Kiongozi wa kanisa la @5fchurch @apostlekathrynkrick amesema anaweza kufanya chochote ambacho Mungu amemuagiza kukifanya bila kujali watu watasemaje kuhusu jambo hilo.
Ameyasema hayoo siku ya jana kwenye ibada katika kanisa la 5F church lililopo los angles Marekani.Monday, August 24, 2026
MTUME KATHRYN KRICK ASEMA ANAWEZA KUFANYA CHOCHOTE AMBACHO MUNGU AMEMUAGIZA KUFANYA
Ameeleza amejinza hayo kutoka kwa baba yake wa kiroho Mhe. Nabii Mkuu Prof.
GeorDavie ambaye ni mtu jasiri na anayefanya mambo ambayo Mungu amemuamrisha
kuyafanya bila kujali maneno ya watu.
Aidha amesema
anamuheshimu baba yake wa kiroho Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie kama Biblia
inaelekeza kuwaheshimu wanaoshtahili heshima.
Mtume Kathryine
krick amekuwa akifanya huduma za kiroho katika nchi mbalimbali duniani Zaidi ya
190 huku akiowaombea Baraka na uponyaji kwa nguvu ya Mungu inayowashangaza
mataifa.
MCHUNGAJI KIONGOZI MAMA ANNA DAVIE AWASHUKURU INTERNATIONAL PARTNERS KUENDELEA KUSAPOTI KAZI YA MUNGU
Mchungaji Kiongozi Mama Anna Davie amewashukuru na kufurahishwa na wana international Partner ambao wanatoa fedha zao kwa moyo wakupenda kwa ajili ya kusapoti maono ya Mtu mkuu wa Mungu.
Ameyasema hayo hii leo wakati wa ibada ya chuo kikuu cha manabii iliyofanyika katika nyumba nyumba ya matamko ngurumo ya upako kisongo.Akizungumza amesema kuwa
ni jambo la ajabu mtu kutoa kwa hiari na kwa furaha kwa ajili ya kutimiza kazi
ya huduma huku wakitegemea kupokea baraka.
Naye Mtume Elisifa
Kephasi akifundisha somo la chagua kwenda mbele sio kurudi nyuma amesema kuwa
katika kwenda mbele lazima uchague kwenda na Mungu na sio kundi la watu kwa
sababu watu wanaweza kukuacha njiani lakini Mungu hawezi kukuacha.
Kwa upande wake Mchungaji
Paulo Mkumbo amesema mtu atakapo liandama agano ambalo Mungu amefanya na Baba
wa Kiroho kwa nguvu zote utamuona Mungu katika Maisha yako.
Wednesday, August 19, 2026
SERIKALI YATOA MAELEKEZO KUADIMIKA KWA SARUJI
Serikali imewapa siku
saba wamiliki wa viwanda vya kuzalisha saruji nchini kuwasilisha mapendekezo ya
namna ya kutatua changamoto ya bei ya saruji inayotajwa kuwa juu katika soko
pamoja na upatikanaji wake.
Hatua hiyo imefikiwa
baada ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Balozi Waziri Salum,
kukutana na kufanya mazungumzo na wamiliki wa viwanda vya saruji Agosti 18,
2026 jijini Dodoma.
Salum amesema, kikao
kimelenga kutafuta suluhu ya changamoto iliyosababisha kuadimika kwa bidhaa
hiyo na bei kuwa juu sokoni.
Kikao hicho kimehudhuriwa
pia na viongozi wa taasisi mbalimbali zinazohusika na udhibiti, viwango na
masoko, ikiwemo Tume ya Ushindani (FCC), Shirika la Viwango Tanzania (TBS),
TanTrade, pamoja na Wakurugenzi kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara.
Akizungumza katika kikao
hicho, Balozi Salum amesisitiza umuhimu wa kupata suluhu ya kudumu
itakayosaidia kuhakikisha saruji inapatikana kwa bei inayozingatia maslahi ya
wazalishaji, wafanyabiashara na wananchi.
