Thursday, July 16, 2026

FIFA KUANGALIA UWEZEKANO WA KUIADHIBU ARGENTINA

Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) linachunguza uwezekano wa kuichukulia hatua za kinidhamu timu ya taifa ya Argentina, baada ya wachezaji wake kuinua bango lenye ujumbe wa kisiasa kuhusu Visiwa vya Falkland.

Tukio hilo lilitokea Jumatano usiku mara baada ya Argentina kuifunga England mabao mawili kwa moja katika nusu fainali ya Kombe la Dunia.

Wachezaji wa Argentina walisherehekea ushindi huo kwa kubeba bango lililoandikwa "Visiwa vya Falkland ni vya Argentina."

Serikali ya Uingereza, kupitia ofisi ya Waziri Mkuu, imeunga mkono wito wa kutaka FIFA ichukue hatua kali dhidi ya mabingwa hao watetezi. Visiwa vya Falkland ni eneo la ng'ambo la Uingereza tangu vita vya mwaka 1982, na wananchi wake walipiga kura mwaka 2013 kusalia chini ya Uingereza.

Sheria za FIFA zinakataza vikali ujumbe wa kisiasa uwanjani, na tayari Argentina ilishawahi kupigwa faini kwa kosa kama hili mwaka 2024.

TANZANIA KUONGEZA KASI KATIKA HUDUMA YA UPANDIKIZAJI WA ULOTO


Serikali imeeleza dhamira yake ya kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha huduma za afya za kibingwa katika Afrika Mashariki na Kati huku ikitoa wito kwa Watanzania na wadau mbalimbali kushiriki kuchangia Mfuko wa Upandikizaji wa Figo na Uloto ili kuwawezesha wagonjwa wasiokuwa na uwezo kupata matibabu yanayookoa maisha.

Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa (Mb), wakati akiwasilisha taarifa kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), katika hafla ya chakula cha pamoja cha kuchangisha fedha kwa ajili ya kugharamia huduma za upandikizaji wa figo na uloto katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, iliyofanyika jijini Dodoma.


TAZAMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO JULAI 17, 2026











 

Monday, July 13, 2026

MHE. NABII MKUU PROF. GEORDAVIE ATOA KIASI CHA SHILINGI MILIONI 58

Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie leo ametoa kiasi cha shilingi milioni 58 ambapo shilingi milioni 53 ni kwa ajili ya kusapoti maono ya rais wa umoja wa makanisa ya kitume na kinabii tanzania Nabii Dkt. Joshua Mwantyala na shilingi milioni 5 kwa mchungaji hananja.

Ametoa fedha hizo alipokuwa akizungumza na mitume na manabii kupitia kongamano la kurejesha thamani lililofanyika Morogoro katika huduma ya Nabii Dkt. Joshua ambaye pia ndio muandaaji wa kongamano hilo ambapo shilingi miloni 50 ni kwa ajili ya kuendeleza maono, shilingi milioni tatu kwa ajili ya nh’ombe wa maziwa ikiwa ni zawadi ya kumbukizi yake ya siku ya kuzaliwa.

Amempongeza na kufurahishwa na maono yake na kusema kuwa kiasi hicho cha fedha amempa ili zimsaidie kuendeleza maono yake.

MHE. NABII MKUU PROF. GEORDAVIE AWATAKA WATUMISHI WA MUNGU KUWA NA UMOJA NA UPENDO

Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie mlezi wa umoja wa makanisa ya kitume na kinabii amewataka watumishi wa mungu kuwa na umoja na upendo ili mungu aweze kuonekana katika utumishi wao.

Ameyasema hayo jumapili ya July 12, 2026 alipokuwa akizungumza  na watumishi wa mungu, wachungaji, walimu, wainjilisti, mitume na manabii kupitia kongamano la kurejesha thamani lililofanyika Mkoani Morogoro.

Akizungumza Nabii Mkuu amesema kuwa upendo wa kweli unakosekana kwa watumishi ka sababu kuna mafarakano mengi ambayo yanasababisha Mungu asionekane.

Amesema watumishi wa Mungu watakaposhikana mungu ataonekana zaidi na watafanya kazi zaidi katika huduma zao.


