Tuesday, January 26, 2016

BUNGE LA 11 MKUTANO WA PILI UMEANZA RASMI MJINI DODOMA


Bunge la 11 mkutano wa pili kikao cha kwanza la Jamhuri ya muungano wa Tanzania limeanza leo mjini Dodoma ambapo limefunguliwa kwa
dua pamoja na kula kiapo cha uaminifu kwa wabunge 11, ambao wamechaguliwa na wengine kuteuliwa na Rais baada ya kumalizika kwa Mkutano wa Kwanza wa Bunge.

Wabunge hao ni pamoja na Goodluck Mlinga wa Jimbo la Ulanga, Shaaban Shekilindi wa Lushoto, Godbless Lema wa Arusha Mjini, Omar Kigoda Jimbo la Handeni, Deogratias Ngalawa wa Ludewa na Rashid Chauchau wa Masasi.
Spika wa Bunge la Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania..Mh. Job Ndugai

Maswali kadhaa yameulizwa na wabunge na kisha kujibiwa ambapo kwa siku ya leo jumla ya maswali ya msingi ya kawaida 125 yanategemewa kuulizwa na kujibiwa.
Maswali yaliyoonesha kuwagusa wengi ni pamoja na maswali yaliyohusu tatizo la njaa linalokabili maeneo mbalimbali hapa nchini, elimu, maliasili pamoja na  maji.
Kuhusu tatizo la njaa serikali imesema itaendelea kufanya tathmini ya hali ya njaa nchini na kwamba hakuna mtanzania yeyote atakayekufa njaa kutokana na ukosefu wa chakula.
Akijibu swali la Mbunge wa Mpwapwa mkoani Dodoma George Malima Lubeleje aliyetaka kufahamu hatua ambayo serikali imechukua kukabilina na njaa katika wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu amesema serikali imeanzaa kugawanya chakula cha msaada.

No comments:

Post a Comment