Tuesday, July 14, 2026
Monday, July 13, 2026
MHE. NABII MKUU PROF. GEORDAVIE ATOA KIASI CHA SHILINGI MILIONI 58
Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie leo ametoa kiasi cha shilingi
milioni 58 ambapo shilingi milioni 53 ni kwa ajili ya kusapoti maono ya rais wa
umoja wa makanisa ya kitume na kinabii tanzania Nabii Dkt. Joshua Mwantyala na
shilingi milioni 5 kwa mchungaji hananja.
Ametoa fedha hizo alipokuwa akizungumza na mitume na manabii
kupitia kongamano la kurejesha thamani lililofanyika Morogoro katika huduma ya Nabii
Dkt. Joshua ambaye pia ndio muandaaji wa kongamano hilo ambapo shilingi miloni
50 ni kwa ajili ya kuendeleza maono, shilingi milioni tatu kwa ajili ya nh’ombe
wa maziwa ikiwa ni zawadi ya kumbukizi yake ya siku ya kuzaliwa.
Amempongeza na kufurahishwa na maono yake na kusema kuwa
kiasi hicho cha fedha amempa ili zimsaidie kuendeleza maono yake.
MHE. NABII MKUU PROF. GEORDAVIE AWATAKA WATUMISHI WA MUNGU KUWA NA UMOJA NA UPENDO
Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie mlezi wa umoja wa makanisa ya
kitume na kinabii amewataka watumishi wa mungu kuwa na umoja na upendo ili
mungu aweze kuonekana katika utumishi wao.
Ameyasema hayo jumapili ya July 12, 2026 alipokuwa
akizungumza na watumishi wa mungu, wachungaji, walimu, wainjilisti, mitume na manabii kupitia kongamano
la kurejesha thamani lililofanyika Mkoani Morogoro.
Akizungumza Nabii Mkuu amesema kuwa upendo wa kweli
unakosekana kwa watumishi ka sababu kuna mafarakano mengi ambayo yanasababisha Mungu
asionekane.
Amesema watumishi wa Mungu watakaposhikana mungu ataonekana
zaidi na watafanya kazi zaidi katika huduma zao.
Sunday, July 12, 2026
MHE. NABII MKUU PROF. GEORDAVIE AMEMUWEKA WAKFU MTUMISHI WA MUNGU NABII JOSHUA MWANTYALA
Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie amemuweka Wakfu Mtumishi wa
Mungu Nabii Joshua Mwantyala ambaye pia ni Rais wa umoja wa makanisa ya kitume
na Kinabii Tanzania.
Zoezi hilo amelifanya kupitia siku ya mwisho ya kongamano la
siku tatu la kurejesha thamani aliloliandaa mkoani Morogoro ambapo wakfu huo
amemuweka kwa kummiminia mafuta yeye kama Madhabahu na kumpokea rasmi kama
mtoto wake wa kiroho.
Akimuweka wakfu Nabii Mkuu ametamka ya kuwa majira mapya
yanakuja huku akiachilia matamko kwa Nabii Joshua kuwa na baraka za uwepo wa
Mungu, Baraka ya ulinzi, baraka ya uongozi ambapo na alimkabidhi kipaza sauti
microphone kama baraka ya fimbo kwa musa na kwamba atakapoongea sauti yake
itakwenda juu sana kwa nchi na itakuwa na mamlaka yenye utiisho.
WAZIRI DEUS SANGU AWAOMBA WATUMISHI WA MUNGU KUENDELEA KUDUMISHA AMANI YA NCHI
Waziri wa nchi, ofisi ya Waziri mkuu, kazi, ajira na
mahusiano ya kazi Deusi Sangu amewaomba watumishi wa mungu waendelee
kudumisha umaadili, mshikamano na amani ya nchi.
Ameyasema hayo katika kongamano la kurejesha thamani, lililofanyika Mkoani Morogoro ambalo pia
lilikuwa na lengo la kuiombea nchi ambapo ameongeza kuwa serikali inawatambua
na kuwathamani watumishi wa mungu.
Amesema katika kuishi dhamira hiyo Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani wakati akizindua bunge la
13 aliipa wizara yake jukumu la kuratibu mahusiano baina ya serikali na makundi
ya kijamii ambapo uratibu huo unahusisha wadau wa siasa, taasisi za dini, Asasi
za Kiraia na mashirika yasiyo ya kiserikali na kwamba wanafanya kazi na wadau
hao wote kwa karibu ili kuhakikisha wanaimarisha amani, utulivu upendo,
mshikamano na maridhiano ya kitaifa.
