Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Luanda, Angola ambapo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla ya Uzinduzi wa Hospitali iliyopewa jina la Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, tarehe 31 Julai.
Friday, July 31, 2026
Tuesday, July 28, 2026
UMEME JUA KISHAPU AWAMU YA PILI KUIONGEZEA TANZANIA MEGAWATI 100 ZA NISHATI JADIDIFU
Hatua
hiyo imekuja baada ya kukamilika kwa awamu ya kwanza ya mradi huo wenye uwezo
wa kuzalisha jumla ya megawati 50 na kuingizwa katika Gridi ya Taifa, jambo
lililoongeza uwezo na uthabiti wa gridi hiyo na kuimarisha upatikanaji wa umeme
katika maeneo mbalimbali nchini.
Akizungumza
katika hafla hiyo Julai 27, 2026, Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi,
amesema sekta ya nishati ni mhimili wa maendeleo ya Taifa ambapo Serikali
inaendelea kufanya jitihada za kuongeza vyanzo mseto vya uzalishaji wa umeme
(Energy Mix) ili kuhakikisha Tanzania haitegemei chanzo kimoja pekee cha
uzalishaji wa umeme.
Thursday, July 23, 2026
Kambi ya matibabu ya bure iliyofanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha, imefanikiwa kutoa huduma kwa wagonjwa zaidi ya 24,871, hatua inayoonyesha mwitikio mkubwa wa wananchi katika kupata huduma za afya za kibingwa na kibobezi.
Idadi hiyo inaonesha
mafanikio makubwa ya kambi hiyo iliyowaleta pamoja madaktari bingwa na wabobezi
kutoka hospitali na taasisi mbalimbali nchini, wakitoa huduma za uchunguzi,
matibabu, vipimo na ushauri wa afya bila malipo kwa wananchi kutoka Arusha na
mikoa jirani.
Makonda amesema
kuwa,Kambi ya matibabu ya madaktari bingwa imefanikiwa kubaini wananchi 1,930
waliokuwa na shinikizo la juu la damu bila kufahamu hali zao za kiafya, hatua
iliyotajwa kuwa muhimu katika kuzuia madhara ya magonjwa yasiyoambukiza kupitia
uchunguzi wa mapema.
Akizungumza na waandishi
wa habari baada ya kukamilika kwa kambi hiyo, Mbunge wa Arusha ambaye pia ni
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Mhe. Paul Makonda, amesema jumla
ya wananchi 6,070 walifanyiwa uchunguzi wa shinikizo la damu, ambapo asilimia
65 walibainika kuwa na tatizo hilo
Amesema kati yao,
wananchi 1,930 waligundulika kwa mara ya kwanza kuwa na ugonjwa huo na
wataendelea kufuatiliwa na wataalamu wa afya ili kupata matibabu na ushauri
unaostahili.
Thursday, July 16, 2026
TANZANIA KUONGEZA KASI KATIKA HUDUMA YA UPANDIKIZAJI WA ULOTO
Serikali imeeleza dhamira
yake ya kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha huduma za afya za kibingwa katika
Afrika Mashariki na Kati huku ikitoa wito kwa Watanzania na wadau mbalimbali
kushiriki kuchangia Mfuko wa Upandikizaji wa Figo na Uloto ili kuwawezesha wagonjwa
wasiokuwa na uwezo kupata matibabu yanayookoa maisha.
Kauli hiyo ilitolewa na
Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa (Mb), wakati akiwasilisha taarifa kwa
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck
Nchemba (Mb), katika hafla ya chakula cha pamoja cha kuchangisha fedha kwa ajili
ya kugharamia huduma za upandikizaji wa figo na uloto katika Hospitali ya
Benjamin Mkapa, iliyofanyika jijini Dodoma.
Sunday, July 12, 2026
WAZIRI DEUS SANGU AWAOMBA WATUMISHI WA MUNGU KUENDELEA KUDUMISHA AMANI YA NCHI
Waziri wa nchi, ofisi ya Waziri mkuu, kazi, ajira na
mahusiano ya kazi Deusi Sangu amewaomba watumishi wa mungu waendelee
kudumisha umaadili, mshikamano na amani ya nchi.
