakubwa mwaka jana.

Katika ripoti yake ya kurasa 60 iliyozinduliwa huko Brazil kuelekea kuanza kwa Kongamano la Kimataifa la UKIMWI, Umoja wa Mataifa unasema jamii ya kimataifa imeingia katika enzi za siasa na ubanaji wa fedha mambo yanayotishia kuharibu mazuri yote yaliyopatikana kwa miongo kadhaa katika vita dhidi ya virusi hivyo.

Shirika la UNAIDS linasema ufadhili ulipungua kwa asilimia 18 mwaka 2025 hadi dola bilioni 7.3 hicho kikiwa kiwango cha chini zaidi katika karibu miongo miwili.

Kabla kuingia madarakani kwa Donald Trump, Marekani ndiyo iliyokuwa mfadhili mkuu ikichangia asilimia 75 ya ufadhili jumla wa dunia.

Chanzo: DW


UMEME JUA KISHAPU AWAMU YA PILI KUIONGEZEA TANZANIA MEGAWATI 100 ZA NISHATI JADIDIFU

Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) imeingia hatua mpya ya kuongeza vyanzo vya uzalishaji umeme baada ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa awamu ya pili ya Mradi wa umeme kwa nguvu ya Jua Kishapu utakaozalisha jumla ya megawati 100.

Hatua hiyo imekuja baada ya kukamilika kwa awamu ya kwanza ya mradi huo wenye uwezo wa kuzalisha jumla ya megawati 50 na kuingizwa katika Gridi ya Taifa, jambo lililoongeza uwezo na uthabiti wa gridi hiyo na kuimarisha upatikanaji wa umeme katika maeneo mbalimbali nchini.

Akizungumza katika hafla hiyo Julai 27, 2026, Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema sekta ya nishati ni mhimili wa maendeleo ya Taifa ambapo Serikali inaendelea kufanya jitihada za kuongeza vyanzo mseto vya uzalishaji wa umeme (Energy Mix) ili kuhakikisha Tanzania haitegemei chanzo kimoja pekee cha uzalishaji wa umeme.


TAZAMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO JULAI 28, 2026














 

Monday, July 27, 2026

MOROCCO, ALGERIA ZAANZA VIZURI WAFCON


Timu za Taifa za soka za wanawake za Morocco na Algeria zimeanza vyema kampeni zao za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake (WAFCON) 2026 kwa kuibuka na ushindi katika michezo yao ya kwanza ya hatua ya makundi.

Wenyeji Morocco wameonyesha ubora kwa kuichapa Kenya (Harambee Starlets) mabao 4-0 katika mchezo wa Kundi A, huku Algeria ikiifunga Senegal mabao 2-0 na kuanza michuano hiyo kwa pointi tatu muhimu.

Michuano hiyo inaendelea leo ambapo Timu ya Taifa ya Wanawake ya Tanzania, Twiga Stars, itashuka dimbani kuivaa Afrika Kusini katika mchezo wa Kundi B utakaochezwa saa 2:00 usiku.

 


MAAMBUKIZI YA EBOLA YAPINDUKIA 3,000 KONGO

 


Haya yanafanyika wakati ambapo maambukizi yameripotiwa kuongezeka kwa karibu 1,000 katika kipindi cha siku kumi tu.

Takwimu rasmi zinaonesha kuwa jumla ya visa 3,075 sasa vimethibitishwa katika mikoa mitano baada ya mlipuko huo wa Ebola kuvuka maambukizi 2,000 mnamo Julai 15.

Mamlaka zinasema ugunduzi wa maambukizi na juhudi za kupima zimechangia katika kugundua maambukizi zaidi.

Mlipuko huo uliotangazwa mnamo Mei 15, unasababishwa na aina ya kirusi cha Bundibugyo ambacho bado hakijapata chanjo au tiba.

Kulingana na Shirika la Afya Ulimwenguni, WHO, karibu asilimia 90 ya visa vimeripotiwa katika mkoa wa kaskazini mashariki wa Ituri, ambao unapakana na Sudan Kusini na Uganda.

Mlipuko huo huenda ukadumu kwa miezi kadhaa zaidi kutokana na mgomo wa wahudumu wa afya wanaolalamikia kutolipwa mishara yao na kutatiza utoaji huduma katika baadhi ya hospitali.

Thursday, July 23, 2026


Kambi ya matibabu ya bure iliyofanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha, imefanikiwa kutoa huduma kwa wagonjwa zaidi ya 24,871, hatua inayoonyesha mwitikio mkubwa wa wananchi katika kupata huduma za afya za kibingwa na kibobezi. 

Idadi hiyo inaonesha mafanikio makubwa ya kambi hiyo iliyowaleta pamoja madaktari bingwa na wabobezi kutoka hospitali na taasisi mbalimbali nchini, wakitoa huduma za uchunguzi, matibabu, vipimo na ushauri wa afya bila malipo kwa wananchi kutoka Arusha na mikoa jirani. 

Makonda amesema kuwa,Kambi ya matibabu ya madaktari bingwa imefanikiwa kubaini wananchi 1,930 waliokuwa na shinikizo la juu la damu bila kufahamu hali zao za kiafya, hatua iliyotajwa kuwa muhimu katika kuzuia madhara ya magonjwa yasiyoambukiza kupitia uchunguzi wa mapema.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukamilika kwa kambi hiyo, Mbunge wa Arusha ambaye pia ni Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Mhe. Paul Makonda, amesema jumla ya wananchi 6,070 walifanyiwa uchunguzi wa shinikizo la damu, ambapo asilimia 65 walibainika kuwa na tatizo hilo

Amesema kati yao, wananchi 1,930 waligundulika kwa mara ya kwanza kuwa na ugonjwa huo na wataendelea kufuatiliwa na wataalamu wa afya ili kupata matibabu na ushauri unaostahili.

MALI, NIGER NA BURKINA FASO ZATAFUTA KUANDAA AFCON 2032


Mali, Niger na Burkina Faso, nchi tatu zinazoongozwa na serikali za kijeshi zinawania kwa pamoja kuwa wenyeji wa Kombe la Mataifa ya Afrika AFCON mwaka 2032.

Shirikisho la Soka la Mali lilisema katika taarifa kwamba maafisa wake walikutana na rais wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Patrice Motsepe, Jumamosi mjini New York, "kwa lengo la kuandaa zabuni ya pamoja ya kuandaa Kombe la Mataifa ya Afrika 2032."



Nchi hizo tatu jirani, ambazo pia ni washirika ndani ya Muungano wa Nchi za Sahel (Alliance of Sahel States - AES), zinaongozwa na tawala za kijeshi zilizochukua madaraka kupitia mapinduzi.

Aidha, zinakabiliwa na changamoto kubwa za kiusalama kutokana na mashambulizi ya makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali, ambayo yamesababisha vifo vya maelfu ya watu.


TAZAMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO JULAI 23, 2026