Wednesday, April 4, 2018

Rais Magufuli Kuzindua Ukuta Katika Migodi ya Tanzanite


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe, Dkt. John Pombe Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi Ijumaa hii Aprili 06, 2018 kwenye uzinduzi wa ukuta kwenye migodi ya Mirerani mkoani Arusha.

Tarehe 30 Septemba mwaka jana, Rais Magufuli aliamuru kujengwa ukuta huo kuzunguka eneo la Mererani ili kulinda madini ya Tanzanite na kuiwezesha serikali kukusanya kodi kwa urahisi.

No comments:

Post a Comment