Raia nchini Iran hii leo
wanajiandaa kumzika kiongozi wao Ali Khamenei, katika mji alikozaliwa wa
Mashhad, huku mashambulizi mapya ya Marekani yakitishia kusababisha ongezeko
jipya la mvutano.
Mazishi ya kiongozi huyo mkuu wa
zamani yanafuatia ibada za maombolezo zilizodumu kwa siku kadhaa na kuhudhuriwa
na mamilioni ya waombolezaji katika miji mbalimbali nchini Iran na Iraq.
Ali Khamenei aliuawa
Februari 28, siku ya kwanza ya mashambulizi ya Marekani na Israel nchini
Iran yaliyochochea vita hivyo.
Baada ya maandamano makubwa ya
mazishi yaliyopita katika miji mitakatifu ya Najaf na Karbala nchini Iraq siku
ya Jumatano, mwili wake ulitarajiwa kufikishwa katika makazi yake ya mwisho
katika mji mtakatifu wa Mashhad.
Gavana wa Mashhad, Hassan
Hosseini alinukuliwa na televisheni ya serikali akisema kuwa
"anatarajia watu milioni 15” kuhudhuria mazishi hayo ya Khamenei.
Chanzo: DW

No comments:
Post a Comment