Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe
12 Septemba, 2017 ametembelea hospitali ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi
Tanzania (JWTZ) Lugalo, Jijini Dar es Salaam na kumjulia hali Meja Jen.
Mstaafu Vincent Mritaba aliyelazwa hospitalini hapo baada ya
kushambuliwa na watu wenye silaha wakati akiingia nyumbani kwake Ununio,
Kinondoni Jijini Dar es Salaam.