Tuesday, October 31, 2023

BREAKING NEWS: NABII MKUU MHE. DKT. GEORDAVIE KUWEPO REDIONI' JUMATANO HII NOV 01, 2023

Nabii Mkuu Mhe. Dkt. GeorDavie jumatano wiki hii anatarajia kuwepo radioni katika kipindi maalumu kitakachoanza kuanzia  saa mbili na nusu usiku.

Taarifa kutoka ikulu ya Nabii Mkuu imesema kuwa Nabi Mkuu Mhe. Dkt. GeorDavie amesema, Mungu amemuongoza kuja radioni ili kuwaepusha watu wake na pigo ambalo adui amekusudia kukudhuru nalo.

Pia Nabii Mkuu ameongeza kuwa kati ya mambo ambayo Mungu amempa dhamana ya kuja kukufutia ni Pamoja na ajali, kifo cha ghafla na janga la uharibifu huku akisema kuwa Mungu amewakumbuka watu wake.

Aidha kila mmoja ametakiwa kujiandaa kwa sadaka maalumu ya shilingi elfu 10,000 kwa ajili ya kupokea kibali cha kufutiwa majanga yote kwa mpigo kupitia neno la mtu wa Mungu Nabii Mkuu Mhe. Dkt. GeorDavie usiku huo.



Monday, October 30, 2023

NENO LA KINABII WIKI HII KUTOKA KWA NABII MKUU MHE. DKT. GEORDAVIE

NABII MKUU DKT. GEORDAVIE: NAKUTAMKIA KUPOKEA WIKI YA HEKIMA NA UFAHAMU!!

Aidha utajiungamanisha na neno hilo la wiki hii kwa kutuma sadaka yako jumanne na alhamisi kuanzia shilingi 5,000/= na kuendelea na mara baada ya kutuma sadaka yako kupitia namba hizi 0769 00 00 34 / 0788 00 00 35 utaandika maneno yafuatayo;

JUMANNE: HEKIMA

ALHAMISI: UFAHAMU





NABII MKUU DKT. GEORDAVIE "HEKIMA NA UFAHAMU NI CHANZO CHA KUMJUA MTAKATIFU WA MUNGU"

Nabii Mkuu Mheshimiwa Dkt.GeorDavie amesema kuwa mtu anaweza kuwa na hekima lakini akakosa ufahamu.

Nabii Mkuu ameyasema hayo alipokuwa akifundisha katika ibada ya chuo kikuu cha manabii iliyofanyika katika nyumba ya matamko ngurumo ya upako kisongo Arusha ambapo ilikuwa ni iabada ya kupokea hekima na ufahamu.

Akifundisha kuhusu somo lililokuwa na kichwa kisemacho kumjua mtakatifu ni ufahamu Nabii Mkuu amesema kuwa kumjua aliyechaguliwa na Mungu, kumjua mteule aliyebeba kusudi la wakati au majira ni ufahamu.

Pia Nabii Mkuu ameitangaza wiki hii kuwa ni wiki ya kupokea hekima na ufahamu.

Na Beatrice Maina.



Saturday, October 28, 2023

NABII MKUU MHE. DKT. GEORDAVIE JUMAPILI YA KESHO ATAONGOZA IBADA YA CHUO KIKUU CHA MANABII

Nabii Mkuu Mhe. Dkt. GeorDavie jumapili hii anatarajia kuongoza ibada ya chuo kikuu Cha manabii ambapo itakuwa ni ibada ya kupokea hekima na ufahamu.

Akizungumza kuhusu ibada hiyo Nabii Mkuu amesema kuwa pia itakuwa ni siku ya kuwasilisha sadaka za International Partner kwa ajili ya ununuzi wa viti.

Amesema kuwa katika ibada hiyo ya kupokea hekima na ufahamu neno la linalosimamia ni kutoka katika kitabu cha Mithali 9:10 unaosema "Kumcha Bwana ni mwanzo wa hekima na kumjua mtakatifu ni ufahamu"

Aidha Nabii Mkuu amemtaka kila mtu kuwahi ibadani,kuja na sadaka ya international partner pamoja na sadaka maalum ya kupokea hekima na ufahamu.

Na Beatrice Maina, N.Y.U ARUSHA.


Monday, October 23, 2023

MKUU WA WILAYA YA ARUMERU AMPONGEZA NABII MKUU KWA KUSAIDIA JAMII

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru mkoani Arusha Emmanuela Mtatifikolo Kaganda amempongeza Nabii Mkuu Mhe. Dkt. GeorDavie kwa kazi anayoifanya katika kuisadia jamii kiroho na kijamii.