Sunday, July 12, 2026

MHE. NABII MKUU PROF. GEORDAVIE AMEMUWEKA WAKFU MTUMISHI WA MUNGU NABII JOSHUA MWANTYALA


Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie amemuweka Wakfu Mtumishi wa Mungu Nabii Joshua Mwantyala ambaye pia ni Rais wa umoja wa makanisa ya kitume na Kinabii Tanzania.

Zoezi hilo amelifanya kupitia siku ya mwisho ya kongamano la siku tatu la kurejesha thamani aliloliandaa mkoani Morogoro ambapo wakfu huo amemuweka kwa kummiminia mafuta yeye kama Madhabahu na kumpokea rasmi kama mtoto wake wa kiroho.

Akimuweka wakfu Nabii Mkuu ametamka ya kuwa majira mapya yanakuja huku akiachilia matamko kwa Nabii Joshua kuwa na baraka za uwepo wa Mungu, Baraka ya ulinzi, baraka ya uongozi ambapo na alimkabidhi kipaza sauti microphone kama baraka ya fimbo kwa musa na kwamba atakapoongea sauti yake itakwenda juu sana kwa nchi na itakuwa na mamlaka yenye utiisho.


WAZIRI DEUS SANGU AWAOMBA WATUMISHI WA MUNGU KUENDELEA KUDUMISHA AMANI YA NCHI


Waziri wa nchi, ofisi ya Waziri mkuu, kazi, ajira na mahusiano ya kazi Deusi Sangu amewaomba watumishi wa mungu waendelee kudumisha umaadili, mshikamano na amani ya nchi.

Ameyasema hayo katika kongamano la kurejesha thamani, lililofanyika Mkoani Morogoro ambalo pia lilikuwa na lengo la kuiombea nchi ambapo ameongeza kuwa serikali inawatambua na kuwathamani watumishi wa mungu.

Amesema katika kuishi dhamira hiyo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani wakati akizindua bunge la 13 aliipa wizara yake jukumu la kuratibu mahusiano baina ya serikali na makundi ya kijamii ambapo uratibu huo unahusisha wadau wa siasa, taasisi za dini, Asasi za Kiraia na mashirika yasiyo ya kiserikali na kwamba wanafanya kazi na wadau hao wote kwa karibu ili kuhakikisha wanaimarisha amani, utulivu upendo, mshikamano na maridhiano ya kitaifa.

Amesema mambo hayo ndio nguzo kuu na mahusiano na dhamira ya maendeleo ya taifa ya mwaka 2026.


TAZAMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO JULAI 13, 2026

 















Wednesday, July 8, 2026

MAREKANI YAANZISHA UPYA MASHAMBULIZI NCHINI IRAN


Marekani imefanya mashambulizi mapya ya anga dhidi ya Iran mapema leo, hatua iliyojibiwa na Iran kwa kuyalenga mataifa ya Bahrain, Kuwait na Qatar. Hali hii inaongeza mvutano na kuhatarisha tena makubaliano ya muda yaliyolenga kutafuta njia ya kumaliza vita.

Jeshi la Marekani lilishambulia maeneo mbalimbali ya kijeshi na miundombinu ya bandari mapema Jumatano, kufuatia mashambulizi ya Iran dhidi ya meli kadhaa za biashara katika pwani ya Oman, hali iliyosababisha Iran kujibu kwa mashambulizi mengine.

Mashambulizi ya Marekani yalifanywa saa chache baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kusema makubaliano hayo yamefika mwisho kufuatia mashambulizi hayo ya Iran.

Hata hivyo, mashambulizi ya Alhamisi yalionekana kuwa makubwa zaidi kuliko ya awali huku Jeshi la Kuwait likisema limezuia na kudungua droni pamoja na makombora yaliyoelekezwa nchini humo.

Vyombo vya habari vya serikali ya Iran viliripoti milipuko katika maeneo kadhaa, yakiwemo Bushehr, ambako kuna kituo cha nishati ya nyuklia cha Iran, pamoja na miji ya bandari ya kusini ya Chabahar, Konarak, Bandar Abbas na Sirik.

Chanzo: DW