Umoja wa Mataifa unasema
kuna dunia iko kwenye hatari ya kuzuka tena kwa mlipuko wa virusi vya ukimwi.
Shirika la umoja wa
Mataifa linaloshughulikia UKIMWI UNAIDS limesema hii ni kutokana na ufadhili
duniani kupungua pakubwa mwaka jana.
Katika ripoti yake ya
kurasa 60 iliyozinduliwa huko Brazil kuelekea kuanza kwa Kongamano la Kimataifa
la UKIMWI, Umoja wa Mataifa unasema jamii ya kimataifa imeingia katika enzi za
siasa na ubanaji wa fedha mambo yanayotishia kuharibu mazuri yote yaliyopatikana
kwa miongo kadhaa katika vita dhidi ya virusi hivyo.
Shirika la UNAIDS
linasema ufadhili ulipungua kwa asilimia 18 mwaka 2025 hadi dola bilioni 7.3
hicho kikiwa kiwango cha chini zaidi katika karibu miongo miwili.
Kabla kuingia madarakani
kwa Donald Trump, Marekani ndiyo iliyokuwa mfadhili mkuu ikichangia asilimia 75
ya ufadhili jumla wa dunia.
Chanzo: DW

No comments:
Post a Comment