Tuesday, June 11, 2019

Kenya na Uganda wametangaza vikosi vyao kamili vya AFCON 2019

Timu ya taifa ya Kenya na Uganda kwa pamoja wote leo wamefanikiwa kutangaza vikosi vyao vya wachezaji 23 vitakavyoshiriki fainali za mataifa ya Afrika 2019 nchini Misri, Kenya wametangaza kikosi hicho ikiwa ni siku moja
imepita toka wamuengue Brian Mandela kwa kupata majeraha ya
goti.
Kenya wapo Kundi C na timu za Tanzania, Algeria na Senegal ambapo wao walikuwa nchini Ufaransa kuweka kambi ya maandalizi wakati ambo wenzao Algeria wakiwa Doha Qatar, Senegal wakiwa Hispania wakati Tanzania wakiwa nchini Misri.


by Rich Voice.

No comments:

Post a Comment