Monday, July 20, 2026
Sunday, July 19, 2026
HISPANIA YATWAA KOMBE LA DUNIA 2026 BAADA YA KUWABWAGA ARGENTINA
Timu ya Taifa ya Hispania imefanikiwa kutwaa Kombe la Dunia 2026 baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Argentina katika mchezo wa fainali uliochezwa kwenye Uwanja wa MetLife, New Jersey, Marekani.
Bao
pekee la ushindi lilifungwa na mshambuliaji Ferran Torres katika dakika ya 116
ya mchezo.
Mchezo
huo ulilazimika kuchezwa hadi dakika 120 baada ya dakika 90 za kawaida
kumalizika kwa sare ya bila kufungana.
Argentina
ilimaliza dakika 30 za nyongeza ikiwa pungufu uwanjani baada ya kiungo Enzo
Fernández kuonyeshwa kadi nyekundu.
Thursday, July 16, 2026
FIFA KUANGALIA UWEZEKANO WA KUIADHIBU ARGENTINA
Tukio hilo lilitokea
Jumatano usiku mara baada ya Argentina kuifunga England mabao mawili kwa moja
katika nusu fainali ya Kombe la Dunia.
Wachezaji wa Argentina walisherehekea
ushindi huo kwa kubeba bango lililoandikwa "Visiwa vya Falkland ni vya
Argentina."
Serikali ya Uingereza,
kupitia ofisi ya Waziri Mkuu, imeunga mkono wito wa kutaka FIFA ichukue hatua
kali dhidi ya mabingwa hao watetezi. Visiwa vya Falkland ni eneo la ng'ambo la
Uingereza tangu vita vya mwaka 1982, na wananchi wake walipiga kura mwaka 2013
kusalia chini ya Uingereza.
Sheria za FIFA zinakataza
vikali ujumbe wa kisiasa uwanjani, na tayari Argentina ilishawahi kupigwa faini
kwa kosa kama hili mwaka 2024.
TANZANIA KUONGEZA KASI KATIKA HUDUMA YA UPANDIKIZAJI WA ULOTO
Serikali imeeleza dhamira
yake ya kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha huduma za afya za kibingwa katika
Afrika Mashariki na Kati huku ikitoa wito kwa Watanzania na wadau mbalimbali
kushiriki kuchangia Mfuko wa Upandikizaji wa Figo na Uloto ili kuwawezesha wagonjwa
wasiokuwa na uwezo kupata matibabu yanayookoa maisha.
Kauli hiyo ilitolewa na
Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa (Mb), wakati akiwasilisha taarifa kwa
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck
Nchemba (Mb), katika hafla ya chakula cha pamoja cha kuchangisha fedha kwa ajili
ya kugharamia huduma za upandikizaji wa figo na uloto katika Hospitali ya
Benjamin Mkapa, iliyofanyika jijini Dodoma.
Tuesday, July 14, 2026
Monday, July 13, 2026
MHE. NABII MKUU PROF. GEORDAVIE ATOA KIASI CHA SHILINGI MILIONI 58
Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie leo ametoa kiasi cha shilingi
milioni 58 ambapo shilingi milioni 53 ni kwa ajili ya kusapoti maono ya rais wa
umoja wa makanisa ya kitume na kinabii tanzania Nabii Dkt. Joshua Mwantyala na
shilingi milioni 5 kwa mchungaji hananja.
Ametoa fedha hizo alipokuwa akizungumza na mitume na manabii
kupitia kongamano la kurejesha thamani lililofanyika Morogoro katika huduma ya Nabii
Dkt. Joshua ambaye pia ndio muandaaji wa kongamano hilo ambapo shilingi miloni
50 ni kwa ajili ya kuendeleza maono, shilingi milioni tatu kwa ajili ya nh’ombe
wa maziwa ikiwa ni zawadi ya kumbukizi yake ya siku ya kuzaliwa.
Amempongeza na kufurahishwa na maono yake na kusema kuwa
kiasi hicho cha fedha amempa ili zimsaidie kuendeleza maono yake.
MHE. NABII MKUU PROF. GEORDAVIE AWATAKA WATUMISHI WA MUNGU KUWA NA UMOJA NA UPENDO
Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie mlezi wa umoja wa makanisa ya
kitume na kinabii amewataka watumishi wa mungu kuwa na umoja na upendo ili
mungu aweze kuonekana katika utumishi wao.
Ameyasema hayo jumapili ya July 12, 2026 alipokuwa
akizungumza na watumishi wa mungu, wachungaji, walimu, wainjilisti, mitume na manabii kupitia kongamano
la kurejesha thamani lililofanyika Mkoani Morogoro.
Akizungumza Nabii Mkuu amesema kuwa upendo wa kweli
unakosekana kwa watumishi ka sababu kuna mafarakano mengi ambayo yanasababisha Mungu
asionekane.
Amesema watumishi wa Mungu watakaposhikana mungu ataonekana
zaidi na watafanya kazi zaidi katika huduma zao.
Sunday, July 12, 2026
MHE. NABII MKUU PROF. GEORDAVIE AMEMUWEKA WAKFU MTUMISHI WA MUNGU NABII JOSHUA MWANTYALA
Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie amemuweka Wakfu Mtumishi wa
Mungu Nabii Joshua Mwantyala ambaye pia ni Rais wa umoja wa makanisa ya kitume
na Kinabii Tanzania.
Zoezi hilo amelifanya kupitia siku ya mwisho ya kongamano la
siku tatu la kurejesha thamani aliloliandaa mkoani Morogoro ambapo wakfu huo
amemuweka kwa kummiminia mafuta yeye kama Madhabahu na kumpokea rasmi kama
mtoto wake wa kiroho.
Akimuweka wakfu Nabii Mkuu ametamka ya kuwa majira mapya
yanakuja huku akiachilia matamko kwa Nabii Joshua kuwa na baraka za uwepo wa
Mungu, Baraka ya ulinzi, baraka ya uongozi ambapo na alimkabidhi kipaza sauti
microphone kama baraka ya fimbo kwa musa na kwamba atakapoongea sauti yake
itakwenda juu sana kwa nchi na itakuwa na mamlaka yenye utiisho.












%20Instagram.png)
%20Instagram.png)
%20Instagram.png)
































%20Facebook.png)
%20Facebook.png)
%20Facebook.png)