Saturday, October 28, 2023

NABII MKUU MHE. DKT. GEORDAVIE JUMAPILI YA KESHO ATAONGOZA IBADA YA CHUO KIKUU CHA MANABII

Nabii Mkuu Mhe. Dkt. GeorDavie jumapili hii anatarajia kuongoza ibada ya chuo kikuu Cha manabii ambapo itakuwa ni ibada ya kupokea hekima na ufahamu.

Akizungumza kuhusu ibada hiyo Nabii Mkuu amesema kuwa pia itakuwa ni siku ya kuwasilisha sadaka za International Partner kwa ajili ya ununuzi wa viti.

Amesema kuwa katika ibada hiyo ya kupokea hekima na ufahamu neno la linalosimamia ni kutoka katika kitabu cha Mithali 9:10 unaosema "Kumcha Bwana ni mwanzo wa hekima na kumjua mtakatifu ni ufahamu"

Aidha Nabii Mkuu amemtaka kila mtu kuwahi ibadani,kuja na sadaka ya international partner pamoja na sadaka maalum ya kupokea hekima na ufahamu.

Na Beatrice Maina, N.Y.U ARUSHA.


No comments:

Post a Comment