Serikali imeeleza dhamira
yake ya kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha huduma za afya za kibingwa katika
Afrika Mashariki na Kati huku ikitoa wito kwa Watanzania na wadau mbalimbali
kushiriki kuchangia Mfuko wa Upandikizaji wa Figo na Uloto ili kuwawezesha wagonjwa
wasiokuwa na uwezo kupata matibabu yanayookoa maisha.
Kauli hiyo ilitolewa na
Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa (Mb), wakati akiwasilisha taarifa kwa
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck
Nchemba (Mb), katika hafla ya chakula cha pamoja cha kuchangisha fedha kwa ajili
ya kugharamia huduma za upandikizaji wa figo na uloto katika Hospitali ya
Benjamin Mkapa, iliyofanyika jijini Dodoma.

No comments:
Post a Comment