Mchungaji Kiongozi Mama Anna Davie amewashukuru na kufurahishwa na wana international Partner ambao wanatoa fedha zao kwa moyo wakupenda kwa ajili ya kusapoti maono ya Mtu mkuu wa Mungu.
Ameyasema hayo hii leo wakati wa ibada ya chuo kikuu cha manabii iliyofanyika katika nyumba nyumba ya matamko ngurumo ya upako kisongo.Akizungumza amesema kuwa
ni jambo la ajabu mtu kutoa kwa hiari na kwa furaha kwa ajili ya kutimiza kazi
ya huduma huku wakitegemea kupokea baraka.
Naye Mtume Elisifa
Kephasi akifundisha somo la chagua kwenda mbele sio kurudi nyuma amesema kuwa
katika kwenda mbele lazima uchague kwenda na Mungu na sio kundi la watu kwa
sababu watu wanaweza kukuacha njiani lakini Mungu hawezi kukuacha.
Kwa upande wake Mchungaji
Paulo Mkumbo amesema mtu atakapo liandama agano ambalo Mungu amefanya na Baba
wa Kiroho kwa nguvu zote utamuona Mungu katika Maisha yako.




No comments:
Post a Comment