Monday, July 6, 2026

HUENDA WACHEZAJI HAWA TUSIWAONE FANALI ZA WORLD CUP 2030

Hizi ni Picha za Ma-legendi kutoka Mataifa mbali mbali yaliyoshiriki kombe la Dunia 2026 Huko Mexico, Marekani na Canada na tayari wameshaondolewa

Christiano Ronaldo Mwenye Miaka 41 Ureno 

Luca Modric Mwenye Miaka 40 Croatia 

Manuel Neur Mwenye Miaka 40 Ujerumani 

Neymar Santos Jr Miaka 34 Brazil 

Ma-legendi hawa wote huenda tusiwaone katika Kombe la Dunia 2030 kwani tayari baadhi yao wametangaza kustafu soka la kimataifa wakiwa timu na zao za taifa

Tizama wanavyohuzunika



RAIS DKT. SAMIA AMTEMBELEA PACOME HOSPITALINI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amemtembelea kiungo wa Yanga SC, Pacome Zouzoua, anayepatiwa matibabu katika Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam.

Pacome alilazwa hospitalini baada ya kupata majeraha ya mguu wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya NBC, ambapo Yanga SC ilicheza dhidi ya JKT Tanzania. Tukio hilo lilitokea Juni 30, 2026 katika Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Dar es Salaam.



RONALDO NA URENO YAKE YAONDOLEWA KOMBE LA DUNIA NA UHISPANIA

Cristiano na na wenzake wa Ureno wameaga mashindano ya Kombe la Dunia la FIFA 2026 kufuatia kipigo cha 1-0 dhidi ya Uhispania kwenye hatua ya 16 bora katika dimba la Dallas, Texas Marekani.
Uhispania imetinga hatua ya robo fainali na itachuana na mshindi wa mchezo mwingine wa hatua ya 16 bora kati ya wenyeji, Marekani dhidi ya Ubelgiji.
FT: Portugal 🇵🇹 0-1 🇪🇸 Spain
⚽ 90+1 Merino.





WENYEJI MAREKANI WATUPWA NJE WORLD CUP, UBELGIJI IKIIFUATA HISPANIA ROBO FAINALI


Timu ya Taifa ya Ubelgiji ‘The Red Devils’ imetinga hatua ya robo fainali ya Kombe la Dunia la FIFA 2026 kufuatia ushindi wa 4-1 dhidi ya wenyeji wenza wa michuano hiyo, Marekani katika dimba la Seattle, Washington kwenye mchezo wa hatua ya 16 bora.

Ubelgiji itachuana na Uhispania kwenye hatua ya robo fainali, Uhispania ikitinga hatua baada ya kuisukumiza nje Ureno kwenye hatua ya 16 bora.




MAADHIMISHO YA SIKU YA KISWAHILI DUNIANI YAANZA RASMI BURUNDI KWA MIJADALA YA KITAALUMA

Maadhimisho ya 5 ya Siku ya Kiswahili Duniani (MASIKIDU), yanayofanyika tarehe 5 hadi 7 Julai 2026, yamefunguliwa rasmi Nchini Burundi ikiwa ni hatua muhimu ya kihistoria ya kuendeleza lugha ya Kiswahili, yakifanyika sambamba na Kongamano la 3 la Kimataifa la Kiswahili kupitia Kamisheni ya Kiswahili ya Afrika Mashariki (KAKAMA), yakiwakutanisha wadau wa Kiswahili kutoka nchi mbalimbali za Jumuiya ya Afrika Mashariki na kwingineko duniani.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa maadhimisho hayo, Waziri wa Vijana, Michezo na Utamaduni wa Jamhuri ya Burundi, Bi. Lydia Nsekela, amesisitiza kuwa Kiswahili ni nyenzo muhimu ya kuimarisha mshikamano wa kikanda, kukuza utamaduni na kuendeleza ushirikiano kati ya mataifa ya Afrika Mashariki.

Aliongeza kuwa serikali ya Burundi itaendelea kuunga mkono juhudi za kukuza na kueneza matumizi ya Kiswahili katika sekta mbalimbali, ikiwemo elimu, utamaduni na teknolojia.

Maadhimisho hayo yanafanyika chini ya kaulimbiu isemayo “Kiswahili, Wingi-Lugha, na Akili Unde (Kiswahili, Multilingualism and Artificial Intelligence)”, ambapo washiriki wanashiriki mijadala ya kitaaluma, mawasilisho ya mada mbalimbali pamoja na maonesho ya teknolojia yanayoonesha nafasi ya Akili Unde katika maendeleo ya lugha ya Kiswahili.

Kongamano hilo linafanyika likilenga kutoa mapendekezo yatakayochochea matumizi ya Kiswahili katika elimu, utafiti, ubunifu wa kidijitali na ushirikiano wa kimataifa.

kilele cha maadhimisho hayo ni Julai 7, 2026, ambapo shughuli rasmi zitahitimishwa kama sehemu ya kuendeleza ajenda ya kukifanya Kiswahili kuwa lugha ya kimataifa inayochochea maendeleo na umoja wa Afrika Mashariki.

 



Sunday, July 5, 2026

MTU MWENYE IMANI HUMWABUDU MUNGU KWA UTULIVU

Imeelezwa kuwa Mtu mwenye Imani anamwabudu Mungu akiwa mtulivu, mpole na anangoja kwa sababu Mungu ana shughuli naye.

Hayo yamesemwa na Mchungaji Kiongozi Mama Anna Davie wakati akiongoza ibada ya chuo kikuu cha manabii iliyofanyika katika nyumba ya matamko ngurumo ya upako kisongo Arusha ambapo ilikuwa ni ibada ya kupokea nguvu mpya ili kuinuka upya.

