Tuesday, January 8, 2019

JE UNAFAHAMU KUWA MHE. DR. GEORDAVIE KATIKA MWAKA 2018 PEKEE AMETUMIA ZAIDI YA SH. MILIONI 143 KATIKA KUSAIDIA JAMII???


   Amekuwa akitambulika kama Mtumishi wa Mungu mtoaji zaidi Nabii wa Equator, Nabii Mkuu wa karne ya 21, si mwingine ni Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie kutoka Arusha, Tanzania.
  Na siku ya leo tunakuletea kwa uchache baadhi ya matukio ya utoaji aliyoweza kuyafanya kwa mwaka wa 2018 yaliyopelekea Nabii Mkuu ambaye amekuwa msaada na kipenzi cha wengi kutajwa kama Mtumishi Wa Mungu mtoaji zaidi.
  Katika ku-support Watumishi Wa Mungu kutoka katika makanisa mengine tofauti na Ngurumo Ya Upako yaliyo ndani na nje ya Tanzania, Nabii Mkuu ametumia zaidi ya Sh. Milioni 30 katika kuhakikisha anatoa misaada katika huduma hizo ambapo kwa asilimia kubwa zilikuwa haziridhishi kiuchumi (hazijamudu kujitegemea kiuchumi), Nabii Mkuu aliweza kuwasaidia ili kuhakikisha watumishi wanaweza kukidhi mahitaji yao lakini pia ikiwa ni pamoja na kuwasaidia kujenga makanisa yao ili yawe katika hali ya kuridhisha.
  Katika upande mwingine wa kijamii, Nabii Mkuu amekuwa na kawaida ya kupeleka misaada sehemu mbali ikiwa ni pamoja na katika vituo vya watoto yatima ambapo kwa mwaka 2018 Nabii Mkuu amepeleka katika vituo vitatu tofauti hapa Tanzania.
   Mbali na hayo pia Nabii Mkuu ametoa misaada mingine ikiwemo kuwalipia ada wanafunzi wa ngazi mbalimbali mpaka chuo kikuu waliokwama kutokana na kukosekana kwa kipato ili kuwawezesha kuendelea na masomo yao.
  Aidha katika kusaidia watu pia Nabii Mkuu ametumia zaidi ya Milioni 20 katika kusaidia watu mbalimbali wenye mahitaji, ikiwemo wenye uhitaji wa mitaji lakini pia wenye biashara ndogo ndogo katika kuhakikisha wanaweza kuwa na kipato cha kujikimu kimaisha.
  Lakini pia katika upande mwingine Nabii Mkuu amekuwa akiwa-support watu wenye vipaji kwa namna mbalimbali ambapo baadhi ya waliopata neema hiyo ni pamoja na vijana wawili walionunuliwa ngoma na mwingine spika ,kila mmoja kwa wakati wake pamoja na waimbaji wa nyimbo za injili kutoka sehemu mbalimbali.
  Hakuishia hapo katika kusaidia tu, Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie amekuwa akitoa zawadi mbalimbali kwa watu ambapo kwa mwaka wa 2018 ametoa zawadi ya magari nane (8) kwa watu tofauti tofauti wa ndani na nje ya nchi kwa mwaka huo yenye thamani ya jumla milioni 88.
  Aidha katika msimu wa sikukuu mpaka sasa Nabii Mkuu ametoa zawadi kwa njia ya pesa taslimu za zaidi ya sh. Milioni 5 kwa watu mbalimbali ambao walijishindia kwa njia ya kupiga simu kwenye vipindi vilivyokuwa vikiruka kupitia 99.3 N.Y.U FM Radio pamoja na GeorDavie Tv (zoezi hilo linaendelea mpaka sasa) na wengine wakijishindia kupitia mitandao ya kijamii.
  Akizungumzia utoaji huo Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie amesema haya "hiyo ni njia ya Ufalme Wa Mungu kuwabariki watu wake kwakuwa nao wamekuwa wakitoa kwa Ufalme Wa Mungu hivyo sasa ni wakati wao kubarikiwa pia" mwisho wa kunukuu.
         NB: Usisahau kudownload application ya GeorDavie Ministries itakayo kuwezesha kutazama GeorDavie Tv pamoja na kusikiliza 99.3 N.Y.U Radio.

No comments:

Post a Comment