Serikali imewapa siku
saba wamiliki wa viwanda vya kuzalisha saruji nchini kuwasilisha mapendekezo ya
namna ya kutatua changamoto ya bei ya saruji inayotajwa kuwa juu katika soko
pamoja na upatikanaji wake.
Hatua hiyo imefikiwa
baada ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Balozi Waziri Salum,
kukutana na kufanya mazungumzo na wamiliki wa viwanda vya saruji Agosti 18,
2026 jijini Dodoma.
Salum amesema, kikao
kimelenga kutafuta suluhu ya changamoto iliyosababisha kuadimika kwa bidhaa
hiyo na bei kuwa juu sokoni.
Kikao hicho kimehudhuriwa
pia na viongozi wa taasisi mbalimbali zinazohusika na udhibiti, viwango na
masoko, ikiwemo Tume ya Ushindani (FCC), Shirika la Viwango Tanzania (TBS),
TanTrade, pamoja na Wakurugenzi kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara.
Akizungumza katika kikao
hicho, Balozi Salum amesisitiza umuhimu wa kupata suluhu ya kudumu
itakayosaidia kuhakikisha saruji inapatikana kwa bei inayozingatia maslahi ya
wazalishaji, wafanyabiashara na wananchi.

No comments:
Post a Comment