Kwa upande wake Mwalimu wa neno la Mungu Isaya Benson akifundisha kuhusu somo lililokuwa na kichwa kisemacho Mapito yamebeba hatma yako amesema kuwa watu wengi wanakimbia mapito wakati ndio njia ya kuwapeleka katika hatma yao.

Naye Mngojezi wa Nabii Mkuu Claudia Silayo akifundisha ibadani hapo amesema kuwa wazazi wahawatakiwi kuwa legelege kwenye malezi ya Watoto.

Pia Mtumishi mwanafunzi Abel Likinjie amepata nafasi ya katika ibada hiyo ambapo amewataka kuwa wavumilivu ili matamko ya kinabii waliyotamkiwa yaweze kutimia maishani mwao na Baba wa kiroho ajivunie wao.




NORWAY YAIFUATA ENGLAND ROBO FAINALI, HAALAND APELEKA KILIO BRAZIL

Norway imeandika historia kwa kutinga hatua ya robo fainali ya Kombe la Dunia 2026 baada ya kuifunga Brazil mabao 2-1 katika mchezo wa hatua ya 16 bora uliochezwa Julai 5,2026

Nyota wa Norway, Erling Haaland, alikuwa shujaa wa mchezo huo baada ya kufunga mabao yote mawili katika dakika za 79 na 90, na kuipeleka nchi yake robo fainali ya Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza katika historia.

Brazil ilipata nafasi kadhaa za kufunga lakini ilishindwa kuzitumia, ikiwemo mkwaju wa penalti uliokoswa kipindi cha kwanza. Neymar aliifungia Brazil bao la kufutia machozi kwa penalti katika muda wa nyongeza.


Kwa ushindi huo, Norway sasa inasonga mbele kusubiri mshindi wa mchezo kati ya Mexico na England katika hatua ya robo fainali, huku Brazil wakiaga mshindano.



TAZAMA YALIYOOANDIKWA KATIKA KURASA ZA MAGAZETI YA TANZANIA KWA SIKU YA LEO JULAI 06, 2026

 

















Wednesday, July 30, 2025

NABII MKUU AWATAKA WATU KUTAMBUA NGUVU NA LUGHA YA NABII MKUU

Nabii Mkuu Mhe.Dkt.GeorDavie amewataka watu kuitambua Nguvu ya Nabii Mkuu na Lugha anayoitumia maana kuna tofauti kati ya Nabii na Nabii Mkuu.

‎Amesema unapomuona Nabii Mkuu umemuona Mtu mwenye Mamlaka katika Serikali Tukufu ya Ufalme wa Mungu na kwamba Neno lake analotamka ndilo linalokuwa.

‎Ameongeza kuwa Nabii Mkuu anapoingia ni Serikali Tukufu ya Ufalme wa Mungu imeingia na kwamba watu wakitambua jambo hilo lazima watafanikiwa kiroho na kimwili kwa kuyashika matamko ya kinabii.

‎Na Beatrice Maina@NYU ARUSHA.

NABII MKUU AWASHUKURU WALIOMPONGEZA KWA KUTUNUKIWA TUZO YA HESHIMA YA UDAKTARI

Nabii Mkuu Mhe.Dkt.GeorDavie amewashukuru watu wote walio mpongeza kwa kupata tuzo ya heshima ya Udaktari aliyokabidhiwa na umoja wa madaktari na maprofessa  julai  5 jijini Dodoma.

Nabii Mkuu ametoa shukrani hizo jana katika ibada ya chuo kikuu cha manabii iliyofanyika ngurumo ya upako kisongo Arusha ambapo ilikuwa ni ibada ya shukrani kwa kuvuka nusu mwaka na kuanza nusu nyingine kwa ushindi.


Akizungumza Nabii Mkuu amesema kuwa watu wote wamekuwa wamiliki wakubwa wa heshima hiyo na amekuja kuwakabidhi heshima hiyo kwa sababu walionyesha mahitaji yao ya kiroho na kimwili na yeye akayaangalia kwa kuwafungua na kuwasapoti.

Thursday, July 24, 2025

HII NDIO CV YA KOCHA MPYA WA KLABU YA YANGA.

 HII NDIO CV YA KOCHA MPYA WA KLABU YA YANGA.

Anaitwa Romain Folz (35) Kocha mpya wa Yanga,ambae alizaliwa Bordeaux,Ufaransa ðŸ‡«ðŸ‡·

Huyu kocha amefanya kazi sehemu zifuatazo👇

2025 Alikuwa Mkurugenzi wa michezo wa Olympique Akbou ya Algeria ðŸ‡©ðŸ‡¿

2024 Alikuwa kocha msaidizi wa Mamelodi Sundown ya South Africa ðŸ‡¿ðŸ‡¦

2023 Alikuwa kocha mkuu wa Horoya ya Guinea ðŸ‡¬ðŸ‡³

2022 Alikuwa kocha mkuu wa Amazulu ya South Africa ðŸ‡¿ðŸ‡¦

2021 Alikuwa kocha Mkuu wa Township Rollers ya Botswana ðŸ‡§ðŸ‡¼

2019 Alikuwa kocha Msaidizi wa Pyramid ya Egypt ðŸ‡ªðŸ‡¬

2018 Alikuwa kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Uganda ðŸ‡ºðŸ‡¬

Huyu kocha ana UEFA Pro Licence na Pro Licence ya CONMEBOL (America).

Huyu kocha ni Muhumini wa (4-3-3) na timu yake ina-press kinoma.