Sunday, July 12, 2026

MHE. NABII MKUU PROF. GEORDAVIE AMEMUWEKA WAKFU MTUMISHI WA MUNGU NABII JOSHUA MWANTYALA


Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie amemuweka Wakfu Mtumishi wa Mungu Nabii Joshua Mwantyala ambaye pia ni Rais wa umoja wa makanisa ya kitume na Kinabii Tanzania.

Zoezi hilo amelifanya kupitia siku ya mwisho ya kongamano la siku tatu la kurejesha thamani aliloliandaa mkoani Morogoro ambapo wakfu huo amemuweka kwa kummiminia mafuta yeye kama Madhabahu na kumpokea rasmi kama mtoto wake wa kiroho.

Akimuweka wakfu Nabii Mkuu ametamka ya kuwa majira mapya yanakuja huku akiachilia matamko kwa Nabii Joshua kuwa na baraka za uwepo wa Mungu, Baraka ya ulinzi, baraka ya uongozi ambapo na alimkabidhi kipaza sauti microphone kama baraka ya fimbo kwa musa na kwamba atakapoongea sauti yake itakwenda juu sana kwa nchi na itakuwa na mamlaka yenye utiisho.


No comments:

Post a Comment