Thursday, July 23, 2026

MALI, NIGER NA BURKINA FASO ZATAFUTA KUANDAA AFCON 2032


Mali, Niger na Burkina Faso, nchi tatu zinazoongozwa na serikali za kijeshi zinawania kwa pamoja kuwa wenyeji wa Kombe la Mataifa ya Afrika AFCON mwaka 2032.

Shirikisho la Soka la Mali lilisema katika taarifa kwamba maafisa wake walikutana na rais wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Patrice Motsepe, Jumamosi mjini New York, "kwa lengo la kuandaa zabuni ya pamoja ya kuandaa Kombe la Mataifa ya Afrika 2032."



Nchi hizo tatu jirani, ambazo pia ni washirika ndani ya Muungano wa Nchi za Sahel (Alliance of Sahel States - AES), zinaongozwa na tawala za kijeshi zilizochukua madaraka kupitia mapinduzi.

Aidha, zinakabiliwa na changamoto kubwa za kiusalama kutokana na mashambulizi ya makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali, ambayo yamesababisha vifo vya maelfu ya watu.


No comments:

Post a Comment