Monday, November 6, 2017

RAIS MAGUFULI AZUNGUMZIA NDEGE YA BOMBADIER ILIYOZUIWA CANADA

Rais John Magufuli amemwandikia barua waziri mkuu wa Canada kuulizia kuhusu ndege ya Bombadier, inayoshikiliwa nchini humo na kumtaka ashughulike suala hilo kwa haraka.

Akizungumza katika uzinduzi wa Uwanja wa ndege mjini Bukoba leo Jumatatu
Novemba 6, Rais Magufuli amesema amemtuma pia Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju kwenda Canada kushughulikia suala hilo kisheria.

"Nimemwandikia barua waziri wa Canada kuulizia kwanini ndege yetu inakaa zaidi ya miezi sita, tumechoka kusubiri. Nimemtuma pia mwanasheria mkuu ili akapambane nao kisheria," amesema.

Amesisitiza kwamba kama wameamua kupambana kisheria watapambana na amewataka wanasheria wa Tanzania kushikamana ili kuhakikisha kwamba ndege hiyo inakuja Tanzania.

Rais Magufuli amewaonya wananchi pia kuacha kuzungumza kwenye mitandao ya kijamii. Alisema “ninawaomba watu wa vyama vyote waunge mkono juhudi hizi zinazofanywa na serikali.”


Magufuli ambaye ametimiza miaka miwili tangu achaguliwe kuwa Rais wa Tanzania amesema ndege zote sita zilizonunuliwa na Serikali zitakuja.

No comments:

Post a Comment