Serikali
imesema Kikatiba hakuna mgongano wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na Katiba ya Zanzibar unaosababisha ongezeko kubwa la kero za
Muungano na mgongano wa kimamlaka baina ya Serikali ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Hayo
yamesemwa na Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi
bungeni jana mjini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Wingi
Mhe. Juma Kombo lililohusu mgongano wa Katiba hizo.
Prof
Kabudi alisema kuwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeweka
utaratibu mahususi wa kushughulikia tafsiri