Monday, July 13, 2026

MHE. NABII MKUU PROF. GEORDAVIE AWATAKA WATUMISHI WA MUNGU KUWA NA UMOJA NA UPENDO

Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie mlezi wa umoja wa makanisa ya kitume na kinabii amewataka watumishi wa mungu kuwa na umoja na upendo ili mungu aweze kuonekana katika utumishi wao.

Ameyasema hayo jumapili ya July 12, 2026 alipokuwa akizungumza  na watumishi wa mungu, wachungaji, walimu, wainjilisti, mitume na manabii kupitia kongamano la kurejesha thamani lililofanyika Mkoani Morogoro.

Akizungumza Nabii Mkuu amesema kuwa upendo wa kweli unakosekana kwa watumishi ka sababu kuna mafarakano mengi ambayo yanasababisha Mungu asionekane.

Amesema watumishi wa Mungu watakaposhikana mungu ataonekana zaidi na watafanya kazi zaidi katika huduma zao.


No comments:

Post a Comment