Tukio hilo lilitokea
Jumatano usiku mara baada ya Argentina kuifunga England mabao mawili kwa moja
katika nusu fainali ya Kombe la Dunia.
Wachezaji wa Argentina walisherehekea
ushindi huo kwa kubeba bango lililoandikwa "Visiwa vya Falkland ni vya
Argentina."
Serikali ya Uingereza,
kupitia ofisi ya Waziri Mkuu, imeunga mkono wito wa kutaka FIFA ichukue hatua
kali dhidi ya mabingwa hao watetezi. Visiwa vya Falkland ni eneo la ng'ambo la
Uingereza tangu vita vya mwaka 1982, na wananchi wake walipiga kura mwaka 2013
kusalia chini ya Uingereza.
Sheria za FIFA zinakataza
vikali ujumbe wa kisiasa uwanjani, na tayari Argentina ilishawahi kupigwa faini
kwa kosa kama hili mwaka 2024.






















%20Facebook.png)
%20Facebook.png)
%20Facebook.png)
























