Kambi ya matibabu ya bure iliyofanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha, imefanikiwa kutoa huduma kwa wagonjwa zaidi ya 24,871, hatua inayoonyesha mwitikio mkubwa wa wananchi katika kupata huduma za afya za kibingwa na kibobezi.
Idadi hiyo inaonesha
mafanikio makubwa ya kambi hiyo iliyowaleta pamoja madaktari bingwa na wabobezi
kutoka hospitali na taasisi mbalimbali nchini, wakitoa huduma za uchunguzi,
matibabu, vipimo na ushauri wa afya bila malipo kwa wananchi kutoka Arusha na
mikoa jirani.
Makonda amesema
kuwa,Kambi ya matibabu ya madaktari bingwa imefanikiwa kubaini wananchi 1,930
waliokuwa na shinikizo la juu la damu bila kufahamu hali zao za kiafya, hatua
iliyotajwa kuwa muhimu katika kuzuia madhara ya magonjwa yasiyoambukiza kupitia
uchunguzi wa mapema.
Akizungumza na waandishi
wa habari baada ya kukamilika kwa kambi hiyo, Mbunge wa Arusha ambaye pia ni
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Mhe. Paul Makonda, amesema jumla
ya wananchi 6,070 walifanyiwa uchunguzi wa shinikizo la damu, ambapo asilimia
65 walibainika kuwa na tatizo hilo
Amesema kati yao,
wananchi 1,930 waligundulika kwa mara ya kwanza kuwa na ugonjwa huo na
wataendelea kufuatiliwa na wataalamu wa afya ili kupata matibabu na ushauri
unaostahili.


























%20Instagram.png)
%20Instagram.png)
%20Instagram.png)





















