Sunday, July 12, 2026

WAZIRI DEUS SANGU AWAOMBA WATUMISHI WA MUNGU KUENDELEA KUDUMISHA AMANI YA NCHI


Waziri wa nchi, ofisi ya Waziri mkuu, kazi, ajira na mahusiano ya kazi Deusi Sangu amewaomba watumishi wa mungu waendelee kudumisha umaadili, mshikamano na amani ya nchi.

Ameyasema hayo katika kongamano la kurejesha thamani, lililofanyika Mkoani Morogoro ambalo pia lilikuwa na lengo la kuiombea nchi ambapo ameongeza kuwa serikali inawatambua na kuwathamani watumishi wa mungu.

Amesema katika kuishi dhamira hiyo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani wakati akizindua bunge la 13 aliipa wizara yake jukumu la kuratibu mahusiano baina ya serikali na makundi ya kijamii ambapo uratibu huo unahusisha wadau wa siasa, taasisi za dini, Asasi za Kiraia na mashirika yasiyo ya kiserikali na kwamba wanafanya kazi na wadau hao wote kwa karibu ili kuhakikisha wanaimarisha amani, utulivu upendo, mshikamano na maridhiano ya kitaifa.

Amesema mambo hayo ndio nguzo kuu na mahusiano na dhamira ya maendeleo ya taifa ya mwaka 2026.


No comments:

Post a Comment