Wednesday, November 29, 2017

Korea Kaskazi Yarusha Kombora La Masafa Marefu Zaidi Linaloweza Kutua Sehemu Yoyote Duniani

Korea Kaskazini imelifanyia majaribio kombora lake la masafa marefu lililoruka juu zaidi na kudumu angani kwa dakika 53 kabla ya kutua katika bahari ya Japani.
Kwa mujibu wa waziri wa maswala ya ulinzi nchini Marekani James Mattis, kombora hilo ni hatari zaidi kwa sababu liweza kutua katika kona yoyote ile ya dunia ikiwemo Marekani.

Komora hilo liliruka kwa urefu wa kilomita 4,500 na kusafiri umbali wa kilomita 960 kulingana na jeshi la Korea Kusini.

Mara ya mwisho kwa  taifa hilo kulifanyia jaribio kombora lake ni mwezi Septemba. Wakati huo, kombora lake la mwisho lilikuwa la sita la nguvu za kinyuklia mwezi huo.

Korea Kaskazini imeendeleza mpango wake wa kinyuklia pamoja na ule wa utengenezaji wa makombora licha ya vikwazo ilivyowekewa.

Baraza kuu la usalama la umoja wa mataifa linatarajiwa kukutana katika kikao cha dharura ili kuzungumzia hatua hiyo ya kombora lililorushwa jana.

Rais wa Marekani Donald Trump aliarifiwa kuhusu hatua hiyo wakati ambapo kombora hilo bado lilikuwa angani  ambapo aliishia tu kusema ''Tutalishughulikia''.

No comments:

Post a Comment