Monday, July 27, 2026

MOROCCO, ALGERIA ZAANZA VIZURI WAFCON


Timu za Taifa za soka za wanawake za Morocco na Algeria zimeanza vyema kampeni zao za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake (WAFCON) 2026 kwa kuibuka na ushindi katika michezo yao ya kwanza ya hatua ya makundi.

Wenyeji Morocco wameonyesha ubora kwa kuichapa Kenya (Harambee Starlets) mabao 4-0 katika mchezo wa Kundi A, huku Algeria ikiifunga Senegal mabao 2-0 na kuanza michuano hiyo kwa pointi tatu muhimu.

Michuano hiyo inaendelea leo ambapo Timu ya Taifa ya Wanawake ya Tanzania, Twiga Stars, itashuka dimbani kuivaa Afrika Kusini katika mchezo wa Kundi B utakaochezwa saa 2:00 usiku.

 


No comments:

Post a Comment