Wednesday, July 30, 2025

NABII MKUU AWATAKA WATU KUTAMBUA NGUVU NA LUGHA YA NABII MKUU

Nabii Mkuu Mhe.Dkt.GeorDavie amewataka watu kuitambua Nguvu ya Nabii Mkuu na Lugha anayoitumia maana kuna tofauti kati ya Nabii na Nabii Mkuu.

‎Amesema unapomuona Nabii Mkuu umemuona Mtu mwenye Mamlaka katika Serikali Tukufu ya Ufalme wa Mungu na kwamba Neno lake analotamka ndilo linalokuwa.

‎Ameongeza kuwa Nabii Mkuu anapoingia ni Serikali Tukufu ya Ufalme wa Mungu imeingia na kwamba watu wakitambua jambo hilo lazima watafanikiwa kiroho na kimwili kwa kuyashika matamko ya kinabii.

‎Na Beatrice Maina@NYU ARUSHA.

NABII MKUU AWASHUKURU WALIOMPONGEZA KWA KUTUNUKIWA TUZO YA HESHIMA YA UDAKTARI

Nabii Mkuu Mhe.Dkt.GeorDavie amewashukuru watu wote walio mpongeza kwa kupata tuzo ya heshima ya Udaktari aliyokabidhiwa na umoja wa madaktari na maprofessa  julai  5 jijini Dodoma.

Nabii Mkuu ametoa shukrani hizo jana katika ibada ya chuo kikuu cha manabii iliyofanyika ngurumo ya upako kisongo Arusha ambapo ilikuwa ni ibada ya shukrani kwa kuvuka nusu mwaka na kuanza nusu nyingine kwa ushindi.


Akizungumza Nabii Mkuu amesema kuwa watu wote wamekuwa wamiliki wakubwa wa heshima hiyo na amekuja kuwakabidhi heshima hiyo kwa sababu walionyesha mahitaji yao ya kiroho na kimwili na yeye akayaangalia kwa kuwafungua na kuwasapoti.

Thursday, July 24, 2025

HII NDIO CV YA KOCHA MPYA WA KLABU YA YANGA.

 HII NDIO CV YA KOCHA MPYA WA KLABU YA YANGA.

Anaitwa Romain Folz (35) Kocha mpya wa Yanga,ambae alizaliwa Bordeaux,Ufaransa πŸ‡«πŸ‡·

Huyu kocha amefanya kazi sehemu zifuatazoπŸ‘‡

2025 Alikuwa Mkurugenzi wa michezo wa Olympique Akbou ya Algeria πŸ‡©πŸ‡Ώ

2024 Alikuwa kocha msaidizi wa Mamelodi Sundown ya South Africa πŸ‡ΏπŸ‡¦

2023 Alikuwa kocha mkuu wa Horoya ya Guinea πŸ‡¬πŸ‡³

2022 Alikuwa kocha mkuu wa Amazulu ya South Africa πŸ‡ΏπŸ‡¦

2021 Alikuwa kocha Mkuu wa Township Rollers ya Botswana πŸ‡§πŸ‡Ό

2019 Alikuwa kocha Msaidizi wa Pyramid ya Egypt πŸ‡ͺπŸ‡¬

2018 Alikuwa kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Uganda πŸ‡ΊπŸ‡¬

Huyu kocha ana UEFA Pro Licence na Pro Licence ya CONMEBOL (America).

Huyu kocha ni Muhumini wa (4-3-3) na timu yake ina-press kinoma.

NABII MKUU MHE.DKT.GEORDAVIE LEO HII ATUNUKIWA SHAHADA YA HESHIMA YA UDAKTARI.

Nabii Mkuu Mhe.Dkt.GeorDavie leo ametunukiwa shahada ya Udaktari wa heshima na tuzo ikiwa ni kumuheshimisha kutokana na mambo mengi anayofanya katika kuisadia jamii.

‎Tukio hilo limefanyika katika ukumbi wa Sephil Saphire mnamo julai 5, 2025  mjini Dodoma kuanzia majira ya saa tatu asubuhi hadi saa Saba mchana na limeandaliwa na umoja wa Chama Cha Madaktati na Maprofesa Tanzania.

Akizungumza baada ya kutunukiwa shahada hiyo ya falsafa ya udaktari Nabii Mkuu Mke. Dkt. GeorDavie amesema umempa hamasa kubwa na msisimko mpya wa kuendelea kuisaidia jamii na kushughulika na mahitaji mbalimbali ya watu katika kuleta maendeleo kwa ujumla.

‎Akizungumza mara baada ya kumtunuku shahada hiyo mgeni rasmi ambaye pia ni Mwenyekiti wa umoja wa Chama Cha Madaktati na Maprofess, Prof. Rejoice Ndalima amesema kuwa Nabii Mkuu amestahili kwa sababu amekuwa akisaidia wananchi bila kubagua.

‎Aidha tukio hilo kubwa na la kihistoria limehudhuria na Madaktati na Maprofesa wa hapa nchini, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Taifa, watumishi wa Mungu pamoja na watu kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini.

Na Beatrice Maina@NYU ARUSHA.




