Waziri
 wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu 
ametoa agizo kwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kuhakikisha haitoi 
rufaa ya matibabu nje ya nchi ikiwa wana uwezo wa kutibu maradhi husika 
hapa nchini.
Ummy
 amesisitiza wataalamu kutowaogopa wanasiasa ikiwa wana uwezo wa kumtibu
 mgonjwa hapa nchini haina ulazima wa kumwandikia rufaa nje ya nchi hata
 akiwa ni Rais John Magufuli.
Ametoa
 agizo hilo leo Jumatatu wakati akipokea msaada wa vifaa vipya kwa ajili
 ya vyumba viwili vya upasuaji vya watoto wadogo na wodi ya watoto ya 
upasuaji vyenye thamani ya Dola za Marekani 675,000 sawa na Sh1.5 
bilioni,  kutoka kwa wataalamu na wahisani kutoka nchini Uingereza 
kupitia taasisi ya Archie Wood Foundation.
"Rais
 aliponiteua aliniagiza kwamba lazima niachane na rufaa za nje, hatuwezi
 kuachana nazo ikiwa magonjwa yanayoweza kutibiwa ndani yatatibiwa nje,"
 amesema Ummy.
Amesema
 Watanzania wana imani na  Muhimbili  na hivi sasa wengi wanatoka 
hospitali za kulipia na kufuata matibabu ila changamoto iliyopo ni 
majengo lakini wapo mbioni kujenga jengo la ghorofa kwa ajili ya 
wagonjwa wa kulipia.
"Msitoe
 rufaa ya mgonjwa kama hamjajiridhisha kwamba mnaweza kumtibu hapa hata 
kama awe Rais, waziri au nani msitoe rufaa kwani maana yake mtakuwa 
mmeshindwa ni lazima ninyi mseme kwamba hamuwezi na sisi 
tutashughulikia," amesema.
Amewatahadharisha
 wataalamu hao na wanasiasa kwamba lazima wahakikishe kweli hawawezi 
kutibu na kwamba wizara ipo tayari na itawaunga mkono.
 

 
No comments:
Post a Comment