Tuesday, January 15, 2019

NABII MKUU MHE. DR. GEORDAVIE ATANGAZA WIKI YA USHINDI KATIKA MAENEO YOTE MAISHANI.




 KUTOKA IKULU YA NABII MKUU TANZANIA..

    Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie ametangaza kuwa hii ni wiki ya kuwa washindi katika maeneo yote maishani.
    Ameyasema hayo wakati akiongoza ibada ya chuo kikuu cha manabii iliyofanyika katika hema la kukutania, Ngurumo Ya Upako, Kisongo, Arusha.
   Katika ibada hiyo ambayo pia ilikuwa ni ibada ya Silver Partners, Nabii Mkuu alitamka baraka mbalimbali za Kinabii kwa wana-Partners wote ikiwemo baraka ya kushika pesa na kuheshimika.
   Aidha Nabii Mkuu alifundisha umuhimu wa kuwa mwana-Partners na faida zake huku akiwasisitizia watu wote kusapoti kazi ya Mungu kwa nguvu kwa kuna baraka ya kipekee wataipata kwa kufanya hivyo na kuwakumbusha kuwa ili kazi ya Mungu iwe nzuri na ithaminiwe ni lazima igharamikiwe ambapo alitoa nukuu isemayo "Cha gharama kina thamani kama hakina gharama hakina thamani" akimaanisha kuwa kitu chochote chenye thamani lazima kiwe cha gharama hakiwezi kuwa bure ikiwemo Nguvu Ya Mungu.
   Wakati huohuo Nabii Mkuu Mhe. Dr. GeorDavie ametangaza kuwepo katika kipindi cha Maswali Na Majibu  kitakachoruka LIVE kwa njia ya Radio,  99.3  N.Y.U FM pamoja na GEORDAVIE TV siku ya jumatano ambapo kwa siku hiyo yeye ndiye atakayeuliza maswali kwa wasikilizaji na watazamaji na kisha kutoa zawadi ya pesa taslimu kwa wale watakaopatia kwa kujibu maswali hayo vizuri. 


          NB: Usisahau ku-download application ya GeorDavie Ministries itakayo kuwezesha kutazama  GeorDavie Tv pamoja na kusikiliza 99.3 N.Y.U Radio.

No comments:

Post a Comment