Haya yanafanyika wakati ambapo maambukizi yameripotiwa kuongezeka kwa karibu 1,000 katika kipindi cha siku kumi tu.
Takwimu rasmi
zinaonesha kuwa jumla ya visa 3,075 sasa vimethibitishwa katika
mikoa mitano baada ya mlipuko huo wa Ebola kuvuka maambukizi 2,000 mnamo Julai
15.
Mamlaka
zinasema ugunduzi wa maambukizi na juhudi za kupima zimechangia
katika kugundua maambukizi zaidi.
Mlipuko huo uliotangazwa
mnamo Mei 15, unasababishwa na aina ya kirusi cha Bundibugyo ambacho bado
hakijapata chanjo au tiba.
Kulingana na Shirika la
Afya Ulimwenguni, WHO, karibu asilimia 90 ya visa vimeripotiwa katika mkoa wa
kaskazini mashariki wa Ituri, ambao unapakana na Sudan Kusini na Uganda.
Mlipuko huo huenda
ukadumu kwa miezi kadhaa zaidi kutokana na mgomo wa wahudumu wa afya
wanaolalamikia kutolipwa mishara yao na kutatiza utoaji huduma katika baadhi ya
hospitali.

No comments:
Post a Comment