Sunday, February 3, 2019

ZAIDI YA MILIONI 14 YATOLEWA KWA JAMII- JANUARY..



Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie ametoa zaidi ya sh. 14,490,000 (Milioni kumi na nne, laki nne na elfu tisini), kwa mwezi wa January kama zawadi na misaada kwa watu mbalimbali.
Fedha hizo zimetolewa kwa nyakati tofauti tofauti kwa kupitia vipindi mbalimbali vilivyokuwa vikiruka kupitia 99.3 N.Y.U FM pamoja na GEORDAVIE TV lakini wengine wakiweza kujipatia zawadi zao kwa kupitia ibada za Chuo Kikuu Cha Manabii.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya watu walioweza kujishindia zawadi hizo, wamemshukuru Nabii Mkuu kwa zawadi hizo huku wakieleza pia jinsi ambavyo fedha hizo zimeweza kuwasaidia katika maeneo mbalimbali maishani mwao ikiwa ni pamoja na kutatua matatizo ambayo walikuwa nayo.
Katika mwaka huu wa 2019 ambao ni "Mwaka wa kujenga uwezo" Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie, amesema kuwa hizi ni Zama Mpya ambapo Serikali tukufu ya Ufalme wa Mungu inawagusa watu wenye mahitaji kwa njia ya tofauti ambayo ni ya kuwasaidia kifedha na huu ukiwa muendelezo wa zoezi hilo lililoanza mwishoni mwa mwaka jana na bado likiwa endelevu.

NB: Usisahau ku-download application ya GeorDavie Ministries itakayo kuwezesha kutazama GeorDavie Tv pamoja na kusikiliza 99.3 N.Y.U Radio

No comments:

Post a Comment