Ameyasema hayo katika kongamano la kurejesha thamani, lililofanyika Mkoani Morogoro ambalo pia
lilikuwa na lengo la kuiombea nchi ambapo ameongeza kuwa serikali inawatambua
na kuwathamani watumishi wa mungu.
Amesema katika kuishi dhamira hiyo Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani wakati akizindua bunge la
13 aliipa wizara yake jukumu la kuratibu mahusiano baina ya serikali na makundi
ya kijamii ambapo uratibu huo unahusisha wadau wa siasa, taasisi za dini, Asasi
za Kiraia na mashirika yasiyo ya kiserikali na kwamba wanafanya kazi na wadau
hao wote kwa karibu ili kuhakikisha wanaimarisha amani, utulivu upendo,
mshikamano na maridhiano ya kitaifa.
Amesema mambo hayo ndio nguzo kuu na mahusiano na dhamira ya
maendeleo ya taifa ya mwaka 2026.
Monday, July 6, 2026
MAADHIMISHO YA SIKU YA KISWAHILI DUNIANI YAANZA RASMI BURUNDI KWA MIJADALA YA KITAALUMA
Maadhimisho ya 5 ya Siku ya Kiswahili Duniani (MASIKIDU), yanayofanyika tarehe 5 hadi 7 Julai 2026, yamefunguliwa rasmi Nchini Burundi ikiwa ni hatua muhimu ya kihistoria ya kuendeleza lugha ya Kiswahili, yakifanyika sambamba na Kongamano la 3 la Kimataifa la Kiswahili kupitia Kamisheni ya Kiswahili ya Afrika Mashariki (KAKAMA), yakiwakutanisha wadau wa Kiswahili kutoka nchi mbalimbali za Jumuiya ya Afrika Mashariki na kwingineko duniani.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa maadhimisho hayo, Waziri wa Vijana, Michezo na Utamaduni wa Jamhuri ya Burundi, Bi. Lydia Nsekela, amesisitiza kuwa Kiswahili ni nyenzo muhimu ya kuimarisha mshikamano wa kikanda, kukuza utamaduni na kuendeleza ushirikiano kati ya mataifa ya Afrika Mashariki.
Aliongeza kuwa serikali ya Burundi itaendelea kuunga mkono
juhudi za kukuza na kueneza matumizi ya Kiswahili katika sekta mbalimbali,
ikiwemo elimu, utamaduni na teknolojia.
Maadhimisho hayo yanafanyika chini ya kaulimbiu isemayo
“Kiswahili, Wingi-Lugha, na Akili Unde (Kiswahili, Multilingualism and
Artificial Intelligence)”, ambapo washiriki wanashiriki mijadala ya kitaaluma,
mawasilisho ya mada mbalimbali pamoja na maonesho ya teknolojia yanayoonesha
nafasi ya Akili Unde katika maendeleo ya lugha ya Kiswahili.
Kongamano hilo linafanyika likilenga kutoa mapendekezo
yatakayochochea matumizi ya Kiswahili katika elimu, utafiti, ubunifu wa
kidijitali na ushirikiano wa kimataifa.
kilele cha maadhimisho hayo ni Julai 7, 2026, ambapo
shughuli rasmi zitahitimishwa kama sehemu ya kuendeleza ajenda ya kukifanya
Kiswahili kuwa lugha ya kimataifa inayochochea maendeleo na umoja wa Afrika
Mashariki.
Tuesday, July 9, 2019
Simanzi: Sala ya kuaga miili ya wafanyakazi watano wa Azam Tv yafanyika
Bunge la Tanzania kuwa mwenyeji wa vikao vya Kamati ya Uongozi na ya Bajeti za Chama cha Wabunge wa Nchi za Jumuiya ya Madola–Kanda ya Afrika
Upandaji holela wa miti katika njia za umeme Kahama watajwa kusababisha nishati ya umeme kukatika.
Wednesday, July 3, 2019
HOSPITALI YA HAYDOM YANUNUA X RAY MPYA YA KISASA
WIZARA YA VIWANDA YAJIPANGA KUKUZA MASOKO NDANI NA NJE YA NCHI
NUNDU APIGA HESABU ZA UBUNGE JIMBO LA TANGA 2020
Mawaziri Bara, Zanzibar Wasaini Makubaliano ya Ushirikiano

%20Instagram.png)


















