Wednesday, July 8, 2026

MAREKANI YAANZISHA UPYA MASHAMBULIZI NCHINI IRAN


Marekani imefanya mashambulizi mapya ya anga dhidi ya Iran mapema leo, hatua iliyojibiwa na Iran kwa kuyalenga mataifa ya Bahrain, Kuwait na Qatar. Hali hii inaongeza mvutano na kuhatarisha tena makubaliano ya muda yaliyolenga kutafuta njia ya kumaliza vita.

Jeshi la Marekani lilishambulia maeneo mbalimbali ya kijeshi na miundombinu ya bandari mapema Jumatano, kufuatia mashambulizi ya Iran dhidi ya meli kadhaa za biashara katika pwani ya Oman, hali iliyosababisha Iran kujibu kwa mashambulizi mengine.

Mashambulizi ya Marekani yalifanywa saa chache baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kusema makubaliano hayo yamefika mwisho kufuatia mashambulizi hayo ya Iran.

Hata hivyo, mashambulizi ya Alhamisi yalionekana kuwa makubwa zaidi kuliko ya awali huku Jeshi la Kuwait likisema limezuia na kudungua droni pamoja na makombora yaliyoelekezwa nchini humo.

Vyombo vya habari vya serikali ya Iran viliripoti milipuko katika maeneo kadhaa, yakiwemo Bushehr, ambako kuna kituo cha nishati ya nyuklia cha Iran, pamoja na miji ya bandari ya kusini ya Chabahar, Konarak, Bandar Abbas na Sirik.

Chanzo: DW

WAIRAN KUMZIKA AYATOLLAH ALI KHAMENEI NYUMBANI KWAKE MASSHAD

Raia nchini Iran hii leo wanajiandaa kumzika kiongozi wao Ali Khamenei, katika mji alikozaliwa wa Mashhad, huku mashambulizi mapya ya Marekani yakitishia kusababisha ongezeko jipya la mvutano.

Mazishi ya kiongozi huyo mkuu wa zamani yanafuatia ibada za maombolezo zilizodumu kwa siku kadhaa na kuhudhuriwa na mamilioni ya waombolezaji katika miji mbalimbali nchini Iran na Iraq.

Ali Khamenei aliuawa Februari 28, siku ya kwanza ya mashambulizi ya Marekani na Israel nchini Iran yaliyochochea vita hivyo.

Baada ya maandamano makubwa ya mazishi yaliyopita katika miji mitakatifu ya Najaf na Karbala nchini Iraq siku ya Jumatano, mwili wake ulitarajiwa kufikishwa katika makazi yake ya mwisho katika mji mtakatifu wa Mashhad.

Gavana wa Mashhad, Hassan Hosseini alinukuliwa na televisheni ya serikali akisema kuwa "anatarajia watu milioni 15” kuhudhuria mazishi hayo ya Khamenei.

Chanzo: DW


MANCHESTER UNITED YAANGUKIA KWA ANDREY SANTOS BAADA YA KUMKOSA MATEUS FERNANDES


Klabu ya Manchester United imefikia makubaliano na Chelsea juu ya kumsajili kiungo, Andrey Santos kwa ada ya uhamisho ya Euro milioni 56 pamoja na nyongeza ya Euro milioni 2.4 huku Chelsea akipachika kifungu cha asilimia 10 za mauzo ya siku za usoni.

Santos 22, raia wa Brazil tayari amefikia makubaliano ya maslahi binafsi na mashetani hao Wekundu na tayari amepata ruhusa ya kufanya vipimo vya afya kabla ya kukamilika uhamisho huo.

Mashetani hao Wekundu ambao pia wanatarajiwa kumtangaza, Mbrazil mwingine, Ederson kama mchezaji mpya walilazimika kutafuta kiungo mwingine kwa ajili ya kurithi mikoba ya Casemiro ikiwa ni baada ya kuangukia pua katika jitihada zao za kuinasa saini ya Mateus Fernandes aliyetimkia Tottenham Hotspur.

TAZAMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO JULAI 09, 2026

 













Monday, July 6, 2026

HUENDA WACHEZAJI HAWA TUSIWAONE FANALI ZA WORLD CUP 2030

Hizi ni Picha za Ma-legendi kutoka Mataifa mbali mbali yaliyoshiriki kombe la Dunia 2026 Huko Mexico, Marekani na Canada na tayari wameshaondolewa

Christiano Ronaldo Mwenye Miaka 41 Ureno 

Luca Modric Mwenye Miaka 40 Croatia 

Manuel Neur Mwenye Miaka 40 Ujerumani 

Neymar Santos Jr Miaka 34 Brazil 

Ma-legendi hawa wote huenda tusiwaone katika Kombe la Dunia 2030 kwani tayari baadhi yao wametangaza kustafu soka la kimataifa wakiwa timu na zao za taifa

Tizama wanavyohuzunika



RAIS DKT. SAMIA AMTEMBELEA PACOME HOSPITALINI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amemtembelea kiungo wa Yanga SC, Pacome Zouzoua, anayepatiwa matibabu katika Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam.

