Monday, November 27, 2023

NABII MKUU DKT.GEORDAVIE AKABIDHI GARI NA SHILINGI MIL 11.4 KWA MUANDAAJI YA MISS TANZANITE MANYARA.

Nabii Mkuu Mhe.Dkt.GeorDavie ametoa gari jipya aina ya Honda station wagon yenye namba za usajili T169 EEP kwa muandaaji wa mashindano ya Miss Tanzanite Manyara Bi. Aminata pamoja na shilingi milioni 11.4.

Nabii Mkuu amekabidhi gari hilo jana katika ibada ya chuo kikuu cha manabii baada ya Bi.Aminata kuelezea changamoto anazokutana nazo katika kazi yake ambapo Nabii Mkuu aliguswa na kuamua kumsapoti gari hilo na fedha hizo ili aweze kuendesha ofisi yake ikiwa ni pamoja na kuwalipa washindi na washiriki wa mashindano hayo.

Kwa upande wake Bi. Aminata amemshukuru Nabii Mkuu kwa moyo wa upendo wa kusaidia watu huku akimuombea Nabii Mkuu Aishi miaka mingi ili awasaidie watu wengine wanaokutana na changamoto mbalimbali maishani mwao.

Na Beatrice Maina, N.Y.U ARUSHA.



No comments:

Post a Comment