IBADA YA CHUO CHA UPONYAJI TAREHE 12/February/2015.
Nabii Mkuu Mh.Dr.GeorDavie ametoa Unabii wa Muda wa miezi mitano kuanzia
Februari hadi June mwaka huu kuwa kuna mambo yatakayotokea ambayo yatakuwa ya
kushangaza. Mh.Dr.GeorDavie ametoa Unabii huo leo wakati wa ibada ya Chuo cha
Uponyaji iliyofanyika katika hema la Kukutania la Ngurumo ya Upako Chuo Kikuu
cha ManabiiKisongo nje kidogo ya jiji
la Arusha.Akitoa unabii huo amesema kuwa kuanzia mwezi huu kuna vikao fulanifulani vya
mashetani vinavyodai damu za watu lakini watu wanaomwamini Nabii watakuwa
salama.
Katika ibada hiyo iliyohudhuriwa na watu kutoka ndani na nje ya jiji la
Arusha ambao waliweza kufunguliwa kutoka kutoka katika vifungo mbalimbali vya
nguvu za giza huku wengine wakitamkiwa maneno mbalimbali ya Unabii.
Pamoja na mambo mengine Nabii Mkuu amewatamkia watu wote wanaoamini nguvu
ya Kinabii kuwa Mungu amewatua mizigo yote na wako huru kabisa kukaa katika imani
sahihi na Neno la Mungu.
Nabii Mkuu Mh.Dr.GeorDavie atakuwepo katika ibada ya chuo cha uponyaji Alhamisi
Ijayo ya februari 19 katikia hema la Kukutania la Ngurumo ya Upako Chuo Kikuu
cha Manabii ambapo amesema kuja kwake si bure bali ni kwa sababu ya vitu
ambavyo Mungu amemuonye kwa ajili ya watu wake.