Monday, November 27, 2023

NABII MKUU DKT.GEORDAVIE AKABIDHI GARI NA SHILINGI MIL 11.4 KWA MUANDAAJI YA MISS TANZANITE MANYARA.

Nabii Mkuu Mhe.Dkt.GeorDavie ametoa gari jipya aina ya Honda station wagon yenye namba za usajili T169 EEP kwa muandaaji wa mashindano ya Miss Tanzanite Manyara Bi. Aminata pamoja na shilingi milioni 11.4.

Nabii Mkuu amekabidhi gari hilo jana katika ibada ya chuo kikuu cha manabii baada ya Bi.Aminata kuelezea changamoto anazokutana nazo katika kazi yake ambapo Nabii Mkuu aliguswa na kuamua kumsapoti gari hilo na fedha hizo ili aweze kuendesha ofisi yake ikiwa ni pamoja na kuwalipa washindi na washiriki wa mashindano hayo.

Kwa upande wake Bi. Aminata amemshukuru Nabii Mkuu kwa moyo wa upendo wa kusaidia watu huku akimuombea Nabii Mkuu Aishi miaka mingi ili awasaidie watu wengine wanaokutana na changamoto mbalimbali maishani mwao.

Na Beatrice Maina, N.Y.U ARUSHA.



NABII MKUU MHE. DKT. GEORDAVIE AISHUKURU SERIKALI KWA KUMPA BARABARA.

Nabii Mkuu Mhe Dkt.GeorDavie ameishukuru serikali kwa kutambua mchango wake katika jamii na kumpa heshima ya kuandika jina lake na huduma yake kwenye barabara mbili hapa jijini Arusha ambapo kuna barabara ya GeorDavie Road na Ngurumo ya Upako Road.

Akizungumza Nabii Mkuu amesema kuwa ataendelea kusaidia wananchi na kwamba furaha yake ni kusaidia watu huku akisema amefanya mambo mengi mema kwa watu na hakutarajia siku moja atapewa heshima kubwa kama hii ya kupewa Barabara ambazo zitakuwa ni historia hata kwa vizazi vijavyo.

Aidha kwa hapa nchini hatujaona barabara nyingine yenye jina la Mtumishi wa Mungu na Nabii Mkuu Mhe Dkt.GeorDavie amekuwa Mtumishi wa Mungu wa kwanza kupewa barabara zenye jina na huduma yake ambapo GeorDavie Road ipo barabara ya kuelekea Ikulu ya Nabii Mkuu.

Kuna Barabara nyingine kama Nyerere, Ally Hassan Mwinyi, Kawawa Road, Sokoine Road na Sasa tuna Barabara ya GeorDavie na Ngurumo ya Upako Road ambapo zinapatikana Barabara ya Dodoma Arusha.



Friday, November 17, 2023

NABII MKUU DKT. GEORDAVIE KUPANDISHA VIWANGO VYA WATU KIMAISHA.

Nabii Mkuu Mheshimiwa Dkt.GeorDavie Balozi wa Amani anatarajia kupandisha viwango vya watu kimaisha ili waondokane na umasikini.


Nabii Mkuu atawapandisha watu viwango kupitia ibada ya chuo kikuu cha manabii itakayofanyika katika nyumba ya matamko Kisongo Arusha ambapo itakuwa ni ibada ya kupanda viwango kimaisha.

Aidha amewata watu kuja na sadaka maalum ya kujiambatanisha na matamko ya kinabii ya kupanda viwango.

Na Beatrice Maina, N.Y.U RADIO.



NABII MKUU KUPOKEA ZAWADI ZA PONGEZI JUMAPILI HII NOV 19, 2023

Nabii Mkuu Mheshimiwa Dkt.GeorDavie anatarajia kupokea zawadi za pongezi kwa kuanzisha Ngurumo ya Upako  Radio ( N.Y.U. FM 99.3 MHz) kutoka kwa watoto wake wa kiroho.

Nabii Mkuu atapokea pongezi hizo ambazo ni kwa mfumo ya fedha katika ibada ya chuo kikuu cha manabii itakayofanyika jumapili katika nyumba ya matamko Ngurumo ya Upako Kisongo jijini Arusha ambapo itakuwa ni ibada ya kupanda viwango kimaisha.

Akizungumza kuhusu Radio Kadinali wa kwanza wa huduma ya Ngurumo ya Upako Mtume Gaudensia Luila amesema kuwa siku tutamshukuru Mungu kwa ajili ya radio ambayo imefanyika Baraka na msaada mkubwa kwa watu wengi ambapo kupitia radio watu wamepomea uponyaji, mitaji na Baraka mbalimbali za kiroho na kimwili.

