Tuesday, January 15, 2019

NABII MKUU MHE. DR. GEORDAVIE ATANGAZA WIKI YA USHINDI KATIKA MAENEO YOTE MAISHANI.




 KUTOKA IKULU YA NABII MKUU TANZANIA..

    Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie ametangaza kuwa hii ni wiki ya kuwa washindi katika maeneo yote maishani.
    Ameyasema hayo wakati akiongoza ibada ya chuo kikuu cha manabii iliyofanyika katika hema la kukutania, Ngurumo Ya Upako, Kisongo, Arusha.
   Katika ibada hiyo ambayo pia ilikuwa ni ibada ya Silver Partners, Nabii Mkuu alitamka baraka mbalimbali za Kinabii kwa wana-Partners wote ikiwemo baraka ya kushika pesa na kuheshimika.
   Aidha Nabii Mkuu alifundisha umuhimu wa kuwa mwana-Partners na faida zake huku akiwasisitizia watu wote kusapoti kazi ya Mungu kwa nguvu kwa kuna baraka ya kipekee wataipata kwa kufanya hivyo na kuwakumbusha kuwa ili kazi ya Mungu iwe nzuri na ithaminiwe ni lazima igharamikiwe ambapo alitoa nukuu isemayo "Cha gharama kina thamani kama hakina gharama hakina thamani" akimaanisha kuwa kitu chochote chenye thamani lazima kiwe cha gharama hakiwezi kuwa bure ikiwemo Nguvu Ya Mungu.
   Wakati huohuo Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie ametangaza kuwepo katika kipindi cha Maswali Na Majibu  kitakachoruka LIVE kwa njia ya Radio,  99.3  N.Y.U FM pamoja na GEORDAVIE TV siku ya jumatano ambapo kwa siku hiyo yeye ndiye atakayeuliza maswali kwa wasikilizaji na watazamaji na kisha kutoa zawadi ya pesa taslimu kwa wale watakaopatia kwa kujibu maswali hayo vizuri. 


          NB: Usisahau ku-download application ya GeorDavie Ministries itakayo kuwezesha kutazama  GeorDavie Tv pamoja na kusikiliza 99.3 N.Y.U Radio.

Tuesday, January 8, 2019

JE UNAFAHAMU KUWA MHE. DR. GEORDAVIE KATIKA MWAKA 2018 PEKEE AMETUMIA ZAIDI YA SH. MILIONI 143 KATIKA KUSAIDIA JAMII???


   Amekuwa akitambulika kama Mtumishi wa Mungu mtoaji zaidi Nabii wa Equator, Nabii Mkuu wa karne ya 21, si mwingine ni Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie kutoka Arusha, Tanzania.
  Na siku ya leo tunakuletea kwa uchache baadhi ya matukio ya utoaji aliyoweza kuyafanya kwa mwaka wa 2018 yaliyopelekea Nabii Mkuu ambaye amekuwa msaada na kipenzi cha wengi kutajwa kama Mtumishi Wa Mungu mtoaji zaidi.
  Katika ku-support Watumishi Wa Mungu kutoka katika makanisa mengine tofauti na Ngurumo Ya Upako yaliyo ndani na nje ya Tanzania, Nabii Mkuu ametumia zaidi ya Sh. Milioni 30 katika kuhakikisha anatoa misaada katika huduma hizo ambapo kwa asilimia kubwa zilikuwa haziridhishi kiuchumi (hazijamudu kujitegemea kiuchumi), Nabii Mkuu aliweza kuwasaidia ili kuhakikisha watumishi wanaweza kukidhi mahitaji yao lakini pia ikiwa ni pamoja na kuwasaidia kujenga makanisa yao ili yawe katika hali ya kuridhisha.
  Katika upande mwingine wa kijamii, Nabii Mkuu amekuwa na kawaida ya kupeleka misaada sehemu mbali ikiwa ni pamoja na katika vituo vya watoto yatima ambapo kwa mwaka 2018 Nabii Mkuu amepeleka katika vituo vitatu tofauti hapa Tanzania.
   Mbali na hayo pia Nabii Mkuu ametoa misaada mingine ikiwemo kuwalipia ada wanafunzi wa ngazi mbalimbali mpaka chuo kikuu waliokwama kutokana na kukosekana kwa kipato ili kuwawezesha kuendelea na masomo yao.
  Aidha katika kusaidia watu pia Nabii Mkuu ametumia zaidi ya Milioni 20 katika kusaidia watu mbalimbali wenye mahitaji, ikiwemo wenye uhitaji wa mitaji lakini pia wenye biashara ndogo ndogo katika kuhakikisha wanaweza kuwa na kipato cha kujikimu kimaisha.
  Lakini pia katika upande mwingine Nabii Mkuu amekuwa akiwa-support watu wenye vipaji kwa namna mbalimbali ambapo baadhi ya waliopata neema hiyo ni pamoja na vijana wawili walionunuliwa ngoma na mwingine spika ,kila mmoja kwa wakati wake pamoja na waimbaji wa nyimbo za injili kutoka sehemu mbalimbali.
  Hakuishia hapo katika kusaidia tu, Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie amekuwa akitoa zawadi mbalimbali kwa watu ambapo kwa mwaka wa 2018 ametoa zawadi ya magari nane (8) kwa watu tofauti tofauti wa ndani na nje ya nchi kwa mwaka huo yenye thamani ya jumla milioni 88.
  Aidha katika msimu wa sikukuu mpaka sasa Nabii Mkuu ametoa zawadi kwa njia ya pesa taslimu za zaidi ya sh. Milioni 5 kwa watu mbalimbali ambao walijishindia kwa njia ya kupiga simu kwenye vipindi vilivyokuwa vikiruka kupitia 99.3 N.Y.U FM Radio pamoja na GeorDavie Tv (zoezi hilo linaendelea mpaka sasa) na wengine wakijishindia kupitia mitandao ya kijamii.
  Akizungumzia utoaji huo Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie amesema haya "hiyo ni njia ya Ufalme Wa Mungu kuwabariki watu wake kwakuwa nao wamekuwa wakitoa kwa Ufalme Wa Mungu hivyo sasa ni wakati wao kubarikiwa pia" mwisho wa kunukuu.
         NB: Usisahau kudownload application ya GeorDavie Ministries itakayo kuwezesha kutazama GeorDavie Tv pamoja na kusikiliza 99.3 N.Y.U Radio.

