Tuesday, February 19, 2019

WAPEWA PESA ZA MITAJI MIDOGO...!!


Jumla ya sh. Milioni moja, laki tisa na elfu hamsini (1,950,000) zimetolewa na Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie kwa watu takribani kumi (10) wenye uhitaji wa aina mbalimbali waliojitokeza.
Ni katika ibada ya Chuo Kikuu Cha Manabii iliyofanyika katika hema la kukutania Ngurumo Ya Upako, ambapo Nabii Mkuu aliwataka watu wenye uhitaji wa pesa za kujikimu kujitokeza ambapo watu hao walijitokeza na kuweza kupata Neema hiyo ya kusaidiwa na Nabii Mkuu.
Pia watu wengine tofauti tofauti kwa nyakati tofauti wameweza kufikiwa na neema ya kusaidiwa kifedha na Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie ambapo amekuwa akituma pesa kwa kadiri jinsi Roho Wa Mungu amekuwa akimuongoza kuwasaidia watu hao ambao wamekuwa wakimuelezea uhitaji wao pamoja na hali ngumu wanazopitia kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi kwa kupitia namba ya kunyanyua mikono ya Nabii.
Aidha Nabii Mkuu anatarajia kuwepo siku ya ijumaa katika hema la kukutania Ngurumo Ya Upako, Kisongo, Arusha ambapo itakuwa ni siku ya International Partners (IP) siku ambayo ni maalum kwa wana-International Partners kuwasilisha michango yao kwaajili ya ku-support GeorDavie Tv mikononi mwa Nabii Mkuu.

NB: Usisahau ku-download application ya GeorDavie Ministries itakayo kuwezesha kutazama GeorDavie Tv pamoja na kusikiliza 99.3 N.Y.U Radio

No comments:

Post a Comment