Thursday, October 5, 2017

IGP SIRRO AUNDA KAMATI YA KUCHUNGUZA MIILI ILIYOOKOTWA BAHAHIRI

Inspekta Jenerali wa Polisi, Simon Sirro amesema wameunda timu ya wataalamu kuchunguza miili iliyookotwa na sampuli kutoka miili hiyo zimechukuliwa.
Amesema iwapo kuna watu ambao ndugu zao wamepotea ni vyema wakafika katika ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) kwa ajili ya vipimo na kufanyika upelelezi.
 “Bahari ni kubwa inapita katika nchi nyingi na inachukua kila kitu, haya mambo yanapotokea hata nchi nyingine yanatokea, kwa hiyo kimsingi tumeunda timu ya wataalamu ya kupeleleza kuhusu miili hii, wamechukua majimaji kutoka mwilini,” alisema.
 IGP Sirro alisema, “Kama kuna mtu ambaye ndugu yake amepotea afike makao makuu ya Polisi upande wa DCI tuweze kufanya uchunguzi kuona kama ni ndugu yake.”
 Alisema miili hiyo haijabainika kuwa ni ya watu wa Taifa gani.
 “Tatizo letu Watanzania ni kwamba moja kwa moja wanaanza kuhisi, sijui kwa nini tunakuwa tunaishi kwa hisia na hii hisia hisia si nzuri, tuseme kitu tukiwa na uhakika. Ikitokea jambo utasema ni Sirro, utasema ni nani, hii si nzuri na niwaambie tumwogope Mungu pia,” alisema IGP Sirro.


No comments:

Post a Comment