Bunge la Niger limepiga kura kwa
kauli moja, kutuma vikosi nchini Nigeria kujiunga na mapambano ya kikanda dhidi
ya kundi la Boko Haram. Kulingana na azimio la bunge hilo, Niger itatuma
wanajeshi 750 nchini Nigeria.
Wavuvi hawaendi tena ziwani kuvua, wakulima
hawaendi tena mashambani, shule zimefungwa. Wakaazi wa maeneo ya mpakani ya
Diffa na Bosso, kusini mwa Niger wamejawa na hofu, kutokana na magaidi
waliojigeuza wapiganaji wa jihadi, ambao wanatishia usalama wa taifa lao."
Hao ni makatili tu wasioheshimu sheria, wanaiba, kuuwa, na kubaka,"
alisema Abdou Lokoko, mfanyakazi wa shirika lisilo la kiserikali nchini Niger.