NABII MKUU MHE.DKT GEORDAVIE ATAKA AMANI YA NCHI ILINDWE.

‎‎Nabii Mkuu Mhe.Dkt.GeorDavie amewataka wananchi kulinda Amani iliyopo nchini.

‎‎Nabii Mkuu ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na wanahabari wa vyombo mbalimbali vya habari katika ukumbi wa Sephil Saphire jijini Dodoma.

‎" Tulinde Utulivu na Amani katika Nchi ya Tanzania pia tujitoze kupiga kura kwa sababu ni swala la msingi na Haki ya Kila mtu"/Amesema Nabii Mkuu Dkt.GeorDavie Balozi wa Amani Taifa.

‎Aidha amewataka pia viongozi wa Dini kuendelea kumuombea Rais na kuyasema yote mema aliyoyafanya katika kutekeleza shughuli mbalimbali ya kimaendeleo.

‎Na Beatrice Maina@NYU ARUSHA. #GeorDavietv YouTube #GeorDavietv Instagram #GeorDavie Facebook #GeorDavie TikTok #GeorDavie Maarifa







NABII MKUU MHE DKT. GEORDAVIE LEO AMETOA ZAWADI YA GARI AINA YA BMW KWA MWALIMU ISAYA BENSON.

Nabii Mkuu Mhe.Dkt.GeorDavie mchana wa Leo amemzawadia Mwalimu wa NENO la Mungu Isaya Benson Gari aina ya BMW X5 na shilingi milioni mbili kwa msikilizaji wa NYU FM RADIO kijana Makochali ambaye alizungumza jambo lililomgusa Nabii Mkuu.

‎‎Nabii Mkuu ametoa zawadi hizo mchana wa Leo kupitia kipindi cha zijue TABIA ZA MITUME NA MANABII kinachorushwa na NYU RADIO kila siku ya jumamosi kuanzia saa nne kamili asubuhi hadi saa Saba kamili mchana.

‎‎Akitoa zawadi hiyo ya gari kwa Mwalimu Isaya Nabii Mkuu amesema anampongeza kwa kazi nzuri anayofanya ikiwemo kipindi cha Maswali na Majibu, Tabia za Mitume na Manabii na kipindi cha Hazina katika Historia huku akimuelezea Mwalimu Isaya kuwa ni kijana mchapa kazi ,anayefanya tafiti mbalimbali na anaeleza kiustarabu.

‎‎Kwa upande wake Mwalimu Isaya Benson amemshukuru Nabii Mkuu kwa kumpandisha thamani kwa mara nyingine kwa kumpa BMW X5.

‎‎Aidha mpaka muda huu ambapo habari hii inakwenda hewani bado Nabii Mkuu anaendelea na zoezi la utoaji wa zawadi kwa wasikilizaji ambao wanapata nafasi ya kupiga simu studio za NYU RADIO na kuulizwa maswali kisha kuzawadiwa shilingi elfu hamsini(50) kwa kila mtu ambapo hadi sasa watu 10 tayari wamejipatia zawadi hizo.

‎Na Beatrice Maina @NYU ARUSHA. #GeorDavietv YouTube #GeorDavietv Instagram #GeorDavie Facebook #GeorDavie TikTok #GeorDavie Maarifa



Monday, November 27, 2023

NABII MKUU DKT.GEORDAVIE AKABIDHI GARI NA SHILINGI MIL 11.4 KWA MUANDAAJI YA MISS TANZANITE MANYARA.

Nabii Mkuu Mhe.Dkt.GeorDavie ametoa gari jipya aina ya Honda station wagon yenye namba za usajili T169 EEP kwa muandaaji wa mashindano ya Miss Tanzanite Manyara Bi. Aminata pamoja na shilingi milioni 11.4.

Nabii Mkuu amekabidhi gari hilo jana katika ibada ya chuo kikuu cha manabii baada ya Bi.Aminata kuelezea changamoto anazokutana nazo katika kazi yake ambapo Nabii Mkuu aliguswa na kuamua kumsapoti gari hilo na fedha hizo ili aweze kuendesha ofisi yake ikiwa ni pamoja na kuwalipa washindi na washiriki wa mashindano hayo.

Kwa upande wake Bi. Aminata amemshukuru Nabii Mkuu kwa moyo wa upendo wa kusaidia watu huku akimuombea Nabii Mkuu Aishi miaka mingi ili awasaidie watu wengine wanaokutana na changamoto mbalimbali maishani mwao.

Na Beatrice Maina, N.Y.U ARUSHA.



NABII MKUU MHE. DKT. GEORDAVIE AISHUKURU SERIKALI KWA KUMPA BARABARA.

Nabii Mkuu Mhe Dkt.GeorDavie ameishukuru serikali kwa kutambua mchango wake katika jamii na kumpa heshima ya kuandika jina lake na huduma yake kwenye barabara mbili hapa jijini Arusha ambapo kuna barabara ya GeorDavie Road na Ngurumo ya Upako Road.

