Tuesday, January 22, 2019

ATOA ZAWADI YA PIKIPIKI NA PESA KEM KEM KAMA ZAWADI KWA WATU WALIOWEZA KUJIBU MASWALI!


Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie amezidi kubariki jamii kwa kumwaga pesa ikiwa ni mara baada ya kutoa zawadi ya pikipiki pamoja na pesa taslim, zaidi ya shilingi milioni moja kama zawadi.

Nabii Mkuu alitoa zawadi ya Pikipiki yenye thamani ya shilingi Milioni mbili na laki nne (2,400,000) kwa Ndugu. Tito Paul pamoja na zawadi ya pesa alizojishindia kwa kujibu maswali aliyomuuliza kwa ufasaha kabisa.
Kwa upande wake Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie akizungumzia hilo amewataka watu kuchangamkia nafasi ya kujibu maswali hayo kwani kwa kufanya hivyo watajiongezea nafasi ya kushinda zawadi mbalimbali kama magari, nyumba, pikipiki na pesa za mtaji, ada na za kujikimu katika mahitaji mengine.
Akielezea mgawanyiko wa maswali yanayoulizwa katika vipindi hivyo Nabii Mkuu amesema kuwa maswali hayo yamegawanyika katika sehemu tatu (3).. 60% yakiwa yanahusu huduma, 20% N.Y.U Radio na 20% nyingine yakiwa yanahusu GeorDavie Tv ambapo watu wametakiwa kufuatilia vipindi kwa makini pamoja na kuhudhuria ibada katika Hema la Kukutania Ngurumo Ya Upako ili kupata uelewa zaidi wa kuweza kujieleza ili waweze kushinda zawadi hizo.
Akifafanua zaidi Nabii Mkuu amesema kuwa haya ni majira mapya ambayo Serikali Tukufu Ya Ufalme Wa Mungu inawabariki watu wake kwa njia ya tofauti ambapo amesema kuwa zoezi hilo bado linaendelea.
Tangu kuanza kwa mwaka huu Nabii Mkuu ametoa zaidi ya shilingi milioni nane (8) kwa jamii, ambapo zawadi hizo watu wamekuwa wakijishindia kwa njia ya kujibu maswali katika vipindi mbalimbali vinavyoruka kupitia 99.3 N.Y.U RADIO pamoja na GEORDAVIE TV.
Katika muendelezo wa utoaji wa zawadi hizo Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie ametangaza kuwepo tena katika kipindi cha "Q & A AKILI KUBWA" kitakachoruka Live kwa njia ya 99.3 N.Y.U RADIO pamoja na GEORDAVIE TV jumatano ya week hii, kuanzia majira ya saa mbili na nusu usiku, ambapo atakuwa akiuliza maswali na kutoa zawadi ya pesa kwa washindi watakaojibu vizuri.
Aidha Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie ameitangaza week hii kuwa ni week ya kung'oa kila pando la adui na mabaya yote na kuongeza kuwa week hii Roho Wa Mungu atadumu kung'oa kila pando la adui lenye lengo la kudhoofisha watu.
NB: Usisahau kudownload application ya GeorDavie Ministries itakayo kuwezesha kutazama GeorDavie Tv pamoja na kusikiliza 99.3 N.Y.U Radio

No comments:

Post a Comment