Amesema mambo hayo ndio nguzo kuu na mahusiano na dhamira ya
maendeleo ya taifa ya mwaka 2026.
Thursday, July 9, 2026
Wednesday, July 8, 2026
MAREKANI YAANZISHA UPYA MASHAMBULIZI NCHINI IRAN
Marekani imefanya mashambulizi mapya ya anga dhidi ya Iran mapema leo, hatua iliyojibiwa na Iran kwa kuyalenga mataifa ya Bahrain, Kuwait na Qatar. Hali hii inaongeza mvutano na kuhatarisha tena makubaliano ya muda yaliyolenga kutafuta njia ya kumaliza vita.
Jeshi la Marekani lilishambulia
maeneo mbalimbali ya kijeshi na miundombinu ya bandari mapema Jumatano,
kufuatia mashambulizi ya Iran dhidi ya meli kadhaa za biashara katika pwani ya
Oman, hali iliyosababisha Iran kujibu kwa mashambulizi mengine.
Mashambulizi
ya Marekani yalifanywa saa chache baada ya Rais wa Marekani
Donald Trump kusema makubaliano hayo yamefika mwisho kufuatia mashambulizi hayo
ya Iran.
Hata hivyo, mashambulizi ya
Alhamisi yalionekana kuwa makubwa zaidi kuliko ya awali huku Jeshi la Kuwait
likisema limezuia na kudungua droni pamoja na makombora yaliyoelekezwa nchini
humo.
Vyombo vya habari vya serikali ya
Iran viliripoti milipuko katika maeneo kadhaa, yakiwemo Bushehr, ambako kuna
kituo cha nishati ya nyuklia cha Iran, pamoja na miji ya bandari ya kusini ya
Chabahar, Konarak, Bandar Abbas na Sirik.
Chanzo: DW
WAIRAN KUMZIKA AYATOLLAH ALI KHAMENEI NYUMBANI KWAKE MASSHAD
Raia nchini Iran hii leo
wanajiandaa kumzika kiongozi wao Ali Khamenei, katika mji alikozaliwa wa
Mashhad, huku mashambulizi mapya ya Marekani yakitishia kusababisha ongezeko
jipya la mvutano.
Mazishi ya kiongozi huyo mkuu wa
zamani yanafuatia ibada za maombolezo zilizodumu kwa siku kadhaa na kuhudhuriwa
na mamilioni ya waombolezaji katika miji mbalimbali nchini Iran na Iraq.
Ali Khamenei aliuawa
Februari 28, siku ya kwanza ya mashambulizi ya Marekani na Israel nchini
Iran yaliyochochea vita hivyo.
Baada ya maandamano makubwa ya
mazishi yaliyopita katika miji mitakatifu ya Najaf na Karbala nchini Iraq siku
ya Jumatano, mwili wake ulitarajiwa kufikishwa katika makazi yake ya mwisho
katika mji mtakatifu wa Mashhad.
Gavana wa Mashhad, Hassan
Hosseini alinukuliwa na televisheni ya serikali akisema kuwa
"anatarajia watu milioni 15” kuhudhuria mazishi hayo ya Khamenei.
Chanzo: DW
MANCHESTER UNITED YAANGUKIA KWA ANDREY SANTOS BAADA YA KUMKOSA MATEUS FERNANDES
Klabu ya Manchester United imefikia makubaliano na Chelsea juu ya kumsajili kiungo, Andrey Santos kwa ada ya uhamisho ya Euro milioni 56 pamoja na nyongeza ya Euro milioni 2.4 huku Chelsea akipachika kifungu cha asilimia 10 za mauzo ya siku za usoni.
Santos 22, raia wa Brazil tayari amefikia makubaliano ya maslahi binafsi na mashetani hao Wekundu na tayari amepata ruhusa ya kufanya vipimo vya afya kabla ya kukamilika uhamisho huo.
Mashetani hao Wekundu ambao pia wanatarajiwa kumtangaza, Mbrazil mwingine, Ederson kama mchezaji mpya walilazimika kutafuta kiungo mwingine kwa ajili ya kurithi mikoba ya Casemiro ikiwa ni baada ya kuangukia pua katika jitihada zao za kuinasa saini ya Mateus Fernandes aliyetimkia Tottenham Hotspur.










%20Facebook.png)
%20Facebook.png)
%20Facebook.png)






