Tuesday, December 25, 2018

NABII MKUU MHE. DR. GEORDAVIE AMEWATAKA WATU KUTOKUANGALIA MAZINGIRA YANASEMA NINI BALI WAANGALIE KUSUDI LA MUNGU KATIKA MAISHA YAO.





   Jumapili ya tarehe 23.12.018 Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie aliongoza ibada ya jiji katika Chuo Kikuu Cha Manabii Ngurumo Ya Upako Arusha, ambapo ilikuwa ni ibada ya Christmas ya kudhihirisha kusudi la Mungu maishani.

   Akifundisha somo lenye kichwa kisemacho "Usiangalie mazingira bali kusudi la Mungu" Nabii Mkuu amesema kuwa kuna wakati mazingira yanaweza kueleza kitu kingine lakini pia Mungu akawa na kusudi maishani mwako ambapo alimtolea mfano Yesu Kristo na kusema kuwa kuzaliwa kwake katika hori la ng'ombe haikuwa sababu ya kusudi alilokuwa nalo kupotea.
   Aidha Nabii Mkuu amesema kuwa katika maisha kuna vitu vitatu.. Mazingira, Wakati na Kusudi na kuongeza kwamba "Mazingira hukabiliwa na wakati" ikiwa siyo wakati wa Mungu huwezi kulazimisha na pia ikiwa ni wakati wa Mungu huwezi kuuzuia.

   Mbali na hayo Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeoDavie alifungua watu mbalimbali waliofika wakiwa na vifungo vya nguvu za giza, na pia kutamka maneno ya baraka kwa watu wote ili wazidi kuinuka, kubarikiwa, kung'aa na kufanikiwa.

   Pia Nabii Mkuu ametangaza kuwepo tena katika katika hema la kukutania Ngurumo Ya Upako siku ya jumatano ya tarehe 26.12.018 ambapo itakuwa ni ibada ya hitimisho la Siku kuu ya kukusanya (SKYK) ambapo watu wote wametakiwa kufika wakiwa wamefunga pamoja na bajeti zao za mwaka 2019.


    NB: Usisahau ku-download application ya GeorDavie Ministries itakayo kuwezesha kutazama  GeorDavie Tv pamoja na kusikiliza 99.3 N.Y.U Radio.

Monday, December 10, 2018

NABII MKUU MHE. DR. GEORDAVIE AONGOZA IBADA YA MWISHO KWA SILVER PARTNERS.



KUTOKA KATIKA IBADA YA JIJI, CHUO KIKUU CHA MANABII, ILIYOFANYIKA KATIKA HEMA LA KUKUTANIA NGURUMO YA UPAKO, KISONGO, ARUSHA..
Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie aliongoza ibada ya chuo kikuu cha manabii siku ya jana ambapo ilikuwa ni ibada ya Silver Partners ya mwisho kwa mwaka huu wa 2018, ambapo aliweza kutamka baraka mbalimbali kwa wana-Silver Partners wote.

Saturday, October 13, 2018

Waziri Mkuu Aitisha Nyaraka Za Uendeshaji Soko La Kibaigwa.....Ni baada ya wafanyabiashara na mbunge kulalamikia uendeshwaji wake

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wasimamizi na waendeshaji wa Soko la Kimataifa la Mazao Mchanganyiko la Kibaigwa pamoja viongozi wa Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (MVIWATA) kufika ofisini kwake Oktoba 22, 2018 wakiwa na nyaraka zote zinazoonesha uendeshaji wa soko hilo.

Taifa Stars Yapigwa 3-0 Na Cape Verde

Kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars'  jana usiku kimekubali kichapo cha mabao 3-0 kutoka kwa Cape Verde  na sasa kitalazimika kuanza kupiga mahesabu ya mataifa yaliyopo kundi L ili kuona kama kinaweza kufuzu fainali za AFCON 2019 nchini Cameroon.

MAGAZETI YA LEO OCTOBER 13.

JOEL LWAGA Feat CHRIS SHALOM UMEJUA KUNIFURAHISHA OFFICIAL VIDEO