Ametoa pongezi hizo alipokuwa akizungumza katika ibada ya chuo kikuu cha manabii iliyofanyika katika nyumba ya matamko ngurumo ya upako ambapo ilikuwa ni ibada ya Adhimisho la zawadi ya Nabii Mkuu.

Akizungumza katika ibada hiyo amemuomba Nabii Mkuu kuendelea kuwasaidia watu kiroho na hata kijamii huku akisema kuwa ameguswa na jambo ambalo Nabii Mkuu amelifanya la kuwasapoti wanawake waliokuwa wanajiuza.

Na Beatrice Maina, N.Y.U ARUSHA.

NABII MKUU ATOA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 27 KUSAIDIA WATU MBALIMBALI WAKIWEMO WANAWAKE WALIOKUWA WANAJIUZA.

Nabii Mkuu Mhe. Dkt.GeorDavie Balozi wa Amani jumapili ya jana ametoa fedha zaidi ya shilingi milioni 27 kusaidia watu mbalimbali wakiwemo wanawake ambao walikuwa wakijiuza ili kujiingizia kipato cha kujikimu kimaisha.

Nabii Mkuu ametoa fedha hizo katika ibada ya chuo kikuu cha manabii iliyofanyika katika nyumba ya amtamko ngurumo ya upako kisongo mkoani Arusha na ilikuwa ni ibada ya adhimisho la zawadi ya Nabii Mkuu.

Akizungumza wakati anatoa msaada huo kwa watu hao Nabii Mkuu amesema amewataka watu kutambua kwamba huduma ya kinabii ni huduma yenye mamlaka maana ukitamka neno linakuwa kwa sababu wanawake hao walisikia agizo na kulifuata kwa kuamua kubadilika na kuongeza kuwa kazi waliyokuwa wakiifanya ilikuwa inahitaji ufungulivu wa kiroho kabla ya kuwasapoti.

Pia Nabii mkuu ametangaza kuwa hii ni wiki ya kuepushwa na ajali na kupokea ulinzi mkamilifu.

Aidha Ibada hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali akiwemo Mkuu wa wilaya ya Arumeru Emmanuela Mtatifikolo Kaganda Pamoja na Mbunge wa Jimbo la Arusha mjini Mhe. Mrisho Gambo na watumishi wa Mungu kutoka makanisa mengine ikiwa ni Pamoja na Baraza la Mitume na Manabii Tanzania.

Na Beatrice Maina - N.Y.U ARUSHA.











MRISHO GAMBO "KAZI ANAZOFANYA NABII MKUU ZINAIONYESHA KUWA NI DINI YA KWELI"

Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Mhe. Mrisho Gambo amesema kwamba kazi anazozifanya Nabii Mkuu Mhe. Dkt. GeorDavie katika kuwasaidia watu kiuchumi ni ishara tosha kuwa hiyo ndio dini ya kweli.

Mhe. Gambo ameyasema hayo alipokuwa akitoa zawadi kwa Nabii Mkuu Mkuu Mhe. Dkt. GeorDavie ambapo ilikuwa ni sikukuu ya adhimisho la zawadi ya Nabii Mkuu.

Aidha amesema kuwa amekuwa akijifunza mambo mengi wakati wote anaposhiriki ibada za huduma ya ngurumo ya upako kwani ipo tofauti na huduma nyingine.

Na Beatrice Maina, N.Y.U ARUSHA






PICHA ZA SHAMRASHAMRA ZA WATU NA MATUKIO MBALIMBALI WAKATI WA KUMPOKEA NABII MKUU MHE. DKT. GEORDAVIE KATIKA NYUMBA YA MATAMKO.















NABII MKUU MHE. DKT. GEORDAVIE "HII NI WIKI YA KUEPUSHWA NA AJALI NA KUPOKEA ULINZI"

Nabii Mkuu Mhe. Dkt. GeorDavie ametangaza neno la wiki hii kuwa hii ni wiki ya kuepushwa na Ajali na kupokea Ulinzi mkamilifu.

Ametangaza neno hilo jumapili ya Oktoba 22, 2023 katika ibada ya chuo kikuu cha manabii iliyofanyika katika nyumba ya matamko kisongo Arusha ambapo ilikuwa ni ibada ya kupokea Thawabu ya Nabii Mkuu na ilikuwa ni sikukuu ya adhimisho la zawadi ya Nabii Mkuu.

Nabii Mkuu Mhe. Dkt. GeorDavie amesema kuwa neno la kinabii linapokuja limekusudiwa kuwakinga wana wa Mungu na mabaya yote ya adui.