Pacome alilazwa hospitalini baada ya kupata majeraha ya mguu wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya NBC, ambapo Yanga SC ilicheza dhidi ya JKT Tanzania. Tukio hilo lilitokea Juni 30, 2026 katika Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Dar es Salaam.



RONALDO NA URENO YAKE YAONDOLEWA KOMBE LA DUNIA NA UHISPANIA

Cristiano na na wenzake wa Ureno wameaga mashindano ya Kombe la Dunia la FIFA 2026 kufuatia kipigo cha 1-0 dhidi ya Uhispania kwenye hatua ya 16 bora katika dimba la Dallas, Texas Marekani.
Uhispania imetinga hatua ya robo fainali na itachuana na mshindi wa mchezo mwingine wa hatua ya 16 bora kati ya wenyeji, Marekani dhidi ya Ubelgiji.
FT: Portugal 🇵🇹 0-1 🇪🇸 Spain
⚽ 90+1 Merino.





WENYEJI MAREKANI WATUPWA NJE WORLD CUP, UBELGIJI IKIIFUATA HISPANIA ROBO FAINALI


Timu ya Taifa ya Ubelgiji ‘The Red Devils’ imetinga hatua ya robo fainali ya Kombe la Dunia la FIFA 2026 kufuatia ushindi wa 4-1 dhidi ya wenyeji wenza wa michuano hiyo, Marekani katika dimba la Seattle, Washington kwenye mchezo wa hatua ya 16 bora.

Ubelgiji itachuana na Uhispania kwenye hatua ya robo fainali, Uhispania ikitinga hatua baada ya kuisukumiza nje Ureno kwenye hatua ya 16 bora.




MAADHIMISHO YA SIKU YA KISWAHILI DUNIANI YAANZA RASMI BURUNDI KWA MIJADALA YA KITAALUMA

Maadhimisho ya 5 ya Siku ya Kiswahili Duniani (MASIKIDU), yanayofanyika tarehe 5 hadi 7 Julai 2026, yamefunguliwa rasmi Nchini Burundi ikiwa ni hatua muhimu ya kihistoria ya kuendeleza lugha ya Kiswahili, yakifanyika sambamba na Kongamano la 3 la Kimataifa la Kiswahili kupitia Kamisheni ya Kiswahili ya Afrika Mashariki (KAKAMA), yakiwakutanisha wadau wa Kiswahili kutoka nchi mbalimbali za Jumuiya ya Afrika Mashariki na kwingineko duniani.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa maadhimisho hayo, Waziri wa Vijana, Michezo na Utamaduni wa Jamhuri ya Burundi, Bi. Lydia Nsekela, amesisitiza kuwa Kiswahili ni nyenzo muhimu ya kuimarisha mshikamano wa kikanda, kukuza utamaduni na kuendeleza ushirikiano kati ya mataifa ya Afrika Mashariki.

Aliongeza kuwa serikali ya Burundi itaendelea kuunga mkono juhudi za kukuza na kueneza matumizi ya Kiswahili katika sekta mbalimbali, ikiwemo elimu, utamaduni na teknolojia.

Maadhimisho hayo yanafanyika chini ya kaulimbiu isemayo “Kiswahili, Wingi-Lugha, na Akili Unde (Kiswahili, Multilingualism and Artificial Intelligence)”, ambapo washiriki wanashiriki mijadala ya kitaaluma, mawasilisho ya mada mbalimbali pamoja na maonesho ya teknolojia yanayoonesha nafasi ya Akili Unde katika maendeleo ya lugha ya Kiswahili.

Kongamano hilo linafanyika likilenga kutoa mapendekezo yatakayochochea matumizi ya Kiswahili katika elimu, utafiti, ubunifu wa kidijitali na ushirikiano wa kimataifa.

kilele cha maadhimisho hayo ni Julai 7, 2026, ambapo shughuli rasmi zitahitimishwa kama sehemu ya kuendeleza ajenda ya kukifanya Kiswahili kuwa lugha ya kimataifa inayochochea maendeleo na umoja wa Afrika Mashariki.