TAARIFA KWA UMMA
UFAFANUZI WA HOJA ZA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI (NEC) DHIDI YA TAMKO LA ASASI ZA KIRAIA
Kituo
cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimepokea barua Kumb. Na.
BA.71/75/01/124 ya tarehe 22 February 2018 kutoka kwa Mkurugenzi wa
Uchaguzi Ndugu Kailima Ramadhani na kupitia kwa umakini mkubwa hoja za
Tume Ya Uchaguzi dhidi ya tamko lililotolewa na umoja wa Asasi Za
Kiraia, chini ya Jukwaa la Wakurugenzi wa AZAKI, Februari 21, 2018
kuzungumzia hali ya usalama wa raia, haki za binadamu na utawala wa
sheria hapa nchini.