Tuesday, July 28, 2026

DAGLO ASEMA WAPIGANAJI WAKE "HURU SASA" KUPAMBANA NA JESHI

Mkuu wa wanamgambo wa RSF nchini Sudan Mohamed Hamdan Daglo amewaambia wapiganaji wake kuwa "wameachiliwa huru" sasa kupambana na jeshi la nchi hiyo.

Ujumbe huu wa Daglo kwa wapiganaji wake ambao wametuhumiwa kwa mauaji ya kimbari unakuja siku moja baada ya kupoteza udhibiti wa barabara moja kuu kati ya Mji Mkuu Khartoum na mji mkubwa wa eneo la Kordofan wa El-Obeid.

Kwa wiki kadhaa sasa Umoja wa Mataifa umeonya kuwa huenda wapiganaji wa RSF wakasababisha mauaji makubwa katika eneo la Kordofan, wakati wanapotafuta kuuzingira mji wa El-Obeid kuelekea uvamizi mkubwa wanaotazamia kuufanya.

Wafanyakazi wa misaada ya kiutu wanakadiria kuwa tangu Aprili 2023, vita kati ya wapiganaji wa Daglo na mkuu wa jeshi Abdel Fattah al-Burhan vimesababisha vifo vya zaidi ya watu laki mbili na kusababisha mgogoro mkubwa zaidi duniani wa njaa na raia kuyakimbia makaazi yao.

 

Chanzo: DW


No comments:

Post a Comment