Monday, February 17, 2014

(NEWS). MADEREVA WA BENAKO WILAYA YA NGARA WALIA NA KUMALIZIWA KWA EGESHO LA MAGARI

Baadhi ya madereva katika mji mdogo wa Benako Wilayani Ngara mkoani Kagera wameiomba halmashauri ya wilaya hiyo kukamilisha ujenzi wa kituo cha kuegesha magari kilichoanza kujengwa tangu miaka mitatu iliyopita kwenye eneo hiloWakiongea na N.Y.U Radio madreva hao wamesema wanapata shida katika kusafirisha na kushusha abiria kutokana na kuwepo msongamano wa magari makubwa yanayokwenda na kutoka katika nchi za maziwa makuu.Mmoja wa maderva hao amesema kuwa kituo cha kuegesha magari katika mji wa benaco kiliwekewa jiwe la msingi katika mbio za  mwenge kitaifa mwaka juzi lakini hadi  kufikia sasa wananchi hawaoni kinachoendelea katika ujenzi huo.
Aidha Diwani wa kata ya kasulo Dr Philbert Kiiza amesema ucheleweshwaji wa kujenga kituo hicho umechangiwa na wenye viwanja katika eneo la ujenzi kutojenga makazi kwa kufuata taratibu za mipango miji katika kata humo.

No comments:

Post a Comment