Akizungumza Nabii Mkuu amesema kuwa ataendelea kusaidia wananchi na kwamba furaha yake ni kusaidia watu huku akisema amefanya mambo mengi mema kwa watu na hakutarajia siku moja atapewa heshima kubwa kama hii ya kupewa Barabara ambazo zitakuwa ni historia hata kwa vizazi vijavyo.

Aidha kwa hapa nchini hatujaona barabara nyingine yenye jina la Mtumishi wa Mungu na Nabii Mkuu Mhe Dkt.GeorDavie amekuwa Mtumishi wa Mungu wa kwanza kupewa barabara zenye jina na huduma yake ambapo GeorDavie Road ipo barabara ya kuelekea Ikulu ya Nabii Mkuu.

Kuna Barabara nyingine kama Nyerere, Ally Hassan Mwinyi, Kawawa Road, Sokoine Road na Sasa tuna Barabara ya GeorDavie na Ngurumo ya Upako Road ambapo zinapatikana Barabara ya Dodoma Arusha.



Friday, November 17, 2023

NABII MKUU DKT. GEORDAVIE KUPANDISHA VIWANGO VYA WATU KIMAISHA.

Nabii Mkuu Mheshimiwa Dkt.GeorDavie Balozi wa Amani anatarajia kupandisha viwango vya watu kimaisha ili waondokane na umasikini.


Nabii Mkuu atawapandisha watu viwango kupitia ibada ya chuo kikuu cha manabii itakayofanyika katika nyumba ya matamko Kisongo Arusha ambapo itakuwa ni ibada ya kupanda viwango kimaisha.

Aidha amewata watu kuja na sadaka maalum ya kujiambatanisha na matamko ya kinabii ya kupanda viwango.

Na Beatrice Maina, N.Y.U RADIO.



NABII MKUU KUPOKEA ZAWADI ZA PONGEZI JUMAPILI HII NOV 19, 2023

Nabii Mkuu Mheshimiwa Dkt.GeorDavie anatarajia kupokea zawadi za pongezi kwa kuanzisha Ngurumo ya Upako  Radio ( N.Y.U. FM 99.3 MHz) kutoka kwa watoto wake wa kiroho.

Nabii Mkuu atapokea pongezi hizo ambazo ni kwa mfumo ya fedha katika ibada ya chuo kikuu cha manabii itakayofanyika jumapili katika nyumba ya matamko Ngurumo ya Upako Kisongo jijini Arusha ambapo itakuwa ni ibada ya kupanda viwango kimaisha.

Akizungumza kuhusu Radio Kadinali wa kwanza wa huduma ya Ngurumo ya Upako Mtume Gaudensia Luila amesema kuwa siku tutamshukuru Mungu kwa ajili ya radio ambayo imefanyika Baraka na msaada mkubwa kwa watu wengi ambapo kupitia radio watu wamepomea uponyaji, mitaji na Baraka mbalimbali za kiroho na kimwili.

Amesema tunapomshukuru Mungu kwa ajili ya radio pia ni wajibu wetu kumpongeza Nabii Mkuu ambaye ndiye muanzilishi na msimamizi wa Radio.

Aidha katika ibada hiyo kila mtu atapata nafasi ya kusapoti Radio pamoja na kumpongeza Nabii Mkuu kwa mambo mengi anayoyafanya kwa watu bila mbalimbali kubagua na huduma kwa ujumla.

Na Beatrice Maina, N.Y.U ARUSHA. 



Tuesday, November 14, 2023

DKT.GEORDAVIE" FEDHA INAPATIKANA KWA KUFANYA KAZI KWA BIDII."

Nabii Mkuu Mhe.Dkt.GeorDavie amewataka watu kutambua kuwa fedha inapatikana kwa kufanya kazi kwa bidii na kuwa na akili yenye ufahamu.


Nabii Mkuu ameyasema hayo wakati akizungumza na kufundisha watu hekima mbalimbali zinazoweza kuwasaidia katika maisha yao.

Akizungumza Nabii Mkuu amesema kuwa hakuna uchawi kwenye utajiri kitu kinachotakiwa ili mtu aweze kufanikiwa ni kufanya kazi kwa bidii.

Na Beatrice Maina, N.Y.U.ARUSHA.



Monday, November 13, 2023

NABII MKUU" ACHA KULIPIZA KISASI SAMEHE UISHI KWA AMANI NA FURAHA."

Nabii Mkuu Mhe.Dkt.GeorDavie Balozi wa Amani amewataka watu kuacha tabia ya kulipiza kisasi kwa watu waliowakosea na badala yake wawe watu wa kusamehe ili waweze kupokea Baraka zao kutoka kwa Mungu.


Nabii Mkuu ameyasema hayo alipokuwa akifundisha somo lililokuwa na kichwa kisemacho "Kumjua Mtakatifu ni Ufahamu"i katika ibada ya chuo kikuu cha manabii ambapo ilikuwa ni ibada ya kuongozeka kiuchumi.

Akizungumza Nabii Mkuu amesema kuwa makosa ni mengi hivyo kinachotakiwa ni kuishi katika ufahamu huku akieleza jinsi ambavyo yeye amedumu kuwasamehe watu wengi ambao walimkosea maishani.

Na Beatrice Maina, N Y.U ARUSHA.