Monday, March 30, 2015

IBADA YA JUMAPILI TAREHE 29/MARCH/2015

Maelfu ya watu waliokusanyika katika chuo kikuu cha Manabii Kisongo katika ibada ya jiji wamepokea Baraka mbalimbali za kinabii na kufunguliwa katika vifungo mbalimbali.

Katika ibada hiyo Nabii Mkuu Mheshimiwa Dr.GeorDavie ametamka Baraka kwa watu wote wanaomwami Nabii  kupokea siku saba za ukamilifu wa uponyaji katika miili yao huku wakiendelea na siku 41 za maadui kubeba mizigo yao.




DR.  GeorDavie ametangaza kuwa mienzi tisa hii iliyobaki ili kumaliza mwaka wa 2015 ni mienzi ya kuona faida katika kila eneo na pia ametamka kwa watu wanaomuaminia nabii kuzaa matunda kila mwezi katika kila eneo.
Amefafanua kuwa maneno ya kinabii yanayotamkwa kila siku ni ya thamani  hivyo ni lazima yafanyiwe kazi  kwani  wapo maelfu ya watu  wanaotamani kuwa na neema ya kuwa na nabii katika nchi zao.

Hata hivyo mtumishi mwanafunzi William James  ameitaka jamii  kutambua wakati na mambo ya kimungu yanavyoendelea na kumsikiliza mungu anayezungumza sasa kwa wakati wetu na siyo kusismamia mambo yale Mungu aliyoyafanya na watu wa zamani.

Sanjari na hayo watu wengi wameweza kufunguliwa vifungo mbalimbali ikiwemo watu waliokuwa kukosa raha na amani wametamkiwa furaha na amani na hali hiyo kutoweshwa kwao,huku nabii mkuu akitamka kwamba katika wiki hii tutakumbuka mahali ambapo Mungu ametutoa na sasa  tulipofika.


SIKILIZA NA DOWNLOAD NENO LA KUNABII LA WIKI HII.


No comments:

Post a Comment