Amesema tunapomshukuru Mungu kwa ajili ya radio pia ni wajibu wetu kumpongeza Nabii Mkuu ambaye ndiye muanzilishi na msimamizi wa Radio.

Aidha katika ibada hiyo kila mtu atapata nafasi ya kusapoti Radio pamoja na kumpongeza Nabii Mkuu kwa mambo mengi anayoyafanya kwa watu bila mbalimbali kubagua na huduma kwa ujumla.

Na Beatrice Maina, N.Y.U ARUSHA. 



Tuesday, November 14, 2023

DKT.GEORDAVIE" FEDHA INAPATIKANA KWA KUFANYA KAZI KWA BIDII."

Nabii Mkuu Mhe.Dkt.GeorDavie amewataka watu kutambua kuwa fedha inapatikana kwa kufanya kazi kwa bidii na kuwa na akili yenye ufahamu.


Nabii Mkuu ameyasema hayo wakati akizungumza na kufundisha watu hekima mbalimbali zinazoweza kuwasaidia katika maisha yao.

Akizungumza Nabii Mkuu amesema kuwa hakuna uchawi kwenye utajiri kitu kinachotakiwa ili mtu aweze kufanikiwa ni kufanya kazi kwa bidii.

Na Beatrice Maina, N.Y.U.ARUSHA.



Monday, November 13, 2023

NABII MKUU" ACHA KULIPIZA KISASI SAMEHE UISHI KWA AMANI NA FURAHA."

Nabii Mkuu Mhe.Dkt.GeorDavie Balozi wa Amani amewataka watu kuacha tabia ya kulipiza kisasi kwa watu waliowakosea na badala yake wawe watu wa kusamehe ili waweze kupokea Baraka zao kutoka kwa Mungu.


Nabii Mkuu ameyasema hayo alipokuwa akifundisha somo lililokuwa na kichwa kisemacho "Kumjua Mtakatifu ni Ufahamu"i katika ibada ya chuo kikuu cha manabii ambapo ilikuwa ni ibada ya kuongozeka kiuchumi.

Akizungumza Nabii Mkuu amesema kuwa makosa ni mengi hivyo kinachotakiwa ni kuishi katika ufahamu huku akieleza jinsi ambavyo yeye amedumu kuwasamehe watu wengi ambao walimkosea maishani.

Na Beatrice Maina, N Y.U ARUSHA.


Saturday, November 11, 2023

NABII MKUU MHE. DKT. GEORDAVIE ANATARAJIA KUONGOZA IBADA YA JUMAPILI YA KESHO NOV12, 2023

Nabii Mkuu Mhe. Dkt.GeorDavie kesho jumapili anatarajia kuwaongeza maelfu ya watu kiuchumi kupitia ibada ya chuo kikuu cha manabii itakayofanyika katika nyumba ya amtamko ngurumo ya upako kisongo Arusha.

Akizungumza kuhusu ibada hiyo Nabii Mkuu amesema kuwa itakuwa ni ibada ya kuongezeka kiuchumi ambapo pia amemtaka kila mtu kuja na sadaka yake ya silver partner ambayo itawafungulia mlango wa kuongezeka kiuchumi.

Aidha katika huduma ya Ngurumo ya Upako huwa watu wanatoa sadaka zao kila mwezi kwa ajili ya kusapoti maono ya mtu wa Mungu Nabii Mkuu Mhe. Dkt. GeorDavie.

Na Beatrice Maina, N.Y.U ARUSHA.


Sunday, November 5, 2023

NENO LA WIKI HII KINABII KWA AJILI YAKO KUTOKA KWA NABII MKUU MHE. DKT. GEORDAVIE

Nabii Mkuu Mhe. Dkt. GeorDavie ametanga neno la wiki hii kuwa hii ni wiki ya kukumbukwa kwa maombi yako.

Ametanga neno hilo jumapili ya tarehe 05.11.2023 katika ibada iliyofanyika nyumba ya matamko kisongo Arusha ambapo ilikuwa ni ibada ya kukumbukwa kwa maombi yako.

Nabii Mkuu amesema kuwa kila jambo ulilowahi kuomba kwa wakati wowote ule wiki hii linakumbukwa huku akiongeza kuwa wiki hii imekuwa ni kumbukumbu mbele ya Mungu kwa ajili ya maombi yako ili kila jambo liweze kujibiwa.

