Mhe. Nabii Mkuu Prof. GeorDavie amemuweka Wakfu Mtumishi wa
Mungu Nabii Joshua Mwantyala ambaye pia ni Rais wa umoja wa makanisa ya kitume
na Kinabii Tanzania.
Zoezi hilo amelifanya kupitia siku ya mwisho ya kongamano la
siku tatu la kurejesha thamani aliloliandaa mkoani Morogoro ambapo wakfu huo
amemuweka kwa kummiminia mafuta yeye kama Madhabahu na kumpokea rasmi kama
mtoto wake wa kiroho.
Akimuweka wakfu Nabii Mkuu ametamka ya kuwa majira mapya
yanakuja huku akiachilia matamko kwa Nabii Joshua kuwa na baraka za uwepo wa
Mungu, Baraka ya ulinzi, baraka ya uongozi ambapo na alimkabidhi kipaza sauti
microphone kama baraka ya fimbo kwa musa na kwamba atakapoongea sauti yake
itakwenda juu sana kwa nchi na itakuwa na mamlaka yenye utiisho.
%20Facebook.png)
No comments:
Post a Comment