Wednesday, March 27, 2019

WABARIKIWA FEDHA KWAAJILI YA KUKUZA BIASHARA ZAO..



Neema ya kifedha imewatembelea baadhi ya watu waliokuwa na mahitaji ya fedha kwaajili ya kukuza biashara zao pamoja na kulipa madeni, ambapo Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie aliwapatia fedha taslimu kwaajili ya kukidhi mahitaji yao.
Ni siku ya jumapili katika Ibada ya jiji, iliyofanyika katika katika hema la kukutania Ngurumo Ya Upako.. Kisongo, Arusha ambapo jumla ya 1,200,000 (milioni moja na laki mbili) ilitolewa nae Nabii Mkuu kwaajili ya kuwa-support kwenye shughuli zao waweze kujikimu kimaisha.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti watu hao wameelezea ugumu waliokuwa wakiupata kiuchumi na wepesi waliouona mara baada ya kubarikiwa kifedha nae Nabii Mkuu na kuahidi kufanya kazi kwa bidii kuhakikisha wanaitendea haki fedha waliyopewa na Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie.
Aidha siku ya jumapili katika Ibada ya Chuo Kikuu Cha Manabii ilikuwa ibada ya "Kupatiwa uelekeo mpya na sahihi maishani" ambapo Nabii Mkuu alifanya Huduma ya Unabii wa mtu mmoja mmoja wa kupita katikati ya maelfu ya watu waliofika siku ya jana na kuwahudumia kila mmoja kwa nafasi yake.
Akizungumza Nabii Mkuu alisema kuwa watu wengi wanateseka maishani kwa sababu ya uelekeo mbaya/ usiokuwa sahihi waliokuwa nao ambao huwapelekea kuteseka kwa maumivu na vifungo mbalimbali vya nguvu za giza, ambapo Nabii Mkuu aliwafungua na kuwatamkia matamko mbalimbali ya kuwapatia uelekeo mpya.
Wakati huo huo Nabii Mkuu ametangaza kuwepo tena jumapili ya tarehe 31/3/019 itakayokuwa ibada kufidiwa muda uliopotea.

NB: Usisahau ku-download application ya GeorDavie Ministries itakayo kuwezesha kutazama GeorDavie Tv pamoja na kusikiliza 99.3 N.Y.U Radio

No comments:

Post a Comment