Thursday, May 10, 2018

Malaysia yapata kiongozi mkongwe zaidi duniani aliyechaguliwa

Dr.Mahathir Mohamad aibuka mshindi akiwa na miaka 92
Waziri mkuu wa zamani wa Malaysia Dr.Mahathir Mohamad amepata ushindi wa kihistoria katika uchaguzi mkuu uliofanyika katika hilo. Kiongozi huyo ameweza kukiangusha chama ambacho kimekuwa madarakani tangu mwaka 1957 ambacho kimekuwa kikidaiwa kujihusisha na nasuala ya rushwa na ufisadi.

Dr.Mahathir ameshinda kwa idadi ya uwingi kura,na kukibwaga chama cha Barisan Nasional kilichotawala kwa zaidi ya miaka 60.
Akiwa na umri wa miaka 92 Mhathir ameachana na kuitwa mstaafu na amerejea tena kuchukua nafasi ya mfuasi wake huyo wa zamani yaani Najib Razak ambaye utawala wake umekuwa na shutma kadhaa za rushwa.
Ibrahim Suffian, ni mtafiti wa masuala ya uchaguzi wa kujitegemea wa mjini Kuala Lumpur,anasema matokea haya yameleta mmshituko mkubwa.
Wasiwasi wa kiuchumi ndio suala kuu miongoni mwa raia waliopiga kura Jumatano
"Nafikiri jambo hili,na kufanikiwa kutekeleza mambo kadhaa yanayoonekana kuwa kikwazo.Jambo la kwanza ataunda muungano unaoshirikisha vyama vingine vya upinzani,na mbili nafikiri amewezakuwa na ushiwishi mkubwa kubainisha matatizo ya kisiasa ambayo yamekuwa yakiikabili Malaysia kwa takribani miaka 60 iliyopita,kama masuala ya kodi na mikasa ya rushwa ambayo ilimhusisha hata waziri mkuu pia."
Najib Razak kashindwa na mengi kwani pia anahusishwa na kashfa ya kudaiwa kujipatia kiasi cha dola 700 kutoka taasisi moja ya maendelea ya Malaysia na mamlaka zinaendelea kuchunguza kashfa hiyo.
Kufuatia ushindi wa Dr Mahathir, serikali imetangaza mapumnziko ya siku mbili ya kitaifa kwa siku ya Alhamis na Ijumaa.

No comments:

Post a Comment