Na Deogratius Festo.



Thursday, November 2, 2023

NABII MKUU MHE. DKT. GEORDAVIE AWAFUTIA MAELFU YA WATU MAPIGO MATATU ADUI ALIYOKUSUDIA KUWADHURU

Nabii Mkuu Mhe. Dkt. GeorDavie Balozi wa amani amewafutia maelfu ya watu mapigo matatu ambayo adui alikusudia kuwadhuru watu wa Mungu. 

Nabii Mkuu amefuta mapigo hayo ambayo ni ajali, kifo cha ghafla na janga la uharibifu kupitia kipindi maalum kilichorushwa live kupitia N.Y.U Radio jumatano usiku ambapo Mungu alimpa dhamana ya kufutia watu mapigo hayo.

Akitamka matamko ya kufuta mapigo hayo Nabii Mkuu amesema kuwa Mungu amekukusudia kupokea uzima na uhai na watu wamepokea amani, kuwa salama na kuwa vyema.

Akizungumza katika kipindi hicho Nabii Mkuu amesema kuwa jambo kama hilo haliwezekani kwa maombi bali linamuhitaji Nabii Mkuu ili kutoa maelekezo.

Aidha watu walipata nafasi ya kutuma sadaka zao maalum za kuepuka mapigo yote matatu ya adui sawasawa na maagizo ya Nabii Mkuu.

Na Beatrice Maina, N.Y.U ARUSHA.



Tuesday, October 31, 2023

BREAKING NEWS: NABII MKUU MHE. DKT. GEORDAVIE KUWEPO REDIONI' JUMATANO HII NOV 01, 2023

Nabii Mkuu Mhe. Dkt. GeorDavie jumatano wiki hii anatarajia kuwepo radioni katika kipindi maalumu kitakachoanza kuanzia  saa mbili na nusu usiku.

Taarifa kutoka ikulu ya Nabii Mkuu imesema kuwa Nabi Mkuu Mhe. Dkt. GeorDavie amesema, Mungu amemuongoza kuja radioni ili kuwaepusha watu wake na pigo ambalo adui amekusudia kukudhuru nalo.

Pia Nabii Mkuu ameongeza kuwa kati ya mambo ambayo Mungu amempa dhamana ya kuja kukufutia ni Pamoja na ajali, kifo cha ghafla na janga la uharibifu huku akisema kuwa Mungu amewakumbuka watu wake.

Aidha kila mmoja ametakiwa kujiandaa kwa sadaka maalumu ya shilingi elfu 10,000 kwa ajili ya kupokea kibali cha kufutiwa majanga yote kwa mpigo kupitia neno la mtu wa Mungu Nabii Mkuu Mhe. Dkt. GeorDavie usiku huo.



Monday, October 30, 2023

NENO LA KINABII WIKI HII KUTOKA KWA NABII MKUU MHE. DKT. GEORDAVIE

NABII MKUU DKT. GEORDAVIE: NAKUTAMKIA KUPOKEA WIKI YA HEKIMA NA UFAHAMU!!

Aidha utajiungamanisha na neno hilo la wiki hii kwa kutuma sadaka yako jumanne na alhamisi kuanzia shilingi 5,000/= na kuendelea na mara baada ya kutuma sadaka yako kupitia namba hizi 0769 00 00 34 / 0788 00 00 35 utaandika maneno yafuatayo;

JUMANNE: HEKIMA

ALHAMISI: UFAHAMU





NABII MKUU DKT. GEORDAVIE "HEKIMA NA UFAHAMU NI CHANZO CHA KUMJUA MTAKATIFU WA MUNGU"

Nabii Mkuu Mheshimiwa Dkt.GeorDavie amesema kuwa mtu anaweza kuwa na hekima lakini akakosa ufahamu.

Nabii Mkuu ameyasema hayo alipokuwa akifundisha katika ibada ya chuo kikuu cha manabii iliyofanyika katika nyumba ya matamko ngurumo ya upako kisongo Arusha ambapo ilikuwa ni iabada ya kupokea hekima na ufahamu.

Akifundisha kuhusu somo lililokuwa na kichwa kisemacho kumjua mtakatifu ni ufahamu Nabii Mkuu amesema kuwa kumjua aliyechaguliwa na Mungu, kumjua mteule aliyebeba kusudi la wakati au majira ni ufahamu.

Pia Nabii Mkuu ameitangaza wiki hii kuwa ni wiki ya kupokea hekima na ufahamu.

Na Beatrice Maina.