Waziri
 Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema kuwa 
Tanzania siyo lango la kupitishia dawa za kulevya kwenda nchi za nje 
hivyo ameagiza ulinzi uimarishwe katika mipaka yote ya nchi na kuwa wale
 watakaobainika watachukuliwa hatua kali.
Majaliwa
 amesema hayo wakati akizungumza na watumishi wa kituo cha forodha cha 
Kasumulu kilichopo mpakani mwa Tanzania na Malawi wilayani Kyela,.
 
 
Amesema
 kuwa kunatabia ya baadhi ya watu wasiokuwa waaminifu kuitumia Tanzania 
kama njia ya kupitisha dawa za kulevya kwa ajili ya kupeleka nchi 
za Afrika ya Kusini, Malawi na Zambia.
za Afrika ya Kusini, Malawi na Zambia.
“Endeleeni
 kufanya upekuzi wa kina wa magari, watu na mizigo yote yote katika 
mipaka yetu. Tanzania siyo lango la kupitishia dawa za kulevya na 
Serikali haitakubaliana na jambo hilo.”
Aidha,
 Majaliwa amewataka viongozi hao kuhakikisha biashara zote za magendo 
zinazofanyika mipakani, zikiwemo za kubadilisha fedha zinadhibitiwa kwa 
kuwa zinaikosesha Serikali mapato.
Hata
 hivyo, ameongeza kuwa ni vema yakawepo maduka ya kubadilishia fedha 
katika maeneo hayo ili kudhibiti biashara hiyo ambayo kwa sasa inafanywa
 kimagendo huku Serikali ikikosa kodi.
 
 
No comments:
Post a Comment