Halmashauri zote nchini zimetakiwa kutenga maeneo ya michezo wakati wa
kupanga mipango miji kwa matumizi bora ya ardhi katika maeneo yao.
Wito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Anastazia Wambura alipokuwa akifunga fainali ya mashindano ya
Jimbo Cup inayodhaminiwa na Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini Mhe. Mbunge wa
Mbulu Vijijini, Flatei Massay iliyochezwa katika eneo la kata ya Dongobesh
Wilaya ya Mbulu Mkoani wa Manyara.
“Natoa wito kwa Halmashauri zote ikiwemo halmashauri yenu ya wilaya ya
Mbulu wakati wa kupanga matumizi bora ya ardhi kwa ajili ya mipango miji
mkumbuke kutenga maeneo ya michezo, Baraza la Michezo la Taifa litatoa mafunzo
ya michezo na utaalam” alisema Naibu Waziri Wambura.