Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie mlezi wa umoja wa makanisa ya
kitume na kinabii amewataka watumishi wa mungu kuwa na umoja na upendo ili
mungu aweze kuonekana katika utumishi wao.
Ameyasema hayo jumapili ya July 12, 2026 alipokuwa
akizungumza na watumishi wa mungu, wachungaji, walimu, wainjilisti, mitume na manabii kupitia kongamano
la kurejesha thamani lililofanyika Mkoani Morogoro.
Akizungumza Nabii Mkuu amesema kuwa upendo wa kweli
unakosekana kwa watumishi ka sababu kuna mafarakano mengi ambayo yanasababisha Mungu
asionekane.
Amesema watumishi wa Mungu watakaposhikana mungu ataonekana
zaidi na watafanya kazi zaidi katika huduma zao.
%20Facebook.png)
No comments:
Post a Comment