Monday, July 13, 2026

MHE. NABII MKUU PROF. GEORDAVIE ATOA KIASI CHA SHILINGI MILIONI 58

Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie leo ametoa kiasi cha shilingi milioni 58 ambapo shilingi milioni 53 ni kwa ajili ya kusapoti maono ya rais wa umoja wa makanisa ya kitume na kinabii tanzania Nabii Dkt. Joshua Mwantyala na shilingi milioni 5 kwa mchungaji hananja.

Ametoa fedha hizo alipokuwa akizungumza na mitume na manabii kupitia kongamano la kurejesha thamani lililofanyika Morogoro katika huduma ya Nabii Dkt. Joshua ambaye pia ndio muandaaji wa kongamano hilo ambapo shilingi miloni 50 ni kwa ajili ya kuendeleza maono, shilingi milioni tatu kwa ajili ya nh’ombe wa maziwa ikiwa ni zawadi ya kumbukizi yake ya siku ya kuzaliwa.

Amempongeza na kufurahishwa na maono yake na kusema kuwa kiasi hicho cha fedha amempa ili zimsaidie kuendeleza maono yake.

No comments:

Post a Comment