Sunday, July 5, 2026

MTU MWENYE IMANI HUMWABUDU MUNGU KWA UTULIVU

Imeelezwa kuwa Mtu mwenye Imani anamwabudu Mungu akiwa mtulivu, mpole na anangoja kwa sababu Mungu ana shughuli naye.

Hayo yamesemwa na Mchungaji Kiongozi Mama Anna Davie wakati akiongoza ibada ya chuo kikuu cha manabii iliyofanyika katika nyumba ya matamko ngurumo ya upako kisongo Arusha ambapo ilikuwa ni ibada ya kupokea nguvu mpya ili kuinuka upya.

Kwa upande wake Mwalimu wa neno la Mungu Isaya Benson akifundisha kuhusu somo lililokuwa na kichwa kisemacho Mapito yamebeba hatma yako amesema kuwa watu wengi wanakimbia mapito wakati ndio njia ya kuwapeleka katika hatma yao.

Naye Mngojezi wa Nabii Mkuu Claudia Silayo akifundisha ibadani hapo amesema kuwa wazazi wahawatakiwi kuwa legelege kwenye malezi ya Watoto.

Pia Mtumishi mwanafunzi Abel Likinjie amepata nafasi ya katika ibada hiyo ambapo amewataka kuwa wavumilivu ili matamko ya kinabii waliyotamkiwa yaweze kutimia maishani mwao na Baba wa kiroho ajivunie wao.




No comments:

Post a Comment