KICHERE ASISITIZA UMUHIMU WA KUIMARISHA USHIRIKIANO KATI YA TAASISI ZA UKAGUZI, MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere, amesisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi za ukaguzi, mapambano dhidi ya rushwa na udhibiti wa manunuzi ya umma katika kuzuia upotevu wa rasilimali za Serikali na kukabiliana na utakatishaji fedha.
Ofisi
ya CAG ina jukumu la kufanya ukaguzi unaolenga kuimarisha uwazi, uwajibikaji na
usimamizi bora wa rasilimali za umma.
Ameyasema
hayo leo jijijini Arusha wakati akizungumza katika mkutano wa mwaka wa 19 wa
INTOSAI Working Group on the Fight Against Corruption and Money Laundering
(WGFACML) ulioandaliwa na Ofisi ya Taifa ya ukaguzi (NAOT).
Kichere amesema mapambano dhidi ya rushwa na uhalifu wa kifedha yanahitaji taasisi mbalimbali kufanya kazi kwa pamoja badala ya kila taasisi kutekeleza wajibu wake kwa kujitegemea.
Amesema
ukaguzi wa Serikali haupaswi kuishia katika kubaini dosari baada ya fedha za
umma kutumika, bali unapaswa pia kusaidia kutambua vihatarishi vinavyoweza
kusababisha upotevu wa fedha, ubadhirifu na vitendo vya rushwa mapema.
Tuesday, August 18, 2026
Tuesday, August 11, 2026
KLABU YA FENERBAHCE IMEFIKIA MAKUBALIANO NA NAPOLI YA KUMSAJILI MSHAMBULIAJI, ROMELU LUKAKU
Klabu ya Fenerbahce ya Nchini Uturuki imefikia makubaliano na na Napoli ya Italia juu ya kumsajili mshambuliaji, Romelu Lukaku (33) kwa ada ya uhamisho ya euro milioni 6 itakayofikia euro milioni 8 pamoja na nyongeza.
Nyota
huyo wa Kimataifa wa Ubelgiji tayari amefikia makubaliano ya maslahi binafsi na
klabu hiyo na anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka miwili na chaguo la ongezeko
la mwaka mmoja zaidi.
Mshambuliaji
huyo wa zamani Chelsea na Manchester United anatarajiwa kutia kibindoni
mshahara wa Euro milioni 10 (zaidi ya Tsh bilioni 30.5) kwa mwaka.
Miaka
mitano iliyopita Chelsea ilimsajili nyota huyo kwa dau la Euro milioni 113
akitokea Inter Milan kabla ya kuuzwa kwenda Napoli kwa dau la Euro milioni 30.7
mnamo Agosti 2024 na sasa anatarajiwa kutimkia Uturuki kwa dau la Euro milioni
8.
Wednesday, August 5, 2026
Monday, August 3, 2026
UNAPOKUWA NA MOYO WA KUSHUKURU MUNGU ANAKUONGEZA AFYA, NGUVU, UWEZO NA FAIDA YA KUISHA NA WATU.
Imeelezwa kuwa unapokuwa na moyo wa kushukuru Mungu anakuongeza afya, nguvu, uwezo na faida ya kuisha na watu katika maisha yako.
Hayo yamesemwa na mchungaji kiongozi mama Anna Davie katika ibada ya chuo kikuu cha Manabii iliyofanyika jana katika nyumba ya matamko kisongo Arusha ambapo ilikuwa ni ibada ya shukrani kuu mbele za Mungu.
Naye Askofu Msaidizi Ken Davie alipata nafasi ya kuzungumza katika ibada hiyo na amesema kuwa kila mmoja na wajibu wa kuupendezesha ufalme wa Mungu huku akiongeza kuwa hata shukrani zetu zinatakiwa ziwe harufu nzuri kwa mungu.
Mtume Rose Abel alitapanafasi ya kuhubiri na amemtaka kila mtu kuwa na utaratibu wa kumshukuru mungu hata anapopitia changamoto mbalimbali katika maisha.








































%20Instagram.png)
%20Instagram.png)
%20Instagram.png)










