Mwenyekiti
 wa kamati ya Spika iliyochunguza uchimbaji wa almasi, Azzan Mussa Zungu
 amesema vita ya kupigania rasilimali za nchini imewaunganisha wabunge 
wa vyama vyote.
Kamati
 hiyo iliyoundwa na Spika wa Bunge, Job Ndugai ilipewa jukumu la 
kutathmini mfumo wa uchimbaji, usimamizi, umiliki na udhibiti wa madini 
ya almasi nchini.
Zungu
 ambaye ni mbunge wa Ilala, amesema leo Septemba 7 kuwa wabunge wote 
wanatamani rasilimali za Tanzania zitumike na Watanzania na si kuwapa 
furaha wawekezaji kutoka nje.
“Kamati
 ilipoenda Shinyanga ilibaini upungufu mkubwa katika usimamizi wa madini
 yanayochimbwa na hata wachimbaji wanapofanya ndivyo sivyo, bodi ya 
almasi haichukui hatua yoyote,” amesema Zungu.
Amesema bodi ya almasi imewaangusha Watanzania kwa kushindwa kusimamia vizuri madini hayo ya vito kama ambavyo imepewa dhamana.
“Mgodi
 wa almasi uliopo Shinyanga umekuwa kama shamba la bibi, viongozi wa 
Serikali walikuwa wanaenda kule kuchota fedha na kugawana,” amesema.
Amesema hayo wakati wa kukabidhi ripoti kwa Rais John Magufuli, Ikulu jijini Dar es Salaam.
 

 
No comments:
Post a Comment