Friday, June 8, 2018

Waziri wa Elimu: Serikali Haitavumilia Walimu Wanaoshiriki Vitendo Vya Udhalilishaji Kwa Wanafunzi

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako Ndalichako ameweka wazi kwamba serikali haiwezi kuvumilia vitendo vya udhalilishaji  ambavyo vimeonekana kufanywa na mwalimu wa shule St. Florence iliyopo jijini Dar es salaam.

Waziri Ndalichakoameyasema hayo  wakati akikabidhi zawadi kwa shule na wanafunzi wa darasa la saba, kidato cha nne na sita jijini Dodoma  baada ya kufanya vizuri kwenye matokeo ya mwisho ya mitihani yao.

Akizungumzia suala hilo Ndalichako amewahakikishia wananchi kuwa mwalimu aliyewafanyia udhalilishaji wanafunzi wa kike wa shule ya Mt. Florence vyombo vya dola vinaendelea na uchunguzi lakini watahakikisha serikali inawamchukulia hatua kali.

Pamoja na hayo Waziri Ndalichako ameshauri walimu wa kike kusafiri na wanafunzi wa jinsia ya kike katika ziara mbalimbali za kishule badala ya wanaume ili kuepukana na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kama ilivyowatokea wanafunzi wa shule St. Florence.

Hivi karibuni kuliibuka sintofahamu ndani ya jiji la Dar es salaam na Tanzania kwa ujumla baada ya kuwepo na taarifa kwamba katika shule ya St. Florence mwalimu mmoja aliyetajwa kwa jina la Ayubu kudaiwa kuwanajisi watoto wanne wa darasa la saba.

No comments:

Post a Comment