Friday, July 31, 2026

RAIS SAMIA KUFANYA ZIARA YA KIKAZI NCHINI ANGOLA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Luanda, Angola ambapo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla ya Uzinduzi wa Hospitali iliyopewa jina la Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, tarehe 31 Julai.




TAZAMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO JULAI 31, 2026

 













Tuesday, July 28, 2026

DAGLO ASEMA WAPIGANAJI WAKE "HURU SASA" KUPAMBANA NA JESHI

Mkuu wa wanamgambo wa RSF nchini Sudan Mohamed Hamdan Daglo amewaambia wapiganaji wake kuwa "wameachiliwa huru" sasa kupambana na jeshi la nchi hiyo.

Ujumbe huu wa Daglo kwa wapiganaji wake ambao wametuhumiwa kwa mauaji ya kimbari unakuja siku moja baada ya kupoteza udhibiti wa barabara moja kuu kati ya Mji Mkuu Khartoum na mji mkubwa wa eneo la Kordofan wa El-Obeid.

Kwa wiki kadhaa sasa Umoja wa Mataifa umeonya kuwa huenda wapiganaji wa RSF wakasababisha mauaji makubwa katika eneo la Kordofan, wakati wanapotafuta kuuzingira mji wa El-Obeid kuelekea uvamizi mkubwa wanaotazamia kuufanya.

Wafanyakazi wa misaada ya kiutu wanakadiria kuwa tangu Aprili 2023, vita kati ya wapiganaji wa Daglo na mkuu wa jeshi Abdel Fattah al-Burhan vimesababisha vifo vya zaidi ya watu laki mbili na kusababisha mgogoro mkubwa zaidi duniani wa njaa na raia kuyakimbia makaazi yao.

 

Chanzo: DW


PROF. GEORDAVIE MAFANIKIO HAYAJAWEKWA KWA AJILI YA WATU FULANI


Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie amewataka watu kutambua kwamba kufanikiwa hakuji tu na wala mafanikio hayajawekwa kwa ajili ya watu fulani.

Ameyaema hayo mwishoni mwa wiki {Julai 25, 2026} wakati akifundisha katika mkutano wa akili ya fedha uliofanyika katika ukumbi wa PAPU Tower uliopo Philips jijini Arusha.

Akifundisha Prof. GeorDavie amesema mafanikio hayajawekwa kwa ajili ya watu Fulani ni mtazamo jambo ambalo amesema ni tatizo linawasumbua watu wengi kutokana na Fikra za mambo yaliyopita.


                                                               Habari Na Beatrice Maina

UNAIDS: DUNIA IKO HATARINI KWA MLIPUKO MWENGINE WA UKIMWI



Umoja wa Mataifa unasema kuna dunia iko kwenye hatari ya kuzuka tena kwa mlipuko wa virusi vya ukimwi.

Shirika la umoja wa Mataifa linaloshughulikia UKIMWI UNAIDS limesema hii ni kutokana na ufadhili duniani kupungua pakubwa mwaka jana.

Katika ripoti yake ya kurasa 60 iliyozinduliwa huko Brazil kuelekea kuanza kwa Kongamano la Kimataifa la UKIMWI, Umoja wa Mataifa unasema jamii ya kimataifa imeingia katika enzi za siasa na ubanaji wa fedha mambo yanayotishia kuharibu mazuri yote yaliyopatikana kwa miongo kadhaa katika vita dhidi ya virusi hivyo.

Shirika la UNAIDS linasema ufadhili ulipungua kwa asilimia 18 mwaka 2025 hadi dola bilioni 7.3 hicho kikiwa kiwango cha chini zaidi katika karibu miongo miwili.

Kabla kuingia madarakani kwa Donald Trump, Marekani ndiyo iliyokuwa mfadhili mkuu ikichangia asilimia 75 ya ufadhili jumla wa dunia.

Chanzo: DW


UMEME JUA KISHAPU AWAMU YA PILI KUIONGEZEA TANZANIA MEGAWATI 100 ZA NISHATI JADIDIFU

Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) imeingia hatua mpya ya kuongeza vyanzo vya uzalishaji umeme baada ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa awamu ya pili ya Mradi wa umeme kwa nguvu ya Jua Kishapu utakaozalisha jumla ya megawati 100.

Hatua hiyo imekuja baada ya kukamilika kwa awamu ya kwanza ya mradi huo wenye uwezo wa kuzalisha jumla ya megawati 50 na kuingizwa katika Gridi ya Taifa, jambo lililoongeza uwezo na uthabiti wa gridi hiyo na kuimarisha upatikanaji wa umeme katika maeneo mbalimbali nchini.

Akizungumza katika hafla hiyo Julai 27, 2026, Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema sekta ya nishati ni mhimili wa maendeleo ya Taifa ambapo Serikali inaendelea kufanya jitihada za kuongeza vyanzo mseto vya uzalishaji wa umeme (Energy Mix) ili kuhakikisha Tanzania haitegemei chanzo kimoja pekee cha uzalishaji wa umeme.


TAZAMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO JULAI 28, 2026